Bodi ya Nishati Vijijini (REB) pamoja na Menejimenti ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wamekutana na kufanya mazungumko na ujumbe kutoka nchini Algeria ukiongozwa na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya GISB Electric ambaye pia ni Makamu wa rais wa Kongani ya Viwanda vya Umeme Algeria (CIEL), Dk. Khelifa Mohammed.
Kikao hicho kilichofanyika leo Jijini Dar es Salaam, kililenga kubadilishana uzoefu pamoja na fursa za uwekezaji zilizopo katika sekta ya nishati. Kampuni ya GISB Electric ni moja kati ya kampuni kubwa Afrika ya uzalishaji wa vifaa vya umeme pamoja na ujenzi wa miundombinu ya umeme.