Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya REA Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Gideon Kingu Akutana na Menejimenti
Aodax K. Nshala 1029

Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya REA Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Gideon Kingu Akutana na Menejimenti

Aipongeza kwa Kutekeleza Majukumu Yake Kwa Weledi

Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya Nishati Vijijini, Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Gideon Kingu amefanya mkutano wa kwanza na Menejimenti ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) leo tarehe 06 Oktoba 2023. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassam alimteua Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakala wa Nishati Vijijini tarehe 25 Septemba 2023.

Katika mkutano huo, Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan S. Saidy alimkaribisha Mwenyekiti na kufafanua Muundo na Majukumu ya Wakala kama yalivyoainishwa katika Sheria ya Nishati Vijijini Na. 5 ya Mwaka 2005. Aidha, Mkurugenzi Mkuu alieleza mipango na miradi iliyotekelezwa na Wakala tangu kuanzishwa kwake Mwaka 2007; mipango na miradi inayoendelea kutekelezwa; pamoja na mikakati itakayowezesha Serikali kufikia malengo ya kuhakikisha vijiji vyote vinafikiwa na huduma bora na za kisasa za nishati vijijini kufikia Mwaka 2025.

Mha. Hassan saidy alimweleza Mhe. Mwenyekiti kuwa, pamoja na miradi ya umeme vijijini inayopanua gridi ya Taifa, pia kuna miradi ya nishati jadidifu ambayo inatekelezwa katika maeneo ambayo ni mbali na gridi ya Taifa pamoja na maeneo ambayo hayafikiki kirahisi na miundombinu ya gridi ya Taifa ikiwa ni pamoja na maeneo ya visiwani. 

Mkurugenzi wa Umeme Vijijini, Mha. Jones Olotu alitoa maelezo kuwa, wakati Wakala unaanza kutekeleza majukumu yake Mwaka 2007, upatikanaji wa umeme vijijini ulikuwa umefikia asilimia 2 tu na jumla ya vijiji 506 kati ya vijiji 12,318 vya Tanzania Bara vilikuwa vimefikiwa na miundombinu  ya umeme. Tathmini iliyofanyika Mwaka 2020 ilionesha kuwa, hadi kufikia mwaka huo hali ya upatikanaji wa umeme vijijini ilifikia asilimia 69.6. Kwa sasa Wakala unaandaa kazi ya kutathmini hali ya upatikanaji umeme nchini kufikia mwaka 2025.

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Nishati Jadidifu na Teknolojia Mbadala, Mha. Emanuel Yesaya alieleza mipango na miradi ya Wakala ya kusambaza nishati safi ya kupikia ukiwemo mradi wa kusambaza mitungi ya gesi ya LPG 70,200 kwa ajili ya kuwapatia wananchi nishati safi na salama  ya kupikia; maendeleo ya mradi wa kujenga na kuendeleza vituo vya mafuta ya petroli na dizeli vijijini; uwezeshaji katika kutengeneza majiko banifu (Improved Cook Stoves); pamoja na kuwawezesha waendelezaji binafsi wanaotengeneza mkaa mbadala (briquettes). Aidha, kusimamia utekelezaji wa miradi ya gridi ndogo za umeme (mini grids) inayotekelezwa na waendelezaji miradi waliopata ruzuku mbalimbali kutoka kwa Wakala.

Mwenyekiti wa Bodi, Mhe. Balozi Meja Jenerali Mtaafu Jacob Gideon Kingu ameipongeza Menejimenti ya Wakala kwa namna ambavyo imekuwa ikitekeleza majukumu yake kwa weledi. Mwenyekiti ametoa rai kwamba, kama wataalamu tuhakikishe tunakamilisha utekelezaji wa majukumu na miradi kwa wakati. Amesisitiza kuwa, Wakala uhakikishe kuwa mikataba isimamiwe vizuri, manunuzi yafanyike kwa kufuata sheria, na malipo ya huduma mbalimbali yafuate tararibu ili kuepukana na hoja za ukaguzi.

Mwenyekiti alieleza kuwa atahakikisha anasaidia juhudi za Wakala katika utekelezaji wa shughuli na kwamba, watakapotangazwa wajumbe wa Bodi, watafanya kazi kwa pamoja na Menejimenti katika kufikia malengo ya Taifa kwamba, kila Kijiji na kila kitongoji kinafikiwa na huduma ya umeme.

Share

Print
«September 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
31123456
789
Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

IRINGA, Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini kwa kuendesha mafunzo maalum ya wiki moja yaliyolenga kujenga uwezo wa waendelezaji wa miradi midogo ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower).

Mafunzo hayo yaliyoanza tarehe 7 Septemba, 2026 katika Hoteli ya Sunset mkoani Iringa, yamewakutanisha waendelezaji wa miradi (Developers) zaidi ya 15, hususan kutoka maeneo ya Nyanda za Juu Kusini. Lengo kuu ni kuwajengea uwezo wa kiufundi ili kuongeza ubora wa miradi yao ili iweze kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, tarehe 9 Septemba, 2026, Kaimu Meneja wa Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi kutoka REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya, alisema kuwa REA haishii tu kutoa msaada wa upatikanaji wa nishati vijijini, bali inajikita pia katika kuongeza ujuzi wa wataalamu wa ndani.

"Kuongeza ujuzi kwa waendelezaji hawa kutasaidia kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu na ubora unaohitajika. Hatua hii itaongeza idadi ya miradi inayofikia vigezo vya kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa, kuongeza uzalishaji wa umeme, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii vijijini," alisema Mhandisi Yesaya.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ushirikiano kati ya REA na Wataalamu kutoka Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia (CoET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Maeneo yaliyofundishwa ni pamoja na usanifu wa miradi, upembuzi yakinifu, sayansi ya maji (hydrology), uhandisi wa umeme na elektroniki, pamoja na uendeshaji na matengenezo ya mitambo.

Mbali na mafunzo, REA imebainisha kuwa imekuwa ikisaidia waendelezaji hao kupitia ruzuku za ujenzi, maandalizi ya maandiko ya miradi na usanifu.

Aidha, Wakala huo upo katika mchakato wa kuandaa mfumo wa mikataba ya muda mrefu (Framework Contract) na taasisi za elimu ili kutoa mafunzo endelevu kwenye nishati jadidifu ikiwemo nishati ya jua na mifumo ya gesi vunde.

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wamepongeza mafunzo hayo; akizungumza na Wanahabari, Mhandisi Denis Makoyi kutoka kampuni ya Africa Power Investment, alisema mafunzo hayo yameongeza uelewa mkubwa wa kiufundi katika hatua za utekelezaji wa miradi. Naye Lutengano Kigola kutoka mradi wa Nyalawa Hydropower, aliongeza kuwa mafunzo hayo yanathibitisha kuwa Tanzania ina wataalamu wa ndani wenye uwezo mkubwa wa kuendeleza miradi ya umeme wa maji.

  • MWISHO –

 

Read more
10111213
14
REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuwezesha waendelezaji wadogo wa miradi ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kwa kutoa fedha, msaada wa kitaalamu na mafunzo, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa nishati nchini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top