Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA: Usambazaji Wa Umeme Waendelea Kufungua Fursa Za Uzalishaji, Ajira Na Maendeleo Vijijini
Mohamed Saif 145

REA: Usambazaji Wa Umeme Waendelea Kufungua Fursa Za Uzalishaji, Ajira Na Maendeleo Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA), umesema usambazaji wa umeme vijijini unaendelea kuwa kichocheo kikubwa cha ukuaji wa uchumi kwa kufungua fursa za uzalishaji, ajira na uwekezaji, huku ukiboresha maisha ya wananchi kupitia maendeleo ya sekta mbalimbali za kiuchumi.

Akizungumza katika Maonesho ya Nane Nane katika Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma, Mkurugenzi wa Umeme Vijijini kutoka REA, Mha. Jones Olotu, amesema uwekezaji wa Serikali kupitia REA katika miradi ya kusambaza umeme; umewezesha sekta mbalimbali za uzalishaji kukua kwa kasi na kuongeza mchango wake katika maendeleo ya uchumi wa vijijini.

“Lengo la REA si kusambaza umeme pekee yake bali kuhakikisha umeme unakuwa chachu ya kuleta maendeleo kwa kuwezesha viwanda vidogo na vya kati, biashara, huduma za kijamii pamoja na shughuli nyingine za uzalishaji vijijini,” amesema Mha. Olotu.

Ameeleza kuwa upatikanaji wa umeme wa uhakika umeongeza tija katika shughuli za uzalishaji, umeimarisha mnyororo wa thamani wa mazao ya kilimo kupitia uchakataji, uhifadhi na uongezaji thamani, hatua inayowawezesha wakulima na wajasiriamali kuongeza kipato na ushindani wa bidhaa zao sokoni.

Aidha, amesema maendeleo hayo yameongeza fursa za ajira, kuchochea uwekezaji katika viwanda vidogo na vya kati, kukuza biashara na kuboresha utoaji wa huduma muhimu za kijamii, ili kuimarisha ustawi wa wananchi na uchumi wa vijijini kwa ujumla.

Amesisitiza kuwa REA itaendelea kutekeleza miradi ya kusambaza umeme na kuwaunganisha wananchi na huduma hiyo ili kuhakikisha nishati ya umeme inaendelea kuwa nguzo muhimu ya maendeleo endelevu na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Aidha, wananchi wanaotembelea banda la REA katika Maonesho ya Nanenane wanaendelea kujifunza kuhusu mafanikio ya utekelezaji wa miradi ya umeme vijijini na namna huduma hiyo inavyoendelea kufungua fursa za kiuchumi, kuongeza tija katika uzalishaji na kubadilisha maisha ya Watanzania.

Share

Print
«September 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
31123456
789
Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

IRINGA, Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini kwa kuendesha mafunzo maalum ya wiki moja yaliyolenga kujenga uwezo wa waendelezaji wa miradi midogo ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower).

Mafunzo hayo yaliyoanza tarehe 7 Septemba, 2026 katika Hoteli ya Sunset mkoani Iringa, yamewakutanisha waendelezaji wa miradi (Developers) zaidi ya 15, hususan kutoka maeneo ya Nyanda za Juu Kusini. Lengo kuu ni kuwajengea uwezo wa kiufundi ili kuongeza ubora wa miradi yao ili iweze kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, tarehe 9 Septemba, 2026, Kaimu Meneja wa Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi kutoka REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya, alisema kuwa REA haishii tu kutoa msaada wa upatikanaji wa nishati vijijini, bali inajikita pia katika kuongeza ujuzi wa wataalamu wa ndani.

"Kuongeza ujuzi kwa waendelezaji hawa kutasaidia kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu na ubora unaohitajika. Hatua hii itaongeza idadi ya miradi inayofikia vigezo vya kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa, kuongeza uzalishaji wa umeme, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii vijijini," alisema Mhandisi Yesaya.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ushirikiano kati ya REA na Wataalamu kutoka Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia (CoET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Maeneo yaliyofundishwa ni pamoja na usanifu wa miradi, upembuzi yakinifu, sayansi ya maji (hydrology), uhandisi wa umeme na elektroniki, pamoja na uendeshaji na matengenezo ya mitambo.

Mbali na mafunzo, REA imebainisha kuwa imekuwa ikisaidia waendelezaji hao kupitia ruzuku za ujenzi, maandalizi ya maandiko ya miradi na usanifu.

Aidha, Wakala huo upo katika mchakato wa kuandaa mfumo wa mikataba ya muda mrefu (Framework Contract) na taasisi za elimu ili kutoa mafunzo endelevu kwenye nishati jadidifu ikiwemo nishati ya jua na mifumo ya gesi vunde.

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wamepongeza mafunzo hayo; akizungumza na Wanahabari, Mhandisi Denis Makoyi kutoka kampuni ya Africa Power Investment, alisema mafunzo hayo yameongeza uelewa mkubwa wa kiufundi katika hatua za utekelezaji wa miradi. Naye Lutengano Kigola kutoka mradi wa Nyalawa Hydropower, aliongeza kuwa mafunzo hayo yanathibitisha kuwa Tanzania ina wataalamu wa ndani wenye uwezo mkubwa wa kuendeleza miradi ya umeme wa maji.

  • MWISHO –

 

Read more
10111213
14
REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuwezesha waendelezaji wadogo wa miradi ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kwa kutoa fedha, msaada wa kitaalamu na mafunzo, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa nishati nchini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top