Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mkurugenzi Mkuu wa REA Akagua Utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Kupozea Umeme Ifakara
Aodax K. Nshala 742

Mkurugenzi Mkuu wa REA Akagua Utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Kupozea Umeme Ifakara

Kitakuwa na uwezo wa MVA 20 na kitasaidia wananchi Kilombero, Ulanga na Malinyi

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema ujenzi wa mradi wa kituo cha kupooza na kusambaza umeme Ifakara kitakachokuwa na uwezo wa kuzalisha MVA 20 kitasaidia wananchi wa wilaya za Kilombero, Ulanga na Malinyi kupata huduma bora ya umeme na ya uhakika.

Kituo cha kupoza umeme cha Ifakara kilichoanza kujengwa Machi 2020, kinatarajiwa kuhudumia Wananchi wa wilaya za Kilombero na Ulanga kwa ufanisi mkubwa na kupunguza kwa sehemu kubwa changamoto ya kukatika kwa umeme mara kwa mara.

Hayo yamesemwa tarehe 8 Disemba, 2022 katika mji wa Ifakara, wilayani Kilombero mkoani Morogoro wakati Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Saidy alipozungumza na Wanahabari kuhusu utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Kituo hicho ambao aliuelezea kuwa umeongeza kilomita 82 za miundombinu ya usambazaji wa umeme katika Wilaya ya Kilombero na Ulanga.

Mhandisi Saidy amesema kuwa, ujenzi wa kituo hicho umefikia asilimia 80.1 na unatarajiwa kukamilika mwezi Machi, 2023 ambapo mpaka sasa tayari transfoma ya kisasa imeshawekwa na kituo kitatoa njia nne za umeme ambazo zitapeleka nishati hiyo kwenye maeneo mbalimbali ya wilaya hizo.

Akizungumza kuhusu kurefusha njia za kusambaza umeme, Mhandisi Saidy amesema, mradi huo umeshakamilika na njia hizo zenye jumla ya kilomita 82 zitaweza kufikia vijiji na vitongoji takribani 15 katika wilaya ya Kilombero.

"Kwa muda mrefu wananchi wa maeneo haya walikuwa wanapata changamoto ya kukatika kwa umeme na kupungua kwa nguvu ya umeme ambayo imesababisha kuunguza vifaa vya umeme na hata mitambo, hivyo Mradi huu utaondoa adha ya umeme kukatika na utaboresha ubora wa huduma," alisema.

Mradi huo wa kituo cha kupoza umeme na kilomita 82 za miundombinu ya usambazaji wa umeme vinagharamiwa na Serikali ya Tanzania kwa

kushirikiana na Jumuiya ya Ulaya kwa gharama ya EURO milioni 8.75 ambapo Kituo cha kupoza umeme pekee kimegharimu EURO milioni 5.4.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Idara ya Habari - MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Bwana Gerson Msigwa, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara hiyo, Bwana Rodney Thadeus amesema kuwa nishati inafungamanisha na maendeleo mengine ya kiuchumi ambapo Serikali imeendelea kujenga miundombinu mbalimbali ikiwemo hospitali na shule pamoja na kuwawezesha wakulima, hivyo ukosefu wa nishati utafanya shughuli hizo kutokwenda vizuri.

"Natoa rai kwa Wananchi kushirikiana na Serikali katika kuibadilisha Tanzania kupitia REA ambayo inaendelea kubadilisha maisha ya Watanzania kwa kuhakikisha wanapata nishati," alikaririwa Bwana Thadeus.

Rate article

No rating
Rate this article:
No rating

Share

Print
«April 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
25
Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa  Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za  Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini unakaribisha maombi ya mkopo nafuu kuwezesha ujenzi wa vituo vidogo vya kuuzia bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) vijijini. Mkopo huu utasaidia uwezeshaji wa ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini ili kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya mafuta kwa gharama nafuu, kwa njia salama, na isiyo na madhara kwa mazingira.

Wakala unawasisitiza waombaji walioomba katika awamu ya kwanza na kutokidhi vigezo kuomba tena baada ya kufanya marekebisho  ya  mapungufu yaliyobainishwa katika maombi yao. Aidha maombi mapya ya mkopo yanakaribishwa.

Read more
262728293031
12345
Call for Proposals for Results Based Financing (RBF) Application for Stand Alone Solar Home System (SA-SHS)

Call for Proposals for Results Based Financing (RBF) Application for Stand Alone Solar Home System (SA-SHS)

The Rural Energy Agency (REA) invites eligible firms to apply for grant per new SA-SHS installation in targeted rural communities. The grant includes end-user buying price system subsidization and firm’s performance incentive. The SA-SHS grant application is implemented through the program for Tanzania Rural Electrification Expansion Program Additional Financing (TREEP AF) which is supported by the World Bank.

Read more
67
891011121314
15
Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA

Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA


Wabia wa Maendeleo ambao wanafadhili miradi ya kusambaza nishati vijijini wamepongeza Wakala wa Nishati Vijijini kwa utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini ambayo inaleta tija kwa ustawi wa wananchi.

Read more
161718192021
22232425262728
293012345

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top