Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
BODI YA WAKURUGENZI YA REA WAKUTANA NA WAKANDARASI, PAMOJA NA WATENGENEZAJI WA VIFAA VYA MRADI WA UMEME VIJIJINI
Admin.Frank Mugogo 9660

BODI YA WAKURUGENZI YA REA WAKUTANA NA WAKANDARASI, PAMOJA NA WATENGENEZAJI WA VIFAA VYA MRADI WA UMEME VIJIJINI

1. Bodi ya Wakala wa Nishati Vijijini leo tarehe 08 Juni 2019 imekutana wa Wakandarasi wa Mradi wa REA Awamu ya III Mzunguko wa I katika Ukumbi wa Hazina, Dodoma kujadili changamoto mbalimbali zinazoweza kuchelewesha utekelezaji wa Mradi. Pia Menejimenti ya REA ilishiriki mkutano huo. Mradi wa REA Awamu ya III Mzunguko wa I unagharimu Shilingi Trilioni 1.2, ukiwa ni mradi mkubwa kusini mwa jangwa la Sahara ambapo vijiji 3,559 vitaunganishwa na huduma ya nishati ya umeme nchi nzima.

2. Bodi ya Wakurugenzi ilitaka kujua mahusiano mazuri kati ya Wakandarasi wa Mradi huo pamoja na watengenezaji wa vifaa vya mradi kama vile nguzo, nyaya, transfoma, mita na vifaa vingine. Mahusiano mazuri kati ya Wakandarasi wa watengenezaji vifaa hivyo yanaleta tija katika kuharakisha utekelezaji wa mradi.

3. Wakandarasi walieleza baadhi ya changamoto kuhusu kuchelewa kupata vifaa wanavyoagiza kutoka kwa watengenezaji. Bodi ilielezwa na watengenezaji wa vifaa hivyo kuwa wanavyo vya kutosha na watarekebisha kasoro zozote zilizojitokeza ili kuwawezesha Wakandarasi kukamilisha utekelezaji wa Mradi kwa wakati.

4. Bodi, baada ya kuwasikiliza Wakandarasi pamoja na watengenezaji wa vifaa vya mradi, ilieleza kuwa changamoto zilizoelezwa ziko ndani ya uwezo wa kutatuliwa. Changamoto kubwa iliyoonekana ilikuwa ni uelewa wa baadhi ya taratibu ikiwemo bondi inayowekwa na Benki.

5. Mkutano ulisisitiza kuwa Mradi wa REA Awamu ya III Mzunguko wa I utakamilika ifikapo Desemba, 2019 na Wakandarasi atakayechelewesha Mradi kwa mujibu wa Mkataba hawatavumiliwa.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la LAPF, Ghorofa ya 7
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

E-Mail: info@rea.go.tz
Tel: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Rate article

No rating
Rate this article:
No rating

Share

Print
«April 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
25
Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa  Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za  Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini unakaribisha maombi ya mkopo nafuu kuwezesha ujenzi wa vituo vidogo vya kuuzia bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) vijijini. Mkopo huu utasaidia uwezeshaji wa ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini ili kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya mafuta kwa gharama nafuu, kwa njia salama, na isiyo na madhara kwa mazingira.

Wakala unawasisitiza waombaji walioomba katika awamu ya kwanza na kutokidhi vigezo kuomba tena baada ya kufanya marekebisho  ya  mapungufu yaliyobainishwa katika maombi yao. Aidha maombi mapya ya mkopo yanakaribishwa.

Read more
262728293031
12345
Call for Proposals for Results Based Financing (RBF) Application for Stand Alone Solar Home System (SA-SHS)

Call for Proposals for Results Based Financing (RBF) Application for Stand Alone Solar Home System (SA-SHS)

The Rural Energy Agency (REA) invites eligible firms to apply for grant per new SA-SHS installation in targeted rural communities. The grant includes end-user buying price system subsidization and firm’s performance incentive. The SA-SHS grant application is implemented through the program for Tanzania Rural Electrification Expansion Program Additional Financing (TREEP AF) which is supported by the World Bank.

Read more
67
891011121314
15
Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA

Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA


Wabia wa Maendeleo ambao wanafadhili miradi ya kusambaza nishati vijijini wamepongeza Wakala wa Nishati Vijijini kwa utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini ambayo inaleta tija kwa ustawi wa wananchi.

Read more
161718192021
222324
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25

Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25

Hotuba ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mheshimiwa Dkt. Doto Mashaka Biteko (Mb), Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25.

Read more
25262728
293012345

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top