Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Aihakikishia Ushirikiano Kampuni ya Kuzalisha na Kusambaza Umeme ya Matembwe Village Company ya Mkoani Njombe
Frank A. Mugogo 47

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Aihakikishia Ushirikiano Kampuni ya Kuzalisha na Kusambaza Umeme ya Matembwe Village Company ya Mkoani Njombe

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu ameihakikishia ushirikiano kampuni ya kuzalisha na kusambaza umeme ya Matembwe Village Company Limited ya Mkoani Njombe ili kuiwezesha kuongeza upatikanaji wa umeme na kuwafikia wananchi wengi zaidi waishio maeneo hayo.

Amethibitisha hayo alipofanya ziara katika mradi wa kuzalisha na kusambaza umeme wa Matembwe uliopo katika Tarafa ya Lupembe Wilaya ya Njombe Mkoani Njombe Juni 17, 2025.

"Nimekagua mradi mzima kuanzia eneo la uzalishaji na nimetembelea baadhi ya wanufaika wa mradi ili kujionea uendeshaji wake, uwezo wake na namna ambavyo mradi huu unanufaisha wananchi katika kujiletea maendeleo," alifafanua Mhe. Balozi Kingu.

Alisema ameridhishwa na namna ambavyo mradi huo wa Matembwe unavyofanya kazi na alisisitiza kuwa ipo haja ya kuongeza uzalishaji hasa ikizingatiwa kuwa maji yapo yakutosha.

Aliuthibitishia uongozi wa mradi kuwa Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) itaendelea kutoa ushirikiano wa kuhakikisha uwezeshwaji unaendelea ili kuleta tija inayokusudiwa.

"Kazi iliyofanyika hapa ni kubwa na inaridhisha, ni wakati wenu sasa kujipanga vizuri kuongeza uwezo wa uzalishaji wa umeme katika mradi huu ili walau mtoke kwenye kiwango mnachozalisha sasa cha kilowati 550 muweze kuzalisha umeme mwingi zaidi ili kuinua shughuli za kiuchumi na kijamii kwa wananchi wa maeneo haya na nchi nzima kwa ujumla ," alielekeza Mhe. Balozi Kingu.

Aliwasisitiza kuendelea kutunza mazingira ili kuwezesha miradi hii kuwa endelevu sambamba na kuwajengea uwezo vijana wa vijiji vinavyonufaika na mradi kwenye usimamizi na uendeshaji wa mradi.

"Vijana wanapaswa kutambua huu mradi ni wao; walianzisha babu zao na sasa wao wenyewe wananufaika," alisema.

Akizungumza hali ya uzalishaji na usambazaji umeme, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Matembwe, Johannes Kamonga alisema uhitaji wa umeme ni mkubwa hasa kipindi hiki ambacho viwanda vingi vinajengwa.

Aliipongeza REA kwa kuendelea kuuwezesha mradi huo na aliomba uwezeshaji uongezeke ili kuwezesha upanuzi wa mradi pamoja na kuunganisha wateja wengi zaidi

Alisema hapo awali mradi ulianza na kilowati 120 lakini kadri muda ulivyokwenda mahitaji yaliongezeka na hivyo walilazimika kutafuta uwezeshwaji ili kuongeza uzalishaji sambamba na kuongeza idadi ya wanufaika.

"Tunaishukuru REA kwani imekuwa bega kwa bega nasi, tulianza na vijiji viwili lakini kwa uwezeshwaji kutoka REA sasa tunahudumia vijiji nane," alisema Kamonga.

Akizungumzia uwezeshwaji wa mradi, Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala kutoka REA, Mhandisi Advera Mwijage alisema REA imechangia takriban shilingi bilioni moja kuuwezesha mradi kuunganisha wateja 357 sawa na 16.18%.

Alisema REA imewezesha kutekelezwa kwa miradi mbalimbali ya kuzalisha na kusambaza umeme vijijini katika maeneo mbalimbali ndani ya mikoa yote Tanzania Bara ili kuwezesha wananchi wengi kufikiwa na huduma bora ya Nishati, kupunguza uzalishaji wa hewa ya ukaa, kuongeza ajira nchini, kuongeza mapato serikalini na kuboresha maisha ya Watanzania waishio maeneo ya vijijini.

Aliongeza kuwa mradi unatumia teknolojia ya kusambaza umeme kwa kutumia nyaya zinazopita ardhini suala ambalo alisema huongeza usalama na kupunguza gharama za matengenezo.

"Kwa sasa REA ipo katika hatua ya kuongeza idadi ya kaya 95 kupitia mkataba wa ruzuku ya nyongeza ya fedha," alifafanua Mha. Mwijage.

Mhandisi Mwijage alifafanua kuwa REA imefadhili miradi ya uzalishaji na usambazaji nishati vijijini inayotekelezwa na taasisi mbalimbali za Serikali na Sekta Binafsi kwa kutoa ruzuku pamoja na kuwezesha mikopo ya masharti nafuu sambamba na kuwajengea uwezo waendelezaji wa miradi husika na miongoni mwa miradi iliyonufaika kwa Mkoa wa Njombe ni mradi huo wa Matembwe

Mradi wa kuzalisha na kusambaza umeme wa Matembwe unaendeshwa na kusimamiwa na Kampuni ya Matembwe Village Company Ltd iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Njombe kwa kushirikiana na Serikali za Vijiji vya Matembwe, Yembela na Ikondo.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«July 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
30
REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

Serikali imesambaza kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza (Gereza la Ukonga) mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko yake 464 ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kama njia ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia nchini ambapo msisitizo ni angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia Nishati Safi ifikapo Mwaka 2034.

Read more
1
Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa vitendo.

Read more
2
REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

Katika kuendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imegawa jumla ya mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko ya sahani mbili 461 kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Mara.

Read more
3
REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mpango wa kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petrol na dizeli) maeneo ya vijijini ili kuondoa madhara yatokanayo na njia zisizo salama.

Read more
4
Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewasihi Watanzania kote nchini kuachana na dhana ya kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni gharama ikilinganishwa na matumizi ya kuni na mkaa.

Read more
5
Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Imeelezwa kuwa hadi kufikia mwaka 2030 vitongoji vyote Tanzania Bara vitakuwa vimefikishiwa nishati ya umeme kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa na kusimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Read more
6
78
REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema Wakala umejizatiti kuhakikisha 80% ya Watanzania wanatumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo mwaka 2034 kama ilivyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
910111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top