Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
KONGAMANO LA “BIG RESULTS NOW” MIRADI MIKUBWA YA NISHATI YATAJWA
Host 18888

KONGAMANO LA “BIG RESULTS NOW” MIRADI MIKUBWA YA NISHATI YATAJWA

Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Prof. Sospeter Muhongo, ametaja miradi ya kipaumbele itakayotoa matokeo ya haraka ifikapo 2015/2016, na kunufaisha wananchi katika mikoa mbalimbali nchini. Prof. Muhomgoaliitaja miradi hiyo mikubwa jijini Dar es Salaam mbele ya wadau waliokusanyika katika kongamano la wazi la siku moja kwa lengo la kukusanya maoni kuhusu utekelezaji wa miradi hiyo.

Prof. Muhongo alitoa changamoto kwa wananchi la kumchukulia hatua yeye na watendaji walio chini ya wizara yake, endapo watashindwa kulifikia lengo hilo. Alisema Wizara imedhamiria kuhakikisha miradi hiyo kwa kipindi hicho, inaleta matokeo muafaka ‘big result now’ yatakayoonekana wazi kwa Watanzania wote.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Bw. Eliakim Maswi alisema Watanzania watarajie mambo makubwa kutokana na miradi hiyo ambayo itapelekea kumaliza tatizo la umeme nchini.

Kiambatanisho: Taarifa ya Uchambuzi na Mapendekezo ya Utekelezaji wa Miradi Yenye Lengo la Kuleta Matokeo Makubwa Sasa Kwa Wizara ya Nishati na Madini.

Taarifa ya kimaabara inayoelezea kwa kina uchambuzi wa miradi ya kipaumbele ya nishati iliyotokana na upembuzi wa kimaabara uliofanyika kwa kipindi cha wiki sita (6), kuanzia tarehe 22 Februari hadi tarehe 5 Aprili 2013. Utekelezaji wa miradi hii unaanza rasmi tarehe 1 Julai 2013 na wizara ina jukumu la kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa miradi hii kama ilivyopangwa pamoja na kutatua matatizo yote yanayoweza kukwamisha utekelezaji wa miradi hiyo kukamilika mapema zaidi. Miradi hiyo yote inapaswa kukamilika utekelezwaji wake ifikapo mwezi Juni, 2016.


Imeandaliwa na:

Mohamed M. Saif
Afisa Habari
Wizara ya Nishati na Madini
754/33, Samora Avenue
S. L. P. 2000
Dar es Salaam, Tanzania
info@mem.go.tz
www.mem.go.tz

Share

Print

Documents to download

«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top