Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA yawaneemesha wananchi kwa kukamilisha kituo cha kupoza umeme Ifakara
Frank A. Mugogo 231

REA yawaneemesha wananchi kwa kukamilisha kituo cha kupoza umeme Ifakara

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imekamilisha Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Kupoza Umeme kilichopo Ifakara (Ifakara Substation) na kuleta neema ya umeme wa uhakika kwa wananchi wa wilaya za Kilombero na Ulanga mkoani Morogoro, ambao walikuwa na changamoto ya kupata umeme mdogo na wenye kukatika mara kwa mara.

Kukamilika kwa Mradi wa ujenzi wa Kituo hicho chenye uwezo wa MVA 20 wa Msongo wa Kilovoti 220, kumetokana na mikakati mahsusi ya Serikali kupitia REA, inayolenga kuhakikisha wananchi wote wakiwemo waishio vijijini wanapatiwa umeme wa uhakika.

Akizungumza usiku wa Agosti 28 mwaka huu, wakati wa kuhitimisha zoezi la kuunga Kituo hicho kwenye Gridi ya Taifa, Meneja wa Mradi kutoka REA, Mhandisi Romanus Lwena alieleza kuwa azma ya kutekeleza Mradi huo ilifikiwa baada ya Wakala kubaini changamoto ya umeme mdogo waliyokuwa wakiipata wananchi wa maeneo hayo na hivyo kudhamiria kuitatua.

Mhandisi Lwena alisema, changamoto hiyo ya umeme mdogo imesababisha hali ya uwekezaji katika wilaya hizo kuwa chini pamoja na uwezo mzuri unaotokana na uwepo wa bidhaa za kilimo katika eneo hilo.

“Kwa hivyo, kukamilika kwa Mradi huu, kutawezesha sasa kufungua fursa za uwekezaji kutokana na kuwepo umeme wa uhakika. Pia, kutatatua changamoto ya kukatika umeme mara kwa mara na zaidi, wananchi sasa wataweza kufanya kazi za ujasiriamali za aina mbalimbali kwa ajili ya kukuza uchumi na kujiongezea kipato,” alisema Mhandisi Lwena.

Aidha, manufaa mengine yanayotokana na kukamilika kwa Mradi huu ni kwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuweza kupeleka umeme wa Gridi katika maeneo mengine yaliyo jirani ikiwemo Ulanga. Hii ni kufuatia REA kukamilisha kazi yake ya kujenga Mradi na kuukabidhi kwa TANESCO ambayo ndiyo huhusika na usimamizi na uendeshaji wa miundombinu yote ya umeme nchini.

Mradi wa Kituo cha Kupoza Umeme Ifakara, ulikuwa na mafungu mawili, moja likiwa ni ujenzi wa Kituo hicho na jingine linahusisha usambazaji wa nishati ya umeme kwa wananchi ambayo yote yamekamilika na kubaki kazi ndogo ya kukamilisha kuhakiki vifaa vilivyoungwa ili kuhakikisha viko sawa tayari kwa kuanza kutumika.

Mradi umegharimu jumla ya Euro Milioni 8.75 ambazo ni takribani shilingi bilioni 22 za Tanzania ambapo kati yake, Euro Milioni 2.25 ni fedha za Serikali na Euro Milioni 6.5 ni ufadhili kutoka Umoja wa Ulaya.


Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini - REA
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Rate article

No rating
Rate this article:
No rating

Share

Print
«April 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
25
Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa  Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za  Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini unakaribisha maombi ya mkopo nafuu kuwezesha ujenzi wa vituo vidogo vya kuuzia bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) vijijini. Mkopo huu utasaidia uwezeshaji wa ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini ili kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya mafuta kwa gharama nafuu, kwa njia salama, na isiyo na madhara kwa mazingira.

Wakala unawasisitiza waombaji walioomba katika awamu ya kwanza na kutokidhi vigezo kuomba tena baada ya kufanya marekebisho  ya  mapungufu yaliyobainishwa katika maombi yao. Aidha maombi mapya ya mkopo yanakaribishwa.

Read more
262728293031
12345
Call for Proposals for Results Based Financing (RBF) Application for Stand Alone Solar Home System (SA-SHS)

Call for Proposals for Results Based Financing (RBF) Application for Stand Alone Solar Home System (SA-SHS)

The Rural Energy Agency (REA) invites eligible firms to apply for grant per new SA-SHS installation in targeted rural communities. The grant includes end-user buying price system subsidization and firm’s performance incentive. The SA-SHS grant application is implemented through the program for Tanzania Rural Electrification Expansion Program Additional Financing (TREEP AF) which is supported by the World Bank.

Read more
67
891011121314
15
Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA

Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA


Wabia wa Maendeleo ambao wanafadhili miradi ya kusambaza nishati vijijini wamepongeza Wakala wa Nishati Vijijini kwa utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini ambayo inaleta tija kwa ustawi wa wananchi.

Read more
161718192021
222324
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25

Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25

Hotuba ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mheshimiwa Dkt. Doto Mashaka Biteko (Mb), Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25.

Read more
25262728
293012345

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top