Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
BODI YA WAKURUGENZI YA REA WAKUTANA NA WAKANDARASI, PAMOJA NA WATENGENEZAJI WA VIFAA VYA MRADI WA UMEME VIJIJINI
Admin.Frank Mugogo 9715

BODI YA WAKURUGENZI YA REA WAKUTANA NA WAKANDARASI, PAMOJA NA WATENGENEZAJI WA VIFAA VYA MRADI WA UMEME VIJIJINI

1. Bodi ya Wakala wa Nishati Vijijini leo tarehe 08 Juni 2019 imekutana wa Wakandarasi wa Mradi wa REA Awamu ya III Mzunguko wa I katika Ukumbi wa Hazina, Dodoma kujadili changamoto mbalimbali zinazoweza kuchelewesha utekelezaji wa Mradi. Pia Menejimenti ya REA ilishiriki mkutano huo. Mradi wa REA Awamu ya III Mzunguko wa I unagharimu Shilingi Trilioni 1.2, ukiwa ni mradi mkubwa kusini mwa jangwa la Sahara ambapo vijiji 3,559 vitaunganishwa na huduma ya nishati ya umeme nchi nzima.

2. Bodi ya Wakurugenzi ilitaka kujua mahusiano mazuri kati ya Wakandarasi wa Mradi huo pamoja na watengenezaji wa vifaa vya mradi kama vile nguzo, nyaya, transfoma, mita na vifaa vingine. Mahusiano mazuri kati ya Wakandarasi wa watengenezaji vifaa hivyo yanaleta tija katika kuharakisha utekelezaji wa mradi.

3. Wakandarasi walieleza baadhi ya changamoto kuhusu kuchelewa kupata vifaa wanavyoagiza kutoka kwa watengenezaji. Bodi ilielezwa na watengenezaji wa vifaa hivyo kuwa wanavyo vya kutosha na watarekebisha kasoro zozote zilizojitokeza ili kuwawezesha Wakandarasi kukamilisha utekelezaji wa Mradi kwa wakati.

4. Bodi, baada ya kuwasikiliza Wakandarasi pamoja na watengenezaji wa vifaa vya mradi, ilieleza kuwa changamoto zilizoelezwa ziko ndani ya uwezo wa kutatuliwa. Changamoto kubwa iliyoonekana ilikuwa ni uelewa wa baadhi ya taratibu ikiwemo bondi inayowekwa na Benki.

5. Mkutano ulisisitiza kuwa Mradi wa REA Awamu ya III Mzunguko wa I utakamilika ifikapo Desemba, 2019 na Wakandarasi atakayechelewesha Mradi kwa mujibu wa Mkataba hawatavumiliwa.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la LAPF, Ghorofa ya 7
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

E-Mail: info@rea.go.tz
Tel: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«April 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
311234
CALL FOR PROPOSAL - Supply and Installation of Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions

CALL FOR PROPOSAL - Supply and Installation of Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions

The Rural Energy Agency issue the Second Call for applications from qualified suppliers to Supply and install Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions through on-call basis.

Read more
56
789
Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24

Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24

Please find the attached Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24:

Read more
10111213
14
Wabia wa Maendeleo Waahidi Kuendelea Kushirikiana na Serikali ya Tanzania Kuboresha Maisha ya Wananchi

Wabia wa Maendeleo Waahidi Kuendelea Kushirikiana na Serikali ya Tanzania Kuboresha Maisha ya Wananchi

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego amuopengeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kazi kubwa ya kufikisha umeme vijijini hali iliyobadili maisha ya wananchi vijijini.

Read more
151617181920
21222324252627
REA Yaendelea Kuhamasisha Matumizi ya Nishati Safi Mbeya Vijijini

REA Yaendelea Kuhamasisha Matumizi ya Nishati Safi Mbeya Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unaendelea zoezi la kuhamasisha na kutoa elimu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ambapo Wananchi wa kijiji cha jojo, kata ya Santilya, tarafa ya Isangati, Halmashauri ya Mbeya vijijini, wamefikiwa na huduma hiyo kupitia maonesho maalum yaliyopewa jina la Wakulima Festival.

Read more
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top