Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Kufunga Mifumo ya Nishati Safi ya Kupikia Shule ya Ruhinda
Frank A. Mugogo 95

REA Kufunga Mifumo ya Nishati Safi ya Kupikia Shule ya Ruhinda

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeahidi kujenga mifumo ya nishati safi ya kupikia pamoja na jiko katika shule ya Sekondari ya mchanganyiko ya Ruhinda iliyopo Wilaya ya Karagwe Mkoani Kagera.
 
Ahadi hiyo imetolewa leo Novemba 7, 2024 na Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy wakati wa muendelezo wa ziara ya viongozi mbalimbali wa Serikali waliambatana na Wabia hao wa Maendeleo ambao Serikali imekuwa ikishirikiana na kuwezesha upatikanaji wa nishati bora vijijini. Wabia hao ni Benki ya Dunia, Serikali ya Norway, Serikali ya Sweden, Umoja wa Ulaya, AFD na ADB.
 
Wakati wa ziara hiyo ambayo ililenga kutembelea miradi inayotekelezwa na Wakala huo, viongozi hao walitembelea Shule ya Sekondari ya Mchanganyiko ya Ruhinda ambapo katika risala yao, waliomba kupatiwa mfumo wa nishati safi ya kupikia.
 
“Tumeskia ombi lenu la kutamani kuwa na nishati safi ya kupikia hapa shuleni. Tutaenda kufanya tathmini na kuangalia nishati safi ipi itakayofaa zaidi. Tunaweza kuwa na mifumo hata miwili; mfumo wa gesi na mfumo wa majiko banifu ambayo yanatumia kuni kidogo na ni rafiki kwa mazingira.
 
Lakini pia kwa kuwa mifumo hii tunayotarajia kwenda kuifunga ni ya thamani na ya gharama kubwa. Pia tutawajengea na jengo la jiko zuri,” amesema Mkurugenzi Mkuu huyo.
 
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali (mstaafu), Jacob Kingu amesema Wakala huo umekuwa ukiishi kwa vitendo maelekezo ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk, Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni kinara wa nishati safi wa kupikia Afrika na Duniani kwa ujumla na kuongeza kuwa ujenzi wa mifumo ya kupikia katika shule hiyo ni kielelezo tosha cha utayari wa REA kupambana na nishati zisizo safi katika jamii.
 
“Tunajua shule ikibadilika kwa kutumia nishati safi ya kupikia hata wananchi wanaoizunguka shule hii pia watabadilika,” amesema Mwenyekiti Kingu.
 
Awali akisoma taarifa ya shule hiyo, Mkuu wa Shule hiyo, Ambruce Katorogo amesema kuwa shule hiyo inatumia Zaidi ya shilingi 800,000/= kila mwezi kwa ajili ya kununua kuni zinazotumika kupikia chakula cha wanafunzi shuleni hapo.
 
Awali Mkuu huyo wa shule pia aliishukuru Serikali kupitia REA kwa kuwezesha kufikisha nishati ya umeme katika shule hiyo ambapo imesaidia kuongeza usalama hasa kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum katika shule hiyo.
 
Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano kutoka REA, Bi. Martha Chassama ameendelea kuhamasisha wananchi kuendelea kutumia nishati safi ya kupikia na kusisitiza kuwa Wakala huo unaendelea na kampeni zake mbalimbali kuhamasisha wananchi wanajua madhara yatokanayo na nishati chafu ya kupikia.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627
Mhandisi Saidy Awapongeza Watumishi wa REA

Mhandisi Saidy Awapongeza Watumishi wa REA

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy amewapongeza Watumishi wa Wakala huo kwa kufanya kazi kwa bidii na kujituma hali iliyopelekea kukamilika kwa miradi inayotekelezwa na REA kwa wakati na katika ubora ulikusudiwa.

Read more
282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top