Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mkurugenzi Mkuu wa REA Akagua Utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Kupozea Umeme Ifakara
Aodax K. Nshala 1148

Mkurugenzi Mkuu wa REA Akagua Utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Kupozea Umeme Ifakara

Kitakuwa na uwezo wa MVA 20 na kitasaidia wananchi Kilombero, Ulanga na Malinyi

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema ujenzi wa mradi wa kituo cha kupooza na kusambaza umeme Ifakara kitakachokuwa na uwezo wa kuzalisha MVA 20 kitasaidia wananchi wa wilaya za Kilombero, Ulanga na Malinyi kupata huduma bora ya umeme na ya uhakika.

Kituo cha kupoza umeme cha Ifakara kilichoanza kujengwa Machi 2020, kinatarajiwa kuhudumia Wananchi wa wilaya za Kilombero na Ulanga kwa ufanisi mkubwa na kupunguza kwa sehemu kubwa changamoto ya kukatika kwa umeme mara kwa mara.

Hayo yamesemwa tarehe 8 Disemba, 2022 katika mji wa Ifakara, wilayani Kilombero mkoani Morogoro wakati Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Saidy alipozungumza na Wanahabari kuhusu utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Kituo hicho ambao aliuelezea kuwa umeongeza kilomita 82 za miundombinu ya usambazaji wa umeme katika Wilaya ya Kilombero na Ulanga.

Mhandisi Saidy amesema kuwa, ujenzi wa kituo hicho umefikia asilimia 80.1 na unatarajiwa kukamilika mwezi Machi, 2023 ambapo mpaka sasa tayari transfoma ya kisasa imeshawekwa na kituo kitatoa njia nne za umeme ambazo zitapeleka nishati hiyo kwenye maeneo mbalimbali ya wilaya hizo.

Akizungumza kuhusu kurefusha njia za kusambaza umeme, Mhandisi Saidy amesema, mradi huo umeshakamilika na njia hizo zenye jumla ya kilomita 82 zitaweza kufikia vijiji na vitongoji takribani 15 katika wilaya ya Kilombero.

"Kwa muda mrefu wananchi wa maeneo haya walikuwa wanapata changamoto ya kukatika kwa umeme na kupungua kwa nguvu ya umeme ambayo imesababisha kuunguza vifaa vya umeme na hata mitambo, hivyo Mradi huu utaondoa adha ya umeme kukatika na utaboresha ubora wa huduma," alisema.

Mradi huo wa kituo cha kupoza umeme na kilomita 82 za miundombinu ya usambazaji wa umeme vinagharamiwa na Serikali ya Tanzania kwa

kushirikiana na Jumuiya ya Ulaya kwa gharama ya EURO milioni 8.75 ambapo Kituo cha kupoza umeme pekee kimegharimu EURO milioni 5.4.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Idara ya Habari - MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Bwana Gerson Msigwa, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara hiyo, Bwana Rodney Thadeus amesema kuwa nishati inafungamanisha na maendeleo mengine ya kiuchumi ambapo Serikali imeendelea kujenga miundombinu mbalimbali ikiwemo hospitali na shule pamoja na kuwawezesha wakulima, hivyo ukosefu wa nishati utafanya shughuli hizo kutokwenda vizuri.

"Natoa rai kwa Wananchi kushirikiana na Serikali katika kuibadilisha Tanzania kupitia REA ambayo inaendelea kubadilisha maisha ya Watanzania kwa kuhakikisha wanapata nishati," alikaririwa Bwana Thadeus.

Share

Print
«December 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526
Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya  Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaanza kutekeleza mradi wa kutandaza nyaya za umeme (wiring) kwa wananchi kupitia miradi ya kusambaza umeme inayotekelezwa na wakala kote nchini.

Read more
27282930
123
Hafla ya Utiaji Saini Mikataba ya Nishati Safi

Hafla ya Utiaji Saini Mikataba ya Nishati Safi

Karibu katika Hafla ya Kusaini Mikataba ya Kufunga Miundombinu ya Nishati Safi katika Shule za Sekondari 52 pamoja na Chuo cha VETA.

Read more
45
Shule za Sekondari 52; Chuo cha VETA Kufungiwa Miundombinu ya Nishati Safi

Shule za Sekondari 52; Chuo cha VETA Kufungiwa Miundombinu ya Nishati Safi

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imesaini mikataba ya kufunga miundombinu ya nishati safi ya kupikia kwa shule za Sekondari 52 na Chuo cha VETA kimoja hapa nchini.

Read more
67
891011121314
1516
Mkurugenzi Mkuu REA Awafunda Watumishi

Mkurugenzi Mkuu REA Awafunda Watumishi

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amewataka watumishi kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na maarifa ili kuleta tija katika kuwatumikia wananchi.

Read more
17
REA Yashinda Tuzo ya Utoaji Huduma kwenye Utumishi wa Umma

REA Yashinda Tuzo ya Utoaji Huduma kwenye Utumishi wa Umma

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeshinda tuzo ya Taasisi Bora inayoshughulikia malalamiko ya Wateja pamoja na kutoa mrejesho kwa wakati katika utoaji wa huduma kwa umma (Watanzania) kwa mwaka 2025.

Read more
1819
Majiko Banifu ya Ruzuku yapiga hodi Katavi

Majiko Banifu ya Ruzuku yapiga hodi Katavi

Mkuu wa Mkoa wa Katavi, Mhe. Mwanamvua Mrindoko ametoa wito kwa wananchi wa Katavi kuchangamkia fursa ya kununua majiko banifu kwa bei ruzuku ya shilingi 7,500 yanayosambazwa kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ili kulinda afya, kuokoa misitu na kuhifadhi mazingira.

Read more
2021
REA yapeleka Tabasamu Nsimbo

REA yapeleka Tabasamu Nsimbo

Wananchi wa Kijiji cha Mtakuja Kata ya Kapalala katika Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo Mkoani Katavi wameipongeza Serikali kwa kuweka ruzuku kwenye majiko banifu hatua ambayo wamesema inawezesha mwananchi wa kipato chochote kutumia Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
22232425262728
2930311234

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top