Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA yawaneemesha wananchi kwa kukamilisha kituo cha kupoza umeme Ifakara
Frank A. Mugogo 255

REA yawaneemesha wananchi kwa kukamilisha kituo cha kupoza umeme Ifakara

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imekamilisha Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Kupoza Umeme kilichopo Ifakara (Ifakara Substation) na kuleta neema ya umeme wa uhakika kwa wananchi wa wilaya za Kilombero na Ulanga mkoani Morogoro, ambao walikuwa na changamoto ya kupata umeme mdogo na wenye kukatika mara kwa mara.

Kukamilika kwa Mradi wa ujenzi wa Kituo hicho chenye uwezo wa MVA 20 wa Msongo wa Kilovoti 220, kumetokana na mikakati mahsusi ya Serikali kupitia REA, inayolenga kuhakikisha wananchi wote wakiwemo waishio vijijini wanapatiwa umeme wa uhakika.

Akizungumza usiku wa Agosti 28 mwaka huu, wakati wa kuhitimisha zoezi la kuunga Kituo hicho kwenye Gridi ya Taifa, Meneja wa Mradi kutoka REA, Mhandisi Romanus Lwena alieleza kuwa azma ya kutekeleza Mradi huo ilifikiwa baada ya Wakala kubaini changamoto ya umeme mdogo waliyokuwa wakiipata wananchi wa maeneo hayo na hivyo kudhamiria kuitatua.

Mhandisi Lwena alisema, changamoto hiyo ya umeme mdogo imesababisha hali ya uwekezaji katika wilaya hizo kuwa chini pamoja na uwezo mzuri unaotokana na uwepo wa bidhaa za kilimo katika eneo hilo.

“Kwa hivyo, kukamilika kwa Mradi huu, kutawezesha sasa kufungua fursa za uwekezaji kutokana na kuwepo umeme wa uhakika. Pia, kutatatua changamoto ya kukatika umeme mara kwa mara na zaidi, wananchi sasa wataweza kufanya kazi za ujasiriamali za aina mbalimbali kwa ajili ya kukuza uchumi na kujiongezea kipato,” alisema Mhandisi Lwena.

Aidha, manufaa mengine yanayotokana na kukamilika kwa Mradi huu ni kwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuweza kupeleka umeme wa Gridi katika maeneo mengine yaliyo jirani ikiwemo Ulanga. Hii ni kufuatia REA kukamilisha kazi yake ya kujenga Mradi na kuukabidhi kwa TANESCO ambayo ndiyo huhusika na usimamizi na uendeshaji wa miundombinu yote ya umeme nchini.

Mradi wa Kituo cha Kupoza Umeme Ifakara, ulikuwa na mafungu mawili, moja likiwa ni ujenzi wa Kituo hicho na jingine linahusisha usambazaji wa nishati ya umeme kwa wananchi ambayo yote yamekamilika na kubaki kazi ndogo ya kukamilisha kuhakiki vifaa vilivyoungwa ili kuhakikisha viko sawa tayari kwa kuanza kutumika.

Mradi umegharimu jumla ya Euro Milioni 8.75 ambazo ni takribani shilingi bilioni 22 za Tanzania ambapo kati yake, Euro Milioni 2.25 ni fedha za Serikali na Euro Milioni 6.5 ni ufadhili kutoka Umoja wa Ulaya.


Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini - REA
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Rate article

No rating
Rate this article:
No rating

Share

Print
«July 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
24252627282930
1234
National Clean Cooking Strategy (2024 – 2034)

National Clean Cooking Strategy (2024 – 2034)

The Government of the United Republic of Tanzania, in collaboration with various stakeholders has prepared the National Clean Cooking Strategy. The strategy aims to ensure that 80 percent of Tanzanians use clean cooking solutions by the year 2034.

Read more
567
891011121314
15161718192021
Vijiji 151 Vimebaki Nchi Nzima Kupata Huduma ya Umeme – Kapinga

Vijiji 151 Vimebaki Nchi Nzima Kupata Huduma ya Umeme – Kapinga

Ni vijiji 151 tu nchi nzima ndio ambavyo bado havijafikiwa na huduma ya umeme kati ya Vijiji zaidi ya 12,000 ambapo wilayani Ludewa mkoani Njombe vimebaki Vijiji nane.

Read more
22232425262728
2930311234

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top