Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
KIPAUMBELE CHA SERIKALI KATIKA KUSAMBAZA NISHATI VIJIJINI NI KUPELEKA UMEME KATIKA VITONGOJI
Admin.Frank Mugogo 3719

KIPAUMBELE CHA SERIKALI KATIKA KUSAMBAZA NISHATI VIJIJINI NI KUPELEKA UMEME KATIKA VITONGOJI

Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt Medard Kalemani amesema kipaumbele cha Serikali katika kusambaza nishati vijijini ni kupeleka umeme katika vitongoji.

Waziri Kalemani alisema hayo tarehe 11 Disemba 2020 katika ukumbi wa mikutano wa PSSF uliopo jijini Dodoma wakati akiongea na Menejimenti za Wizara ya Nishati na Taasisi zake. “Tunahitaji kupeleka umeme katika vitongoji vyote, siku hizi watu hawaulizi tena vijiji. Vitongoji viwe kipaumbele sasa” alisema.

Aidha, Mhe Waziri wa Nishati aliwapongeza REA kwa kazi nzuri ya kusambaza umeme vijijini na kuwataka wailinde imani ambayo wamepewa na wananchi kwa kuchapa kazi kwa kasi, ubunifu na usahihi. “Tunawapongeza mmefanya kazi nzuri sana, kupeleka umeme vijijini ni sacrifice, unapeleka nguzo 100 unapata wateja wanne, lakini baada ya miezi sita wateja wanaongezeka. Lazima tukubaliane kufanya kazi mara dufu ya miaka mitano iliyopita na kwa kushirikiana”, alisema.

Naye Naibu Waziri, Mhe. Stephen Byabato alisisitiza ushirikiano katika kazi na kutoa elimu kwa umma kuhusu mafanikio ya miradi inayotekelezwa na Serikali.

Baada ya kukutana na Menejimenti za Wizara ya Nishati, Waziri wa Nishati pamoja na Naibu wake walikutana na Bodi za Wakurugenzi wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ambapo katika kikao hicho, Mhe. Waziri aliagiza kila taasisi iwasilishe mpango ambao unaainisha vipaumbele, changamoto pamoja na ufumbuzi wake.

Aidha, Mhe. Waziri wa Nishati alizitaka Bodi hizo kusimamia mpango kazi huo na kuwachukulia hatua watumishi ambao hawatimizi wajibu wao.

Akipokea maagizo hayo, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Wakili Julius Kalolo aliahidi kutoa ushirikiano kwa Waziri na Naibu wake na kuwa watahakikisha maelekezo waliyotoa yanatekelezwa.


Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz

Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top