Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Bodi ya Nishati Vijijini (REB) yaridhishwa na Usambazaji wa Gesi Asilia mkoani Pwani
National

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) yaridhishwa na Usambazaji wa Gesi Asilia mkoani Pwani

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) yaridhishwa na Usambazaji wa Gesi Asilia mkoani Pwani

Utekelezaji wa mradi wa kusambaza gesi asili katika eneo la Kisemvule, wilayani Mkuranga mkoani Pwani, umeendelea kuibua matumaini mapya kwa Wananchi wa eneo hilo ambapo zaidi ya shilingi bilioni 6.8 zimewekezwa katika kusambaza gesi asilia katika maeneo yaliyopitiwa na mkuza wa bomba la gesi asilia.

Mradi huo umejengwa na Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) na kufadhiliwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeelezwa kuwa ni sehemu ya mkakati wa Serikali ya Awamu ya Sita wa kuhakikisha ifikapo mwaka 2034 asilimia 80 ya Watanzania watakuwa wanatumia nishati safi ya kupikia.

Akizungumza baada ya kutembelea na kukagua Mradi huo; Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi na Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Kingu, amesema utekelezaji wa Mradi huo unaonesha dhamira ya dhati ya Serikali katika kuboresha maisha ya Wananchi na kulinda mazingira.

Amesema Bodi ya Nishati Vijijini inajivunia kuona mwitikio mkubwa wa Wananchi wanaendelea kuhamasika ili kuachana na matumizi ya kuni na mkaa na badala yake kutumia gesi asili, ambayo ni salama, nafuu na rafiki kwa mazingira.

“Huu ni Mradi wa kimkakati unaotekeleza maono ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuona Watanzania wengi wanatumia nishati safi, tunapaswa kulinda miundombinu hii kwa kuwa imegharimu fedha nyingi za Serikali,” amesema Balozi Kingu.

Kwa mujibu wa REA, mradi huo wa mfano ulilenga kuhudumia kaya 2,000 huku hadi sasa kaya 530 zikiwa zimefikiwa na huduma hiyo katika eneo la Kisemvule lenye wakazi zaidi ya 64,000 hali inayotoa fursa ya kupanua zaidi wigo wa huduma hiyo.

Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi, Hassan Saidy amesema taasisi hiyo imeiomba TPDC kufanya tathmini katika maeneo yenye idadi kubwa ya watu ambako bomba la gesi limepita ili kuanzisha miradi ya ubia itakayowezesha wananchi wengi zaidi kuunganishwa na huduma hiyo.

Ametaja baadhi ya maeneo yanayopendekezwa kuwa ni Mkuranga Mjini, Ikwiriri na Kilwa Kivinje, akibainisha kuwa hatua hiyo itaharakisha utekelezaji wa Sera ya Nishati Safi nchini.

Naye Mkurugenzi wa Nishati Jadidifu na Teknolojia za Nishati Mbadala kutoka REA, Mhandisi, Advera Mwijage amesema Bodi ya Nishati Vijijini imeagiza kuongeza kasi ya uunganishwaji wa kaya zaidi ili Mradi huo unufaishe Wananchi wengi zaidi kulingana na mahitaji halisi ya eneo hilo.

Kwa upande wake, Mhandisi, Tumaini Daniel, Meneja Mradi kutoka TPDC amesema Mradi huo umekamilika kwa mafanikio na umeweka msingi mzuri wa upanuzi wa huduma hiyo katika maeneo mengine yenye miundombinu ya bomba la gesi.

Wananchi wa Kisemvule wameanza kunufaika matokeo chanya ya Mradi huo, wakieleza kupungua kwa gharama za matumizi ya nishati na urahisi wa upatikanaji wa gesi asilia kupitia mifumo ya malipo ya simu.

Mradi huo unaendelea kuwa mfano wa utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Nishati Safi ukionesha namna uwekezaji wa kimkakati unavyoweza kubadilisha maisha ya Wanancha ili kulinda mazingira na kuchochea maendeleo ya kiuchumi katika ngazi ya jamii.

MWIS

RSS
«August 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
272829303112
3456789
1011121314
REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefanikiwa kusambaza takribani mitungi laki saba ya gesi ya kupikia (LPG) nchini kote, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa kasi wa Mkakati wa Kitaifa wa Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
1516
1718

Maombi ya Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unakaribisha waombaji wenye vigezo kuomba mkopo wa kuwezesha ujenzi wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) ili kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini.

Pamoja na tangazo hili, tumeweka viambatanisho vifuatavyo:
•    Tangazo la fursa ya mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta ya Petroli na Dizeli vijijini.
•    Mwongozo wa utoaji mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta vijijini.
•    Fomu ya Maombi ya Mkopo.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la REA
Mtaa wa Medeli
P. O. Box 2153,
DODOMA, TANZANIA.

Read more
1920212223
2425262728
Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Yaridhishwa na Usambazaji wa Umeme Kisiwani Jibondo

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Yaridhishwa na Usambazaji wa Umeme Kisiwani Jibondo

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) imeeleza kuridhishwa kwake na kasi ya usambazaji wa nishati ya umeme katika vitongoji vya Kisiwa cha Jibondo, kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mafia, mkoani Pwani.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa REB, Mhe. Balozi na Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu, tarehe 27 Agosti, 2026 alipoambatana na Menejimenti ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kisiwani humo kukagua maendeleo ya mradi huo mkubwa ambao tayari umegharimu kiasi cha shilingi bilioni 8.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Meja Jenerali Kingu amesema kuwa kwa mara ya kwanza katika historia, vitongoji vya Kisiwa cha Jibondo vinatarajia kupata huduma hiyo ya nishati hivi karibuni. Alifafanua kuwa kazi kubwa iliyobaki kwa sasa ni ya usafirishaji wa umeme kwa kutumia waya maalum wa chini ya maji (Submarine cable) kutoka kisiwa kidogo cha Juani kwenda Jibondo, kazi inayotarajiwa kuanza kesho, tarehe 29 Agosti 2026, na kukamilika baada ya siku tano.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy, amesema kuwa maandalizi yote ya miundombinu ikiwemo ujenzi wa njia za kusafirisha umeme ndani ya kisiwa hicho yamekamika kwa asilimia 90 na ameongeza kuwa mara baada ya nyaya hizo za chini ya maji kuunganishwa, wananchi wataanza kuunganishiwa huduma hiyo mara moja.

Mhandisi Saidy amebainisha kuwa mradi huo umefanikiwa kwa ushirikiano wa REA iliyochangia shilingi bilioni 6.8 na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) lililochangia shilingi bilioni 2.

Katika hatua nyingine, Mhandisi Saidy ametoa wito kwa wakazi wa Jibondo kujiandaa kiuchumi ili kuutumia umeme huo katika kuboresha maisha yao na kuendesha shughuli za kimaendeleo, hasa ikizingatiwa kuwa sehemu kubwa ya wakazi wa eneo hilo wamejiajiri kwenye sekta za uvuvi, usindikaji wa mazao ya bahari, na kilimo cha mwani.

Wilaya ya Mafia ina jumla ya vitongoji 136, ambapo vitongoji 111 tayari vimeshafikishiwa huduma ya umeme. Vitongoji vingine 19 vipo kwenye mpango wa utekelezaji kupitia Mradi wa HEP II (B), huku vitongoji 6 vilivyobaki vikiwa ni hivyo vya Kisiwa cha Jibondo vinavyosubiri kuwashwa kwa umeme huo hivi karibuni.

Naye mmoja wa wakazi wa kisiwa hicho, Mzee Abdalah Hassan, ameishukuru Serikali kwa uwekezaji huo mkubwa na kueleza kuwa umeme huo utakuwa mkombozi mkubwa kwao.

"Umeme unahitajika kila mahali. Shuleni utasaidia kuchapisha mitihani na kujifunza kwa njia ya kompyuta, lakini pia utatupa wepesi wa kuandaa chakula na kuleta mwanga majumbani. Tumefarijika sana, ni faraja kubwa isiyo na kifani," amesema Mzee Abdalah.

-         MWISHO –

 

 

Read more
2930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top