Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Yaendelea Kuhamasisha Matumizi ya Nishati Safi Mbeya Vijijini
Frank A. Mugogo 90

REA Yaendelea Kuhamasisha Matumizi ya Nishati Safi Mbeya Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unaendelea zoezi la kuhamasisha na kutoa elimu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ambapo Wananchi wa kijiji cha jojo, kata ya Santilya, tarafa ya Isangati, Halmashauri ya Mbeya vijijini, wamefikiwa na huduma hiyo kupitia maonesho maalum yaliyopewa jina la Wakulima Festival.

Akifungua maonesho hayo, tarehe 27 Aprili, 2025, Naibu Waziri wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Maryprisca Mahundi amepongeza juhudu zinazofanywa na Wakala wa Nishati Vjijini (REA) katika kuwafikia Wananchi wa vijijini hususan katika kuhamasisha na kuelimisha kuhusu matumizi ya teknolojia za nishati safi ya kupikia katika kulinda afya za Watu, kulinda na kutunza mzingira pamoja na kusambaza teknolojia hizo.

“Naipongeza REA kwa kufika hapa kata ya Santilya, kijiji cha Jojo, ili kuhamasisha na kuelimisha Wananchi kuhusu matumizi ya nishati safi ya kupikia, mmetoka mijini na mmekuja vijijini”…

“Matumizi ya nishati safi, ni kampeni maalum ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa lengo la kumpunguzia Mwanamke mzigo mkubwa wa kupika kwa kuni pamoja na athari za kiafya na kimazingira ili pia ashiriki kwenye shughuli nyengine za maendeleo”. Alisema Naibu Waziri, Mhandisi, Maryprisca Mahundi.

Awali, akimkaribisha kwenye banda la REA, Mhandisi Miradi ya Nishati Safi kutoka REA, Raya Majallah alisema, REA imeendelea kutekeleza Miradi ya kusambaza nishati mbalimbali vijijini na baada ya kutekeleza jukumu la kusambaza umeme kwenye vijiji vyote vya Tanzania Bara, sasa msukumo umewekwa kwenye kusambaza umeme kwenye vitongoji pamoja na kusambazaji wa Miradi ya nishati safi ya kupikia, ambapo Mradi wa kusambaza majiko banifu, mitungi ya gesi na majiko yake pamoja na kutoa mikopo mafuu ya ujenzi wa vituo vidogo vya kusambaza bidhaa za mafuta ya petrol na dizeli inaendelea kutekelezwa kikamilifu.

“REA kwa kushirikiana na Wadau (Sekta Binafsi) tumefika hapa kijiji cha Jojo ili kuelimisha na kuhamashisha matumizi ya nishati safi, na kwa kuwa umeme upo kijijini, tunahamasisha matumizi ya majiko ya umeme yanayotumia umeme kidogo (Yanayotumia uniti 1 kwa saa) pamoja na majiko banifu yanayotumia mkaa au kuni kidogo”. Amesema, Mhandisi, Raya Majallah.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma
 

Share

Print
«May 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
2829301234
567891011
12131415
Zaidi ya Bilioni 17 Kusambaza Umeme Vitongojini Singida

Zaidi ya Bilioni 17 Kusambaza Umeme Vitongojini Singida

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa Shilingi Bilioni 17.39 wa kusambaza umeme katika vitongoji 120 utakaonufaisha Kaya 3,960 Mkoani Singida.

Read more
16
Mkurugenzi Mkuu REA Aisisitiza Bodi Mpya ya Zabuni Kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu

Mkurugenzi Mkuu REA Aisisitiza Bodi Mpya ya Zabuni Kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy ameielekeza Bodi mpya ya Zabuni (Tender Board) ya Wakala kuhakikisha inatekeleza majukumu yake kwa kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu ili kuleta tija katika kazi zake.

Read more
1718
19
Benki ya Dunia Yaridhishwa na Utekelezwaji wa Miradi ya REA

Benki ya Dunia Yaridhishwa na Utekelezwaji wa Miradi ya REA

Benki ya Dunia (WB) yaihakikishia ushirikiano Serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika utekelezaji wa miradi ya Nishati kote nchini kwa ulinzi wa mazingira na ustawi wa Taifa kwa ujumla.

Read more
202122
Rais Samia Apeleka Neema Tanga

Rais Samia Apeleka Neema Tanga

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unatekeleza mradi wa Shilingi Bilioni 20 wa kusambaza umeme katika vitongoji 180 utakaonufaisha zaidi ya Kaya 5,940 Mkoani Tanga.

Read more
232425
2627282930311
2345678

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top