Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
MAONESHO YA SABASABA MWAKA 2023
Frank A. Mugogo 296

MAONESHO YA SABASABA MWAKA 2023

NISHATI YA KUPIKIA NI SEHEMU YA VIPAUMBELE VYA KITAIFA

Mkurugenzi wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA); Mhandisi, Francis Songela amesema Serikali kupitia REA imetoa kipaumbele kwenye kuongeza matumizi ya nishati safi na salama ya kupikia na kuongeza kuwa Wananchi wanapaswa kuchangamkia teknolojia mbalimbali kwa kuwa suala hilo lipo kwa ajili ya kulinda afya za Watu, kuboresha maisha yao hususan kwa Wananchi wa vijijini.

Mhandisi Songela ameyasema hayo hivi karibu wakati wa ziara yake kwenye maonesho ya kibiashara ya kimataifa ya Saba Saba na kuongeza kuwa REA itaendelea kutoa elimu na hamasa ya matumizi ya teknolojia mbalimbali ili kuhakikisha Wananchi wengi hususan wa vijijini wanaongeza matumizi ya majiko bora yanayotumia mkaa salama, gesi na Umeme kwa kiwango kidogo ili kulinda afya na mazingira yao.

Mhandisi Songela amesema, maonesho ya Saba Saba ni uwanja wa kutoa elimu pamoja na hamasa kwa Wananchi wengi wanaopata nafasi ya kutembelea na kusisitiza, REA itaendelea kuwashirikisha Wadau wengi ambao ni wagunduzi na waendelezaji wa teknolojia hizo ili kuhakikisha Watanzania wengi wanahamasika na kuanza kutumia teknojia hizo.

“Kwenye maonesho haya, tumeleta Wadau mbalimbali ambao tunashirikiana nao katika kusambaza teknolojia mbalimbali, kuna makampuni mbalimbali ambayo yanatengeza majiko bora ya kupikia, ambayo yanatumia umeme kidogo, hiyo ni fursa pia kwa Sekta Binafsi kuwekeza kwenye nishati ya kupikia”. Amesisitiza Mhandisi Songela.

Naye Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi, Mhandisi, Jones Olotu ametoa wito kwa Wananchi kuchangamkia fursa ya kuomba Mkopo wa Ujenzi na Uendeshaji Vituo Vidogo vya Mafuta Vijijini (Petroli na Dizeli) na kuongeza kuwa fursa ipo wazi na kusema mkopo huo ni wa riba nafuu ya asilimia tano (5) tu.

“Mwananchi, atakopeshwa fedha shilingi milioni 70, atakwenda kujenga kituo kidogo cha kuuza mafuta (Petroli au Dizeli), lakini pia Mkopaji atapewa mtaji wa kuweka mafuta kwa ajili ya kuendesha biashara hiyo, natoa wito kwa Watu wote wenye sifa, wachangamkie fursa hii. Mwisho wa kutuma maombi ya mkopo huo ni Tarehe 25 Agosti, 2023.” Alisisitiza Mhandisi, Olotu.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz

Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top