Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mkurugenzi Mkuu wa REA Akagua Utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Kupozea Umeme Ifakara
Aodax K. Nshala 864

Mkurugenzi Mkuu wa REA Akagua Utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Kupozea Umeme Ifakara

Kitakuwa na uwezo wa MVA 20 na kitasaidia wananchi Kilombero, Ulanga na Malinyi

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema ujenzi wa mradi wa kituo cha kupooza na kusambaza umeme Ifakara kitakachokuwa na uwezo wa kuzalisha MVA 20 kitasaidia wananchi wa wilaya za Kilombero, Ulanga na Malinyi kupata huduma bora ya umeme na ya uhakika.

Kituo cha kupoza umeme cha Ifakara kilichoanza kujengwa Machi 2020, kinatarajiwa kuhudumia Wananchi wa wilaya za Kilombero na Ulanga kwa ufanisi mkubwa na kupunguza kwa sehemu kubwa changamoto ya kukatika kwa umeme mara kwa mara.

Hayo yamesemwa tarehe 8 Disemba, 2022 katika mji wa Ifakara, wilayani Kilombero mkoani Morogoro wakati Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Saidy alipozungumza na Wanahabari kuhusu utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Kituo hicho ambao aliuelezea kuwa umeongeza kilomita 82 za miundombinu ya usambazaji wa umeme katika Wilaya ya Kilombero na Ulanga.

Mhandisi Saidy amesema kuwa, ujenzi wa kituo hicho umefikia asilimia 80.1 na unatarajiwa kukamilika mwezi Machi, 2023 ambapo mpaka sasa tayari transfoma ya kisasa imeshawekwa na kituo kitatoa njia nne za umeme ambazo zitapeleka nishati hiyo kwenye maeneo mbalimbali ya wilaya hizo.

Akizungumza kuhusu kurefusha njia za kusambaza umeme, Mhandisi Saidy amesema, mradi huo umeshakamilika na njia hizo zenye jumla ya kilomita 82 zitaweza kufikia vijiji na vitongoji takribani 15 katika wilaya ya Kilombero.

"Kwa muda mrefu wananchi wa maeneo haya walikuwa wanapata changamoto ya kukatika kwa umeme na kupungua kwa nguvu ya umeme ambayo imesababisha kuunguza vifaa vya umeme na hata mitambo, hivyo Mradi huu utaondoa adha ya umeme kukatika na utaboresha ubora wa huduma," alisema.

Mradi huo wa kituo cha kupoza umeme na kilomita 82 za miundombinu ya usambazaji wa umeme vinagharamiwa na Serikali ya Tanzania kwa

kushirikiana na Jumuiya ya Ulaya kwa gharama ya EURO milioni 8.75 ambapo Kituo cha kupoza umeme pekee kimegharimu EURO milioni 5.4.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Idara ya Habari - MAELEZO na Msemaji Mkuu wa Serikali, Bwana Gerson Msigwa, Mkurugenzi Msaidizi wa Idara hiyo, Bwana Rodney Thadeus amesema kuwa nishati inafungamanisha na maendeleo mengine ya kiuchumi ambapo Serikali imeendelea kujenga miundombinu mbalimbali ikiwemo hospitali na shule pamoja na kuwawezesha wakulima, hivyo ukosefu wa nishati utafanya shughuli hizo kutokwenda vizuri.

"Natoa rai kwa Wananchi kushirikiana na Serikali katika kuibadilisha Tanzania kupitia REA ambayo inaendelea kubadilisha maisha ya Watanzania kwa kuhakikisha wanapata nishati," alikaririwa Bwana Thadeus.

Share

Print
«April 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
311234
CALL FOR PROPOSAL - Supply and Installation of Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions

CALL FOR PROPOSAL - Supply and Installation of Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions

The Rural Energy Agency issue the Second Call for applications from qualified suppliers to Supply and install Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions through on-call basis.

Read more
56
789
Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24

Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24

Please find the attached Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24:

Read more
10111213
14
Wabia wa Maendeleo Waahidi Kuendelea Kushirikiana na Serikali ya Tanzania Kuboresha Maisha ya Wananchi

Wabia wa Maendeleo Waahidi Kuendelea Kushirikiana na Serikali ya Tanzania Kuboresha Maisha ya Wananchi

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego amuopengeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kazi kubwa ya kufikisha umeme vijijini hali iliyobadili maisha ya wananchi vijijini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top