Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
KONGAMANO LA “BIG RESULTS NOW” MIRADI MIKUBWA YA NISHATI YATAJWA
Host 19188

KONGAMANO LA “BIG RESULTS NOW” MIRADI MIKUBWA YA NISHATI YATAJWA

Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Prof. Sospeter Muhongo, ametaja miradi ya kipaumbele itakayotoa matokeo ya haraka ifikapo 2015/2016, na kunufaisha wananchi katika mikoa mbalimbali nchini. Prof. Muhomgoaliitaja miradi hiyo mikubwa jijini Dar es Salaam mbele ya wadau waliokusanyika katika kongamano la wazi la siku moja kwa lengo la kukusanya maoni kuhusu utekelezaji wa miradi hiyo.

Prof. Muhongo alitoa changamoto kwa wananchi la kumchukulia hatua yeye na watendaji walio chini ya wizara yake, endapo watashindwa kulifikia lengo hilo. Alisema Wizara imedhamiria kuhakikisha miradi hiyo kwa kipindi hicho, inaleta matokeo muafaka ‘big result now’ yatakayoonekana wazi kwa Watanzania wote.

Naye Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Bw. Eliakim Maswi alisema Watanzania watarajie mambo makubwa kutokana na miradi hiyo ambayo itapelekea kumaliza tatizo la umeme nchini.

Kiambatanisho: Taarifa ya Uchambuzi na Mapendekezo ya Utekelezaji wa Miradi Yenye Lengo la Kuleta Matokeo Makubwa Sasa Kwa Wizara ya Nishati na Madini.

Taarifa ya kimaabara inayoelezea kwa kina uchambuzi wa miradi ya kipaumbele ya nishati iliyotokana na upembuzi wa kimaabara uliofanyika kwa kipindi cha wiki sita (6), kuanzia tarehe 22 Februari hadi tarehe 5 Aprili 2013. Utekelezaji wa miradi hii unaanza rasmi tarehe 1 Julai 2013 na wizara ina jukumu la kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa miradi hii kama ilivyopangwa pamoja na kutatua matatizo yote yanayoweza kukwamisha utekelezaji wa miradi hiyo kukamilika mapema zaidi. Miradi hiyo yote inapaswa kukamilika utekelezwaji wake ifikapo mwezi Juni, 2016.


Imeandaliwa na:

Mohamed M. Saif
Afisa Habari
Wizara ya Nishati na Madini
754/33, Samora Avenue
S. L. P. 2000
Dar es Salaam, Tanzania
info@mem.go.tz
www.mem.go.tz

Share

Print

Documents to download

«February 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
2627
Rais Samia Apeleka Neema ya Umeme Katika Vitongoji Lindi

Rais Samia Apeleka Neema ya Umeme Katika Vitongoji Lindi

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa shilingi bilioni 25.8 wa kusambaza umeme katika vitongoji 159 utakaonufaisha kaya 5,116 Mkoani Lindi.

Read more
2829
Shangwe Mtwara - Bilioni 15.3 Kusambaza Umeme Vitongoji 175

Shangwe Mtwara - Bilioni 15.3 Kusambaza Umeme Vitongoji 175

Wananchi wa vitongoji vya Msokole na Funguni Kijiji cha Mnazi Kata ya Nalingu Mkoani Mtwara wameishukuru Serikali kwa kuwapelekea mradi wa Umeme unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ambao wamesema unakwenda kubadili maisha yao.

Read more
3031
Mkandarasi Northern Engineering Atakiwa Kuongeza Kasi Ya Ujenzi Wa Mradi Mtwara

Mkandarasi Northern Engineering Atakiwa Kuongeza Kasi Ya Ujenzi Wa Mradi Mtwara

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemtaka Mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Kusambaza umeme katika Vitongoji 150 vya Majimbo 10 Mkoani Mtwara kuongeza kasi ya ujenzi ili kukamilisha Mradi kwa wakati.

Read more
1
2345678
9101112131415
16171819202122
2324252627281
2345678

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top