Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. John Pombe Magufuli, tarehe 06/04/2019 amezindua Mradi wa kusafirisha umeme wa kilovolti 220 kutoka Makambako hadi Songea. Jumla ya wateja wa awali 22,700 wanatarajiwa kuunganishiwa na huduma ya umeme kupitia Mradi huu kwenye vijiji 122.
Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umezindua utekelezaji wa Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu katika Mkoa wa Pwani uliofanyika tarehe 13/03/2017 katika kijiji cha Msufini Wilaya ya Kibaha.
The Rural Energy Agency now invites eligible consulting firms to express interests in providing the Technical Assistance (TA) to implement “off-grid” renewable energy (RE) rural electrification programs.
Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Prof. Sospeter Muhongo, ametaja miradi ya kipaumbele itakayotoa matokeo ya haraka ifikapo 2015/2016, na kunufaisha wananchi katika mikoa mbalimbali nchini. Prof. Muhongo aliitaja miradi hiyo mikubwa jijini Dar es Salaam mbele ya wadau waliokusanyika katika kongamano la wazi la siku moja kwa lengo la kukusanya maoni kuhusu utekelezaji wa miradi hiyo.