Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Yaendelea Kuhamasisha Matumizi ya Nishati Safi Mbeya Vijijini
Frank A. Mugogo 657

REA Yaendelea Kuhamasisha Matumizi ya Nishati Safi Mbeya Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unaendelea zoezi la kuhamasisha na kutoa elimu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ambapo Wananchi wa kijiji cha jojo, kata ya Santilya, tarafa ya Isangati, Halmashauri ya Mbeya vijijini, wamefikiwa na huduma hiyo kupitia maonesho maalum yaliyopewa jina la Wakulima Festival.

Akifungua maonesho hayo, tarehe 27 Aprili, 2025, Naibu Waziri wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Maryprisca Mahundi amepongeza juhudu zinazofanywa na Wakala wa Nishati Vjijini (REA) katika kuwafikia Wananchi wa vijijini hususan katika kuhamasisha na kuelimisha kuhusu matumizi ya teknolojia za nishati safi ya kupikia katika kulinda afya za Watu, kulinda na kutunza mzingira pamoja na kusambaza teknolojia hizo.

“Naipongeza REA kwa kufika hapa kata ya Santilya, kijiji cha Jojo, ili kuhamasisha na kuelimisha Wananchi kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia, mmetoka mijini na mmekuja vijijini”…

“Matumizi ya nishati safi, ni kampeni maalum ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa lengo la kumpunguzia Mwanamke mzigo mkubwa wa kupika kwa kuni pamoja na athari za kiafya na kimazingira ili pia ashiriki kwenye shughuli nyengine za maendeleo”. Alisema Naibu Waziri, Mhandisi, Maryprisca Mahundi.

Awali, akimkaribisha kwenye banda la REA, Mhandisi Miradi ya Nishati Safi kutoka REA, Raya Majallah alisema, REA imeendelea kutekeleza Miradi ya kusambaza nishati mbalimbali vijijini na baada ya kutekeleza jukumu la kusambaza umeme kwenye vijiji vyote vya Tanzania Bara, sasa msukumo umewekwa kwenye kusambaza umeme kwenye vitongoji pamoja na kusambazaji wa Miradi ya nishati safi ya kupikia, ambapo Mradi wa kusambaza majiko banifu, mitungi ya gesi na majiko yake pamoja na kutoa mikopo mafuu ya ujenzi wa vituo vidogo vya kusambaza bidhaa za mafuta ya petrol na dizeli inaendelea kutekelezwa kikamilifu.

“REA kwa kushirikiana na Wadau (Sekta Binafsi) tumefika hapa kijiji cha Jojo ili kuelimisha na kuhamashisha matumizi ya nishati safi, na kwa kuwa umeme upo kijijini, tunahamasisha matumizi ya majiko ya umeme yanayotumia umeme kidogo (Yanayotumia uniti 1 kwa saa) pamoja na majiko banifu yanayotumia mkaa au kuni kidogo”. Amesema, Mhandisi, Raya Majallah.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma
 

Share

Print
«September 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
31123456
789
Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

IRINGA, Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini kwa kuendesha mafunzo maalum ya wiki moja yaliyolenga kujenga uwezo wa waendelezaji wa miradi midogo ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower).

Mafunzo hayo yaliyoanza tarehe 7 Septemba, 2026 katika Hoteli ya Sunset mkoani Iringa, yamewakutanisha waendelezaji wa miradi (Developers) zaidi ya 15, hususan kutoka maeneo ya Nyanda za Juu Kusini. Lengo kuu ni kuwajengea uwezo wa kiufundi ili kuongeza ubora wa miradi yao ili iweze kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, tarehe 9 Septemba, 2026, Kaimu Meneja wa Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi kutoka REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya, alisema kuwa REA haishii tu kutoa msaada wa upatikanaji wa nishati vijijini, bali inajikita pia katika kuongeza ujuzi wa wataalamu wa ndani.

"Kuongeza ujuzi kwa waendelezaji hawa kutasaidia kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu na ubora unaohitajika. Hatua hii itaongeza idadi ya miradi inayofikia vigezo vya kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa, kuongeza uzalishaji wa umeme, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii vijijini," alisema Mhandisi Yesaya.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ushirikiano kati ya REA na Wataalamu kutoka Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia (CoET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Maeneo yaliyofundishwa ni pamoja na usanifu wa miradi, upembuzi yakinifu, sayansi ya maji (hydrology), uhandisi wa umeme na elektroniki, pamoja na uendeshaji na matengenezo ya mitambo.

Mbali na mafunzo, REA imebainisha kuwa imekuwa ikisaidia waendelezaji hao kupitia ruzuku za ujenzi, maandalizi ya maandiko ya miradi na usanifu.

Aidha, Wakala huo upo katika mchakato wa kuandaa mfumo wa mikataba ya muda mrefu (Framework Contract) na taasisi za elimu ili kutoa mafunzo endelevu kwenye nishati jadidifu ikiwemo nishati ya jua na mifumo ya gesi vunde.

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wamepongeza mafunzo hayo; akizungumza na Wanahabari, Mhandisi Denis Makoyi kutoka kampuni ya Africa Power Investment, alisema mafunzo hayo yameongeza uelewa mkubwa wa kiufundi katika hatua za utekelezaji wa miradi. Naye Lutengano Kigola kutoka mradi wa Nyalawa Hydropower, aliongeza kuwa mafunzo hayo yanathibitisha kuwa Tanzania ina wataalamu wa ndani wenye uwezo mkubwa wa kuendeleza miradi ya umeme wa maji.

  • MWISHO –

 

Read more
10111213
14
REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuwezesha waendelezaji wadogo wa miradi ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kwa kutoa fedha, msaada wa kitaalamu na mafunzo, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa nishati nchini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top