Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Rais Samia Awaapisha Waziri na Naibu Waziri wa Nishati
Frank A. Mugogo 231

Rais Samia Awaapisha Waziri na Naibu Waziri wa Nishati

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo Septemba 1, 2023 amewaapisha viongozi aliowateua hivi karibuni (Agosti 30, 2023) kushika nyadhifa mbalimbali akiwemo Mhe. Dkt. Doto Biteko kwa nafasi ya Naibu Waziri Mkuu (Uratibu wa Shughuli za Serikali) na Waziri wa Nishati pamoja na Mhe. Judith Kapinga kwa nafasi ya Naibu Waziri wa Nishati.

Hafla hiyo fupi ya uapisho imefanyika Ikulu Ndogo Tunguu Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali na Vyama vya Siasa.

Akitoa hotuba baada ya kuwaapisha viongozi hao, Rais Samia amewataka kila mmoja kwenda kukiishi kiapo alichoapa kwa kusimama katika nafasi zao zinazowataka kuwatumikia wananchi na kujenga mahusiano mema nao.

“Kiapo mlichoapa hata Mungu anakisikia hivyo naomba mkafanye hivyo mlivyoapa,” amesisitiza na kuongeza kuwa sifa ya upole kwa kiongozi siyo ujinga bali ni maarifa.

Aidha, Mheshimiwa Rais ameeleza kuwa mabadiliko aliyoyafanya katika uteuzi wa viongozi hao siyo adhabu bali ni ya kawaida yanayolenga kuimarisha utendaji kazi Serikalini.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, Makamu wa Rais, Mhe. Dkt. Philip Mpango na Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa wamewapongeza viongozi walioteuliwa na kuwataka kwenda kutimiza wajibu wao ipasavyo.

Kwa upande wao, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Janet Mbene na Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Mhandisi Hassan Saidy, wametoa pongezi kwa Viongozi wapya wa Wizara ya Nishati walioapishwa na kuwaahidi ushirikiano katika kutekeleza majukumu yao hususan katika sekta ya nishati vijijini.

Kabla ya uteuzi, Mhe. Dkt. Biteko alikuwa Waziri wa Madini na Mhe. Kapinga ni Mbunge wa Viti Maalum (Ruvuma).


Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini - REA
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Share

Print
«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top