Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
KIPAUMBELE CHA SERIKALI KATIKA KUSAMBAZA NISHATI VIJIJINI NI KUPELEKA UMEME KATIKA VITONGOJI
Admin.Frank Mugogo 3735

KIPAUMBELE CHA SERIKALI KATIKA KUSAMBAZA NISHATI VIJIJINI NI KUPELEKA UMEME KATIKA VITONGOJI

Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt Medard Kalemani amesema kipaumbele cha Serikali katika kusambaza nishati vijijini ni kupeleka umeme katika vitongoji.

Waziri Kalemani alisema hayo tarehe 11 Disemba 2020 katika ukumbi wa mikutano wa PSSF uliopo jijini Dodoma wakati akiongea na Menejimenti za Wizara ya Nishati na Taasisi zake. “Tunahitaji kupeleka umeme katika vitongoji vyote, siku hizi watu hawaulizi tena vijiji. Vitongoji viwe kipaumbele sasa” alisema.

Aidha, Mhe Waziri wa Nishati aliwapongeza REA kwa kazi nzuri ya kusambaza umeme vijijini na kuwataka wailinde imani ambayo wamepewa na wananchi kwa kuchapa kazi kwa kasi, ubunifu na usahihi. “Tunawapongeza mmefanya kazi nzuri sana, kupeleka umeme vijijini ni sacrifice, unapeleka nguzo 100 unapata wateja wanne, lakini baada ya miezi sita wateja wanaongezeka. Lazima tukubaliane kufanya kazi mara dufu ya miaka mitano iliyopita na kwa kushirikiana”, alisema.

Naye Naibu Waziri, Mhe. Stephen Byabato alisisitiza ushirikiano katika kazi na kutoa elimu kwa umma kuhusu mafanikio ya miradi inayotekelezwa na Serikali.

Baada ya kukutana na Menejimenti za Wizara ya Nishati, Waziri wa Nishati pamoja na Naibu wake walikutana na Bodi za Wakurugenzi wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ambapo katika kikao hicho, Mhe. Waziri aliagiza kila taasisi iwasilishe mpango ambao unaainisha vipaumbele, changamoto pamoja na ufumbuzi wake.

Aidha, Mhe. Waziri wa Nishati alizitaka Bodi hizo kusimamia mpango kazi huo na kuwachukulia hatua watumishi ambao hawatimizi wajibu wao.

Akipokea maagizo hayo, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Wakili Julius Kalolo aliahidi kutoa ushirikiano kwa Waziri na Naibu wake na kuwa watahakikisha maelekezo waliyotoa yanatekelezwa.


Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz

Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«July 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
30
REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

Serikali imesambaza kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza (Gereza la Ukonga) mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko yake 464 ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kama njia ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia nchini ambapo msisitizo ni angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia Nishati Safi ifikapo Mwaka 2034.

Read more
1
Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa vitendo.

Read more
2
REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

Katika kuendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imegawa jumla ya mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko ya sahani mbili 461 kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Mara.

Read more
3
REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mpango wa kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petrol na dizeli) maeneo ya vijijini ili kuondoa madhara yatokanayo na njia zisizo salama.

Read more
4
Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewasihi Watanzania kote nchini kuachana na dhana ya kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni gharama ikilinganishwa na matumizi ya kuni na mkaa.

Read more
5
Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Imeelezwa kuwa hadi kufikia mwaka 2030 vitongoji vyote Tanzania Bara vitakuwa vimefikishiwa nishati ya umeme kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa na kusimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Read more
6
78
REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema Wakala umejizatiti kuhakikisha 80% ya Watanzania wanatumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo mwaka 2034 kama ilivyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
910111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top