Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Rais Samia Awaapisha Waziri na Naibu Waziri wa Nishati
Frank A. Mugogo 246

Rais Samia Awaapisha Waziri na Naibu Waziri wa Nishati

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Septemba 1, 2023 amewaapisha viongozi aliowateua hivi karibuni (Agosti 30, 2023) kushika nyadhifa mbalimbali akiwemo Mhe. Dkt. Doto Biteko kwa nafasi ya Naibu Waziri Mkuu (Uratibu wa Shughuli za Serikali) na Waziri wa Nishati pamoja na Mhe. Judith Kapinga kwa nafasi ya Naibu Waziri wa Nishati.

Hafla hiyo fupi ya uapisho imefanyika Ikulu Ndogo Tunguu Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali na Vyama vya Siasa.

Akitoa hotuba baada ya kuwaapisha viongozi hao, Rais Samia amewataka kila mmoja kwenda kukiishi kiapo alichoapa kwa kusimama katika nafasi zao zinazowataka kuwatumikia wananchi na kujenga mahusiano mema nao.

“Kiapo mlichoapa hata Mungu anakisikia hivyo naomba mkafanye hivyo mlivyoapa,” amesisitiza na kuongeza kuwa sifa ya upole kwa kiongozi siyo ujinga bali ni maarifa.

Aidha, Mheshimiwa Rais ameeleza kuwa mabadiliko aliyoyafanya katika uteuzi wa viongozi hao siyo adhabu bali ni ya kawaida yanayolenga kuimarisha utendaji kazi Serikalini.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Philip Mpango na Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa wamewapongeza viongozi walioteuliwa na kuwataka kwenda kutimiza wajibu wao ipasavyo.

Kwa upande wao, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Janet Mbene na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Hassan Saidy, wametoa pongezi kwa Viongozi wapya wa Wizara ya Nishati walioapishwa na kuwaahidi ushirikiano katika kutekeleza majukumu yao hususan katika sekta ya nishati vijijini.

Kabla ya uteuzi, Mhe. Dkt. Biteko alikuwa Waziri wa Madini na Mhe. Kapinga ni Mbunge wa Viti Maalum (Ruvuma).


Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini - REA
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top