Register
Login
Home
News Center
Announcements
Tenders & Business
Events
Events Calendar
Projects
The Rural Energy Fund
Resources
E-Library
Application Forms
LRTC2014 Online Proposal Form
RBF Online Grant Application Form
About Us
About REA
Organization Structure
The Rural Energy Board
Contact Us
News Center
Announcements
Announcements
Failed to load licensing components. Please Repair / Re-Install Dixit . DO NOT UNINSTALL MODULE!
Bodi ya Nishati Vijijini Yapongeza Uzalishaji wa Vifaa vya Miradi ya Umeme
Tuesday, July 30, 2019
|
Number of views (7242)
|
Categories:
News
,
Announcements
Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini, Wakili Julius Kalolo amevipongeza viwanda vinavyotengeneza vifaa vinavyotumika katika ujenzi wa miundombinu ya miradi ya usambazaji wa umeme vijijini kwa uzalishaji wa vifaa kwa kiwango kikubwa unaochochea ukuaji wa sekta ya nishati nchini.
Bodi ya Nishati Vijijini (REB) ilifanya ziara ya kutembelea viwanda vinavyotengeneza vifaa vinavyotumika katika ujenzi wa miundombinu ya miradi ya usambazaji wa umeme vijijini katika mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Njombe na Iringa ili kujionea shughuli za uzalishaji vifaa hivyo.
Katika ziara hiyo, wamiliki wa viwanda vya vifaa vya umeme wameahidi kuendelea kuzalisha vifaa hivyo kwa kiwango kikubwa ili kukidhi mahitaji ya miradi ya umeme nchini.
Wakili Kalolo alisema ameridhishwa na kasi ya uzalishaji wa vifaa katika viwanda hivyo na kusisitiza umuhimu wake katika kufanikisha kazi kubwa ya utekelezaji wa miradi ya nishati vijijni ambayo inaendelea nchini, ambapo mpaka sasa ni vijiji 7400 kati ya 12,268 vimeunganishwa na huduma ya umeme.
“Ziara hii imetusaidia kujua changamoto wanazokumbana nazo wazalishaji wa vifaa vya umeme, lakini pia naweza kuthibitisha uwezo wao baada ya kutembelea viwanda hivi, ni wazi kwamba suala la nguzo za umeme tunajitosheleza kwa viwanda vyetu, suala la mita na waya sio changamoto, vyote vinazalishwa ndani ya nchi”, aliongeza Wakili Kalolo.
Pia Wakili Kalolo amewapongeza wamiliki wa viwanda hivyo kwa kuajiri wafanyakazi wazawa kwa wingi na kuwataka kuendelea kuongeza wafanyakazi wanaopatikana hapa hapa nchini Tanzania. Wakili Kalolo aliongeza kusema kuwa, Serikali imetengeneza mazingira mazuri ya uwekezaji ili kuhakikisha kuwa juhudi za Rais John Magufuli kwamba Serikali itafikia uchumi wa kati kufikia Mwaka 2025.
Akielezea umuhimu wa viwanda hivyo katika utekelezaji wa miradi ya kusambaza umeme vijijini, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Amos Maganga amesema watengenezaji wa vifaa vinavyotumika katika miradi ya umeme, kama vile mita, waya, transfoma, nguzo na vingine vingi ni wadau muhimu sana katika kuleta mabadiliko chanya ya maendeleo vijijini kupitia nishati ya umeme.
Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la LAPF, Ghorofa ya 7
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507
Please
login
or
register
to post comments.
Search
Categories
RSS
Expand/Collapse
News
(101)
RSS
Expand/Collapse
Events
(26)
RSS
Expand/Collapse
Announcements
(95)
RSS
Expand/Collapse
Press Releases
(12)
RSS
Expand/Collapse
Reports
(9)
RSS
Expand/Collapse
Speeches
(3)
RSS
Expand/Collapse
Business
(61)
«
February 2023
»
Mon
Tue
Wed
Thu
Fri
Sat
Sun
30
31
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
Archive
2022, June
(1)
2022, February
(1)
2021, October
(1)
2021, September
(2)
2021, August
(1)
2021, June
(2)
2020, December
(2)
2020, September
(1)
2020, August
(2)
2020, April
(1)
2020, January
(2)
2019, November
(2)
2019, October
(2)
2019, September
(2)
2019, August
(1)
2019, July
(3)
2019, June
(2)
2019, May
(1)
2019, April
(1)
2019, March
(1)
2019, February
(2)
2018, December
(2)
2018, November
(1)
2018, August
(1)
2018, June
(2)
2018, May
(3)
2018, April
(3)
2018, March
(3)
2017, December
(1)
2017, November
(1)
2017, October
(2)
2017, June
(1)
2017, May
(3)
2017, April
(1)
2017, February
(2)
2017, January
(1)
2016, December
(1)
2016, November
(1)
2016, October
(1)
2016, September
(1)
2016, August
(2)
2016, July
(3)
2016, June
(1)
2016, May
(1)
2016, April
(1)
2016, March
(3)
2016, February
(2)
2016, January
(2)
2015, December
(1)
2015, August
(1)
2015, March
(2)
2014, December
(1)
2014, October
(1)
2014, August
(1)
2014, May
(1)
2014, January
(1)
2013, December
(1)
2013, July
(1)
2013, June
(2)
2013, May
(3)
2012, September
(1)
2012, March
(1)
2011, December
(1)