Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unaendelea zoezi la kuhamasisha na kutoa elimu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ambapo Wananchi wa kijiji cha jojo, kata ya Santilya, tarafa ya Isangati, Halmashauri ya Mbeya vijijini, wamefikiwa na huduma hiyo kupitia maonesho maalum yaliyopewa jina la Wakulima Festival.