Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Rais Samia Awaapisha Waziri na Naibu Waziri wa Nishati
Frank A. Mugogo 569

Rais Samia Awaapisha Waziri na Naibu Waziri wa Nishati

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Septemba 1, 2023 amewaapisha viongozi aliowateua hivi karibuni (Agosti 30, 2023) kushika nyadhifa mbalimbali akiwemo Mhe. Dkt. Doto Biteko kwa nafasi ya Naibu Waziri Mkuu (Uratibu wa Shughuli za Serikali) na Waziri wa Nishati pamoja na Mhe. Judith Kapinga kwa nafasi ya Naibu Waziri wa Nishati.

Hafla hiyo fupi ya uapisho imefanyika Ikulu Ndogo Tunguu Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali na Vyama vya Siasa.

Akitoa hotuba baada ya kuwaapisha viongozi hao, Rais Samia amewataka kila mmoja kwenda kukiishi kiapo alichoapa kwa kusimama katika nafasi zao zinazowataka kuwatumikia wananchi na kujenga mahusiano mema nao.

“Kiapo mlichoapa hata Mungu anakisikia hivyo naomba mkafanye hivyo mlivyoapa,” amesisitiza na kuongeza kuwa sifa ya upole kwa kiongozi siyo ujinga bali ni maarifa.

Aidha, Mheshimiwa Rais ameeleza kuwa mabadiliko aliyoyafanya katika uteuzi wa viongozi hao siyo adhabu bali ni ya kawaida yanayolenga kuimarisha utendaji kazi Serikalini.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Philip Mpango na Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa wamewapongeza viongozi walioteuliwa na kuwataka kwenda kutimiza wajibu wao ipasavyo.

Kwa upande wao, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Janet Mbene na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Hassan Saidy, wametoa pongezi kwa Viongozi wapya wa Wizara ya Nishati walioapishwa na kuwaahidi ushirikiano katika kutekeleza majukumu yao hususan katika sekta ya nishati vijijini.

Kabla ya uteuzi, Mhe. Dkt. Biteko alikuwa Waziri wa Madini na Mhe. Kapinga ni Mbunge wa Viti Maalum (Ruvuma).


Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini - REA
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Share

Print
«February 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
2627
Rais Samia Apeleka Neema ya Umeme Katika Vitongoji Lindi

Rais Samia Apeleka Neema ya Umeme Katika Vitongoji Lindi

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa shilingi bilioni 25.8 wa kusambaza umeme katika vitongoji 159 utakaonufaisha kaya 5,116 Mkoani Lindi.

Read more
2829
Shangwe Mtwara - Bilioni 15.3 Kusambaza Umeme Vitongoji 175

Shangwe Mtwara - Bilioni 15.3 Kusambaza Umeme Vitongoji 175

Wananchi wa vitongoji vya Msokole na Funguni Kijiji cha Mnazi Kata ya Nalingu Mkoani Mtwara wameishukuru Serikali kwa kuwapelekea mradi wa Umeme unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ambao wamesema unakwenda kubadili maisha yao.

Read more
3031
Mkandarasi Northern Engineering Atakiwa Kuongeza Kasi Ya Ujenzi Wa Mradi Mtwara

Mkandarasi Northern Engineering Atakiwa Kuongeza Kasi Ya Ujenzi Wa Mradi Mtwara

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemtaka Mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Kusambaza umeme katika Vitongoji 150 vya Majimbo 10 Mkoani Mtwara kuongeza kasi ya ujenzi ili kukamilisha Mradi kwa wakati.

Read more
1
2
Ukaguzi wa Mradi wa Kusambaza Umeme Mkoani Ruvuma

Ukaguzi wa Mradi wa Kusambaza Umeme Mkoani Ruvuma

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemtaka Mkandarasi Kampuni ya CCC International Engineering Nigeria Ltd anayetekeleza Mradi wa Kusambaza umeme katika Vitongoji 135 vya Majimbo 9 ya uchaguzi Mkoani Ruvuma kuongeza kasi ya ujenzi ili kukamilisha Mradi huo kwa wakati.

Read more
345678
9101112131415
16171819202122
2324252627281
2345678

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top