Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
KONGAMANO LA “BIG RESULTS NOW” MIRADI MIKUBWA YA NISHATI YATAJWA
Host 19014

KONGAMANO LA “BIG RESULTS NOW” MIRADI MIKUBWA YA NISHATI YATAJWA

Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Prof. Sospeter Muhongo, ametaja miradi ya kipaumbele itakayotoa matokeo ya haraka ifikapo 2015/2016, na kunufaisha wananchi katika mikoa mbalimbali nchini. Prof. Muhomgoaliitaja miradi hiyo mikubwa jijini Dar es Salaam mbele ya wadau waliokusanyika katika kongamano la wazi la siku moja kwa lengo la kukusanya maoni kuhusu utekelezaji wa miradi hiyo.

Prof. Muhongo alitoa changamoto kwa wananchi la kumchukulia hatua yeye na watendaji walio chini ya wizara yake, endapo watashindwa kulifikia lengo hilo. Alisema Wizara imedhamiria kuhakikisha miradi hiyo kwa kipindi hicho, inaleta matokeo muafaka ‘big result now’ yatakayoonekana wazi kwa Watanzania wote.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Bw. Eliakim Maswi alisema Watanzania watarajie mambo makubwa kutokana na miradi hiyo ambayo itapelekea kumaliza tatizo la umeme nchini.

Kiambatanisho: Taarifa ya Uchambuzi na Mapendekezo ya Utekelezaji wa Miradi Yenye Lengo la Kuleta Matokeo Makubwa Sasa Kwa Wizara ya Nishati na Madini.

Taarifa ya kimaabara inayoelezea kwa kina uchambuzi wa miradi ya kipaumbele ya nishati iliyotokana na upembuzi wa kimaabara uliofanyika kwa kipindi cha wiki sita (6), kuanzia tarehe 22 Februari hadi tarehe 5 Aprili 2013. Utekelezaji wa miradi hii unaanza rasmi tarehe 1 Julai 2013 na wizara ina jukumu la kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa miradi hii kama ilivyopangwa pamoja na kutatua matatizo yote yanayoweza kukwamisha utekelezaji wa miradi hiyo kukamilika mapema zaidi. Miradi hiyo yote inapaswa kukamilika utekelezwaji wake ifikapo mwezi Juni, 2016.


Imeandaliwa na:

Mohamed M. Saif
Afisa Habari
Wizara ya Nishati na Madini
754/33, Samora Avenue
S. L. P. 2000
Dar es Salaam, Tanzania
info@mem.go.tz
www.mem.go.tz

Share

Print

Documents to download

«September 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
25262728293031
1234
Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

Deadline for submission of Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts has been extended up to 15th September 2025.

The Rural Energy Agency (REA) is seeking proposals from qualified service providers for the supply, installation, and testing of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in eight remote villages across Geita, Ludewa and Mbulu districts. Those villages are located in remote areas with challenging geographical conditions, hence, impractical for grid extension.

Please find the attached documents:

•    Application Form for Supply and Installation of SA-SHS; and
•    Call for Proposals for Result Based Financing Installation of Stand Alone Solar Home Systems.

Read more
567
Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Ahamasisha Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Ahamasisha Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru wa Kitaifa, Ismail Ali Ussi amewahamasisha wananchi kuunga mkono kampeni ya nishati safi ya kupikia ili kulinda afya pamoja kuokoa mazingira.

Read more
8910
Dkt. Biteko Aimwagia Sifa REA, Ataka Taasisi Zingine Ziige

Dkt. Biteko Aimwagia Sifa REA, Ataka Taasisi Zingine Ziige

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko ameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kukamilisha lengo la usambazaji Umeme katika Vijiji 12,318 Nchini na kwa umahiri wake katika kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
11121314
15161718192021
22232425262728
293012345

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top