Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Yaridhishwa na Usambazaji wa Umeme Kisiwani Jibondo
Newsletters

Bilioni 8 zatumika

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Yaridhishwa na Usambazaji wa Umeme Kisiwani Jibondo

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) imeeleza kuridhishwa kwake na kasi ya usambazaji wa nishati ya umeme katika vitongoji vya Kisiwa cha Jibondo, kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mafia, mkoani Pwani.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa REB, Mhe. Balozi na Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu, tarehe 27 Agosti, 2026 alipoambatana na Menejimenti ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kisiwani humo kukagua maendeleo ya mradi huo mkubwa ambao tayari umegharimu kiasi cha shilingi bilioni 8.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Meja Jenerali Kingu amesema kuwa kwa mara ya kwanza katika historia, vitongoji vya Kisiwa cha Jibondo vinatarajia kupata huduma hiyo ya nishati hivi karibuni. Alifafanua kuwa kazi kubwa iliyobaki kwa sasa ni ya usafirishaji wa umeme kwa kutumia waya maalum wa chini ya maji (Submarine cable) kutoka kisiwa kidogo cha Juani kwenda Jibondo, kazi inayotarajiwa kuanza kesho, tarehe 29 Agosti 2026, na kukamilika baada ya siku tano.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy, amesema kuwa maandalizi yote ya miundombinu ikiwemo ujenzi wa njia za kusafirisha umeme ndani ya kisiwa hicho yamekamika kwa asilimia 90 na ameongeza kuwa mara baada ya nyaya hizo za chini ya maji kuunganishwa, wananchi wataanza kuunganishiwa huduma hiyo mara moja.

Mhandisi Saidy amebainisha kuwa mradi huo umefanikiwa kwa ushirikiano wa REA iliyochangia shilingi bilioni 6.8 na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) lililochangia shilingi bilioni 2.

Katika hatua nyingine, Mhandisi Saidy ametoa wito kwa wakazi wa Jibondo kujiandaa kiuchumi ili kuutumia umeme huo katika kuboresha maisha yao na kuendesha shughuli za kimaendeleo, hasa ikizingatiwa kuwa sehemu kubwa ya wakazi wa eneo hilo wamejiajiri kwenye sekta za uvuvi, usindikaji wa mazao ya bahari, na kilimo cha mwani.

Wilaya ya Mafia ina jumla ya vitongoji 136, ambapo vitongoji 111 tayari vimeshafikishiwa huduma ya umeme. Vitongoji vingine 19 vipo kwenye mpango wa utekelezaji kupitia Mradi wa HEP II (B), huku vitongoji 6 vilivyobaki vikiwa ni hivyo vya Kisiwa cha Jibondo vinavyosubiri kuwashwa kwa umeme huo hivi karibuni.

Naye mmoja wa wakazi wa kisiwa hicho, Mzee Abdalah Hassan, ameishukuru Serikali kwa uwekezaji huo mkubwa na kueleza kuwa umeme huo utakuwa mkombozi mkubwa kwao.

"Umeme unahitajika kila mahali. Shuleni utasaidia kuchapisha mitihani na kujifunza kwa njia ya kompyuta, lakini pia utatupa wepesi wa kuandaa chakula na kuleta mwanga majumbani. Tumefarijika sana, ni faraja kubwa isiyo na kifani," amesema Mzee Abdalah.

-         MWISHO –

 

 

Mkaa Mbadala Mkombozi Matumizi ya Nishati kwa Watanzania
Newsletters

Ni kuelekea asilimia 80 ya Watanzania kutumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034

Mkaa Mbadala Mkombozi Matumizi ya Nishati kwa Watanzania

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeendelea kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kutumia teknolojia mbalimbali ikiwemo matumizi ya mkaa mbadala unaozalishwa nchini ili kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034 kulingana na Mkakati wa Kitaifa wa Matumizi ya nishati safi hapa nchini.

Wito huo umetolewa leo Februari 28, 2026 na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu akiwa ameongoza na Menejimenti ya REA wakati walipotembelea kiwanda cha Shirika la Mzinga kujionea kuhusu uzalishaji wa teknolojia ya mkaa mbadala unaofanywa na Shirika hilo mkoani Morogoro.

Balozi Meja Jenerali Mstaafu Kingu ameeleza kuwa Serikali kupitia REA imehamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia ili kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia katika ajenda ya Kitaifa ya nishati safi ya kupikia katika kuwawezesha Watanzania wanatumia nishati hiyo ifikapo mwaka 2034.

"Matumizi ya mkaa mbadala yatatuwezesha kuweza kufikia asilimia 80 ya watanzania kutumia nishati safi ifikapo mwaka 2034. Ni lazima tuipe nguvu ajenda hii kwa kuwa inakwenda kuwa mkombozi kwa nchi yetu, " Ameongeza Balozi Kingu.

Kwa upande wake, Brigedia Jenerali Seif Hamisi ambaye ni Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Mzinga ameishukuru REA kwa fursa hiyo ya kuwatembelea katika kiwanda chao cha Mzinga na kujionea namna uzalishaji wa mkaa mbadala unavyofanywa na kiwanda hicho mkoani humo.

Amesema, ni matarajio yao kuwa kiwanda hicho kinakwenda kukidhi mahitaji ya watumiaji wa mkaa mbadala kwa kuwa kwa sasa wanaendelea kufanya tafiti na kuzungumza na wadau mbalimbali ikiwemo REA ili kuhakikisha wanapata teknolojia za kisasa zitakazowezesha kuanza kuzalisha mkaa huo kwa wingi.

Kwa upande wake, Msimamizi wa Mradi wa mkaa mbadala katika kiwanda cha Mzinga Mha. Amiri Msangi, ameeleza kuwa kwa sasa kiwanda kinaendekea kufanya tafiti wa teknolojia  teknolojia bora na rafiki ya uzalishaji wa mkaa mbadala ili uzalishaji utakapoanza na kuwa mkubwa uweze kuleta tija kwa Watanzania na kuongeza kipato kwa shirika.

Mwisho.

RSS
«September 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
31123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top