Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
KIPAUMBELE CHA SERIKALI KATIKA KUSAMBAZA NISHATI VIJIJINI NI KUPELEKA UMEME KATIKA VITONGOJI
Admin.Frank Mugogo 3714

KIPAUMBELE CHA SERIKALI KATIKA KUSAMBAZA NISHATI VIJIJINI NI KUPELEKA UMEME KATIKA VITONGOJI

Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt Medard Kalemani amesema kipaumbele cha Serikali katika kusambaza nishati vijijini ni kupeleka umeme katika vitongoji.

Waziri Kalemani alisema hayo tarehe 11 Disemba 2020 katika ukumbi wa mikutano wa PSSF uliopo jijini Dodoma wakati akiongea na Menejimenti za Wizara ya Nishati na Taasisi zake. “Tunahitaji kupeleka umeme katika vitongoji vyote, siku hizi watu hawaulizi tena vijiji. Vitongoji viwe kipaumbele sasa” alisema.

Aidha, Mhe Waziri wa Nishati aliwapongeza REA kwa kazi nzuri ya kusambaza umeme vijijini na kuwataka wailinde imani ambayo wamepewa na wananchi kwa kuchapa kazi kwa kasi, ubunifu na usahihi. “Tunawapongeza mmefanya kazi nzuri sana, kupeleka umeme vijijini ni sacrifice, unapeleka nguzo 100 unapata wateja wanne, lakini baada ya miezi sita wateja wanaongezeka. Lazima tukubaliane kufanya kazi mara dufu ya miaka mitano iliyopita na kwa kushirikiana”, alisema.

Naye Naibu Waziri, Mhe. Stephen Byabato alisisitiza ushirikiano katika kazi na kutoa elimu kwa umma kuhusu mafanikio ya miradi inayotekelezwa na Serikali.

Baada ya kukutana na Menejimenti za Wizara ya Nishati, Waziri wa Nishati pamoja na Naibu wake walikutana na Bodi za Wakurugenzi wa Taasisi zilizo chini ya Wizara ambapo katika kikao hicho, Mhe. Waziri aliagiza kila taasisi iwasilishe mpango ambao unaainisha vipaumbele, changamoto pamoja na ufumbuzi wake.

Aidha, Mhe. Waziri wa Nishati alizitaka Bodi hizo kusimamia mpango kazi huo na kuwachukulia hatua watumishi ambao hawatimizi wajibu wao.

Akipokea maagizo hayo, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Wakili Julius Kalolo aliahidi kutoa ushirikiano kwa Waziri na Naibu wake na kuwa watahakikisha maelekezo waliyotoa yanatekelezwa.


Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz

Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top