Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya REA Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Gideon Kingu Akutana na Menejimenti
Aodax K. Nshala 1018

Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya REA Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Gideon Kingu Akutana na Menejimenti

Aipongeza kwa Kutekeleza Majukumu Yake Kwa Weledi

Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya Nishati Vijijini, Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Gideon Kingu amefanya mkutano wa kwanza na Menejimenti ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) leo tarehe 06 Oktoba 2023. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassam alimteua Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakala wa Nishati Vijijini tarehe 25 Septemba 2023.

Katika mkutano huo, Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan S. Saidy alimkaribisha Mwenyekiti na kufafanua Muundo na Majukumu ya Wakala kama yalivyoainishwa katika Sheria ya Nishati Vijijini Na. 5 ya Mwaka 2005. Aidha, Mkurugenzi Mkuu alieleza mipango na miradi iliyotekelezwa na Wakala tangu kuanzishwa kwake Mwaka 2007; mipango na miradi inayoendelea kutekelezwa; pamoja na mikakati itakayowezesha Serikali kufikia malengo ya kuhakikisha vijiji vyote vinafikiwa na huduma bora na za kisasa za nishati vijijini kufikia Mwaka 2025.

Mha. Hassan saidy alimweleza Mhe. Mwenyekiti kuwa, pamoja na miradi ya umeme vijijini inayopanua gridi ya Taifa, pia kuna miradi ya nishati jadidifu ambayo inatekelezwa katika maeneo ambayo ni mbali na gridi ya Taifa pamoja na maeneo ambayo hayafikiki kirahisi na miundombinu ya gridi ya Taifa ikiwa ni pamoja na maeneo ya visiwani. 

Mkurugenzi wa Umeme Vijijini, Mha. Jones Olotu alitoa maelezo kuwa, wakati Wakala unaanza kutekeleza majukumu yake Mwaka 2007, upatikanaji wa umeme vijijini ulikuwa umefikia asilimia 2 tu na jumla ya vijiji 506 kati ya vijiji 12,318 vya Tanzania Bara vilikuwa vimefikiwa na miundombinu  ya umeme. Tathmini iliyofanyika Mwaka 2020 ilionesha kuwa, hadi kufikia mwaka huo hali ya upatikanaji wa umeme vijijini ilifikia asilimia 69.6. Kwa sasa Wakala unaandaa kazi ya kutathmini hali ya upatikanaji umeme nchini kufikia mwaka 2025.

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Nishati Jadidifu na Teknolojia Mbadala, Mha. Emanuel Yesaya alieleza mipango na miradi ya Wakala ya kusambaza nishati safi ya kupikia ukiwemo mradi wa kusambaza mitungi ya gesi ya LPG 70,200 kwa ajili ya kuwapatia wananchi nishati safi na salama  ya kupikia; maendeleo ya mradi wa kujenga na kuendeleza vituo vya mafuta ya petroli na dizeli vijijini; uwezeshaji katika kutengeneza majiko banifu (Improved Cook Stoves); pamoja na kuwawezesha waendelezaji binafsi wanaotengeneza mkaa mbadala (briquettes). Aidha, kusimamia utekelezaji wa miradi ya gridi ndogo za umeme (mini grids) inayotekelezwa na waendelezaji miradi waliopata ruzuku mbalimbali kutoka kwa Wakala.

Mwenyekiti wa Bodi, Mhe. Balozi Meja Jenerali Mtaafu Jacob Gideon Kingu ameipongeza Menejimenti ya Wakala kwa namna ambavyo imekuwa ikitekeleza majukumu yake kwa weledi. Mwenyekiti ametoa rai kwamba, kama wataalamu tuhakikishe tunakamilisha utekelezaji wa majukumu na miradi kwa wakati. Amesisitiza kuwa, Wakala uhakikishe kuwa mikataba isimamiwe vizuri, manunuzi yafanyike kwa kufuata sheria, na malipo ya huduma mbalimbali yafuate tararibu ili kuepukana na hoja za ukaguzi.

Mwenyekiti alieleza kuwa atahakikisha anasaidia juhudi za Wakala katika utekelezaji wa shughuli na kwamba, watakapotangazwa wajumbe wa Bodi, watafanya kazi kwa pamoja na Menejimenti katika kufikia malengo ya Taifa kwamba, kila Kijiji na kila kitongoji kinafikiwa na huduma ya umeme.

Share

Print
«August 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
272829303112
3456789
1011121314
REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefanikiwa kusambaza takribani mitungi laki saba ya gesi ya kupikia (LPG) nchini kote, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa kasi wa Mkakati wa Kitaifa wa Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
1516
1718

Maombi ya Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unakaribisha waombaji wenye vigezo kuomba mkopo wa kuwezesha ujenzi wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) ili kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini.

Pamoja na tangazo hili, tumeweka viambatanisho vifuatavyo:
•    Tangazo la fursa ya mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta ya Petroli na Dizeli vijijini.
•    Mwongozo wa utoaji mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta vijijini.
•    Fomu ya Maombi ya Mkopo.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la REA
Mtaa wa Medeli
P. O. Box 2153,
DODOMA, TANZANIA.

Read more
1920212223
2425262728
Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Yaridhishwa na Usambazaji wa Umeme Kisiwani Jibondo

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Yaridhishwa na Usambazaji wa Umeme Kisiwani Jibondo

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) imeeleza kuridhishwa kwake na kasi ya usambazaji wa nishati ya umeme katika vitongoji vya Kisiwa cha Jibondo, kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mafia, mkoani Pwani.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa REB, Mhe. Balozi na Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu, tarehe 27 Agosti, 2026 alipoambatana na Menejimenti ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kisiwani humo kukagua maendeleo ya mradi huo mkubwa ambao tayari umegharimu kiasi cha shilingi bilioni 8.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Meja Jenerali Kingu amesema kuwa kwa mara ya kwanza katika historia, vitongoji vya Kisiwa cha Jibondo vinatarajia kupata huduma hiyo ya nishati hivi karibuni. Alifafanua kuwa kazi kubwa iliyobaki kwa sasa ni ya usafirishaji wa umeme kwa kutumia waya maalum wa chini ya maji (Submarine cable) kutoka kisiwa kidogo cha Juani kwenda Jibondo, kazi inayotarajiwa kuanza kesho, tarehe 29 Agosti 2026, na kukamilika baada ya siku tano.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy, amesema kuwa maandalizi yote ya miundombinu ikiwemo ujenzi wa njia za kusafirisha umeme ndani ya kisiwa hicho yamekamika kwa asilimia 90 na ameongeza kuwa mara baada ya nyaya hizo za chini ya maji kuunganishwa, wananchi wataanza kuunganishiwa huduma hiyo mara moja.

Mhandisi Saidy amebainisha kuwa mradi huo umefanikiwa kwa ushirikiano wa REA iliyochangia shilingi bilioni 6.8 na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) lililochangia shilingi bilioni 2.

Katika hatua nyingine, Mhandisi Saidy ametoa wito kwa wakazi wa Jibondo kujiandaa kiuchumi ili kuutumia umeme huo katika kuboresha maisha yao na kuendesha shughuli za kimaendeleo, hasa ikizingatiwa kuwa sehemu kubwa ya wakazi wa eneo hilo wamejiajiri kwenye sekta za uvuvi, usindikaji wa mazao ya bahari, na kilimo cha mwani.

Wilaya ya Mafia ina jumla ya vitongoji 136, ambapo vitongoji 111 tayari vimeshafikishiwa huduma ya umeme. Vitongoji vingine 19 vipo kwenye mpango wa utekelezaji kupitia Mradi wa HEP II (B), huku vitongoji 6 vilivyobaki vikiwa ni hivyo vya Kisiwa cha Jibondo vinavyosubiri kuwashwa kwa umeme huo hivi karibuni.

Naye mmoja wa wakazi wa kisiwa hicho, Mzee Abdalah Hassan, ameishukuru Serikali kwa uwekezaji huo mkubwa na kueleza kuwa umeme huo utakuwa mkombozi mkubwa kwao.

"Umeme unahitajika kila mahali. Shuleni utasaidia kuchapisha mitihani na kujifunza kwa njia ya kompyuta, lakini pia utatupa wepesi wa kuandaa chakula na kuleta mwanga majumbani. Tumefarijika sana, ni faraja kubwa isiyo na kifani," amesema Mzee Abdalah.

-         MWISHO –

 

 

Read more
2930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top