Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Yaendelea Kuhamasisha Matumizi ya Nishati Safi Mbeya Vijijini
Frank A. Mugogo 125

REA Yaendelea Kuhamasisha Matumizi ya Nishati Safi Mbeya Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unaendelea zoezi la kuhamasisha na kutoa elimu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ambapo Wananchi wa kijiji cha jojo, kata ya Santilya, tarafa ya Isangati, Halmashauri ya Mbeya vijijini, wamefikiwa na huduma hiyo kupitia maonesho maalum yaliyopewa jina la Wakulima Festival.

Akifungua maonesho hayo, tarehe 27 Aprili, 2025, Naibu Waziri wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Maryprisca Mahundi amepongeza juhudu zinazofanywa na Wakala wa Nishati Vjijini (REA) katika kuwafikia Wananchi wa vijijini hususan katika kuhamasisha na kuelimisha kuhusu matumizi ya teknolojia za nishati safi ya kupikia katika kulinda afya za Watu, kulinda na kutunza mzingira pamoja na kusambaza teknolojia hizo.

“Naipongeza REA kwa kufika hapa kata ya Santilya, kijiji cha Jojo, ili kuhamasisha na kuelimisha Wananchi kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia, mmetoka mijini na mmekuja vijijini”…

“Matumizi ya nishati safi, ni kampeni maalum ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa lengo la kumpunguzia Mwanamke mzigo mkubwa wa kupika kwa kuni pamoja na athari za kiafya na kimazingira ili pia ashiriki kwenye shughuli nyengine za maendeleo”. Alisema Naibu Waziri, Mhandisi, Maryprisca Mahundi.

Awali, akimkaribisha kwenye banda la REA, Mhandisi Miradi ya Nishati Safi kutoka REA, Raya Majallah alisema, REA imeendelea kutekeleza Miradi ya kusambaza nishati mbalimbali vijijini na baada ya kutekeleza jukumu la kusambaza umeme kwenye vijiji vyote vya Tanzania Bara, sasa msukumo umewekwa kwenye kusambaza umeme kwenye vitongoji pamoja na kusambazaji wa Miradi ya nishati safi ya kupikia, ambapo Mradi wa kusambaza majiko banifu, mitungi ya gesi na majiko yake pamoja na kutoa mikopo mafuu ya ujenzi wa vituo vidogo vya kusambaza bidhaa za mafuta ya petrol na dizeli inaendelea kutekelezwa kikamilifu.

“REA kwa kushirikiana na Wadau (Sekta Binafsi) tumefika hapa kijiji cha Jojo ili kuelimisha na kuhamashisha matumizi ya nishati safi, na kwa kuwa umeme upo kijijini, tunahamasisha matumizi ya majiko ya umeme yanayotumia umeme kidogo (Yanayotumia uniti 1 kwa saa) pamoja na majiko banifu yanayotumia mkaa au kuni kidogo”. Amesema, Mhandisi, Raya Majallah.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma
 

Share

Print
«August 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
28293031123
45
Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

The Rural Energy Agency (REA) is seeking proposals from qualified service providers for the supply, installation, and testing of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in eight remote villages across Geita, Ludewa and Mbulu districts. Those villages are located in remote areas with challenging geographical conditions, hence, impractical for grid extension.

Please find the attached documents:

•    Application Form for Supply and Installation of SA-SHS; and
•    Call for Proposals for Result Based Financing Installation of Stand Alone Solar Home Systems.

Read more
678910
111213
Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Wananchi Kijiji cha Usevya Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi wamepongeza hatua zinazochukuliwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kuhakikisha wanafikiwa na nishati safi ya kupikia kwa bei ya ruzuku.

Read more
1415
Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetoa wito kwa viongozi wa dini nchini kushiriki kikamilifu katika kampeni ya kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa lengo la kulinda afya na kuokoa mazingira.

Read more
1617
181920
Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Watanzania wameendelea kuhamasishwa kutumia nishati safi ya kupikia ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Read more
21222324
25262728293031
1234567

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top