Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya REA Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Gideon Kingu Akutana na Menejimenti
Aodax K. Nshala 412

Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya REA Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Gideon Kingu Akutana na Menejimenti

Aipongeza kwa Kutekeleza Majukumu Yake Kwa Weledi

Mwenyekiti Mpya wa Bodi ya Nishati Vijijini, Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Gideon Kingu amefanya mkutano wa kwanza na Menejimenti ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) leo tarehe 06 Oktoba 2023. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dk. Samia Suluhu Hassam alimteua Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakala wa Nishati Vijijini tarehe 25 Septemba 2023.

Katika mkutano huo, Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan S. Saidy alimkaribisha Mwenyekiti na kufafanua Muundo na Majukumu ya Wakala kama yalivyoainishwa katika Sheria ya Nishati Vijijini Na. 5 ya Mwaka 2005. Aidha, Mkurugenzi Mkuu alieleza mipango na miradi iliyotekelezwa na Wakala tangu kuanzishwa kwake Mwaka 2007; mipango na miradi inayoendelea kutekelezwa; pamoja na mikakati itakayowezesha Serikali kufikia malengo ya kuhakikisha vijiji vyote vinafikiwa na huduma bora na za kisasa za nishati vijijini kufikia Mwaka 2025.

Mha. Hassan saidy alimweleza Mhe. Mwenyekiti kuwa, pamoja na miradi ya umeme vijijini inayopanua gridi ya Taifa, pia kuna miradi ya nishati jadidifu ambayo inatekelezwa katika maeneo ambayo ni mbali na gridi ya Taifa pamoja na maeneo ambayo hayafikiki kirahisi na miundombinu ya gridi ya Taifa ikiwa ni pamoja na maeneo ya visiwani. 

Mkurugenzi wa Umeme Vijijini, Mha. Jones Olotu alitoa maelezo kuwa, wakati Wakala unaanza kutekeleza majukumu yake Mwaka 2007, upatikanaji wa umeme vijijini ulikuwa umefikia asilimia 2 tu na jumla ya vijiji 506 kati ya vijiji 12,318 vya Tanzania Bara vilikuwa vimefikiwa na miundombinu  ya umeme. Tathmini iliyofanyika Mwaka 2020 ilionesha kuwa, hadi kufikia mwaka huo hali ya upatikanaji wa umeme vijijini ilifikia asilimia 69.6. Kwa sasa Wakala unaandaa kazi ya kutathmini hali ya upatikanaji umeme nchini kufikia mwaka 2025.

Mwakilishi wa Mkurugenzi wa Nishati Jadidifu na Teknolojia Mbadala, Mha. Emanuel Yesaya alieleza mipango na miradi ya Wakala ya kusambaza nishati safi ya kupikia ukiwemo mradi wa kusambaza mitungi ya gesi ya LPG 70,200 kwa ajili ya kuwapatia wananchi nishati safi na salama  ya kupikia; maendeleo ya mradi wa kujenga na kuendeleza vituo vya mafuta ya petroli na dizeli vijijini; uwezeshaji katika kutengeneza majiko banifu (Improved Cook Stoves); pamoja na kuwawezesha waendelezaji binafsi wanaotengeneza mkaa mbadala (briquettes). Aidha, kusimamia utekelezaji wa miradi ya gridi ndogo za umeme (mini grids) inayotekelezwa na waendelezaji miradi waliopata ruzuku mbalimbali kutoka kwa Wakala.

Mwenyekiti wa Bodi, Mhe. Balozi Meja Jenerali Mtaafu Jacob Gideon Kingu ameipongeza Menejimenti ya Wakala kwa namna ambavyo imekuwa ikitekeleza majukumu yake kwa weledi. Mwenyekiti ametoa rai kwamba, kama wataalamu tuhakikishe tunakamilisha utekelezaji wa majukumu na miradi kwa wakati. Amesisitiza kuwa, Wakala uhakikishe kuwa mikataba isimamiwe vizuri, manunuzi yafanyike kwa kufuata sheria, na malipo ya huduma mbalimbali yafuate tararibu ili kuepukana na hoja za ukaguzi.

Mwenyekiti alieleza kuwa atahakikisha anasaidia juhudi za Wakala katika utekelezaji wa shughuli na kwamba, watakapotangazwa wajumbe wa Bodi, watafanya kazi kwa pamoja na Menejimenti katika kufikia malengo ya Taifa kwamba, kila Kijiji na kila kitongoji kinafikiwa na huduma ya umeme.

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top