Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA yawaneemesha wananchi kwa kukamilisha kituo cha kupoza umeme Ifakara
Frank A. Mugogo 748

REA yawaneemesha wananchi kwa kukamilisha kituo cha kupoza umeme Ifakara

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imekamilisha Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Kupoza Umeme kilichopo Ifakara (Ifakara Substation) na kuleta neema ya umeme wa uhakika kwa wananchi wa wilaya za Kilombero na Ulanga mkoani Morogoro, ambao walikuwa na changamoto ya kupata umeme mdogo na wenye kukatika mara kwa mara.

Kukamilika kwa Mradi wa ujenzi wa Kituo hicho chenye uwezo wa MVA 20 wa Msongo wa Kilovoti 220, kumetokana na mikakati mahsusi ya Serikali kupitia REA, inayolenga kuhakikisha wananchi wote wakiwemo waishio vijijini wanapatiwa umeme wa uhakika.

Akizungumza usiku wa Agosti 28 mwaka huu, wakati wa kuhitimisha zoezi la kuunga Kituo hicho kwenye Gridi ya Taifa, Meneja wa Mradi kutoka REA, Mhandisi Romanus Lwena alieleza kuwa azma ya kutekeleza Mradi huo ilifikiwa baada ya Wakala kubaini changamoto ya umeme mdogo waliyokuwa wakiipata wananchi wa maeneo hayo na hivyo kudhamiria kuitatua.

Mhandisi Lwena alisema, changamoto hiyo ya umeme mdogo imesababisha hali ya uwekezaji katika wilaya hizo kuwa chini pamoja na uwezo mzuri unaotokana na uwepo wa bidhaa za kilimo katika eneo hilo.

“Kwa hivyo, kukamilika kwa Mradi huu, kutawezesha sasa kufungua fursa za uwekezaji kutokana na kuwepo umeme wa uhakika. Pia, kutatatua changamoto ya kukatika umeme mara kwa mara na zaidi, wananchi sasa wataweza kufanya kazi za ujasiriamali za aina mbalimbali kwa ajili ya kukuza uchumi na kujiongezea kipato,” alisema Mhandisi Lwena.

Aidha, manufaa mengine yanayotokana na kukamilika kwa Mradi huu ni kwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuweza kupeleka umeme wa Gridi katika maeneo mengine yaliyo jirani ikiwemo Ulanga. Hii ni kufuatia REA kukamilisha kazi yake ya kujenga Mradi na kuukabidhi kwa TANESCO ambayo ndiyo huhusika na usimamizi na uendeshaji wa miundombinu yote ya umeme nchini.

Mradi wa Kituo cha Kupoza Umeme Ifakara, ulikuwa na mafungu mawili, moja likiwa ni ujenzi wa Kituo hicho na jingine linahusisha usambazaji wa nishati ya umeme kwa wananchi ambayo yote yamekamilika na kubaki kazi ndogo ya kukamilisha kuhakiki vifaa vilivyoungwa ili kuhakikisha viko sawa tayari kwa kuanza kutumika.

Mradi umegharimu jumla ya Euro Milioni 8.75 ambazo ni takribani shilingi bilioni 22 za Tanzania ambapo kati yake, Euro Milioni 2.25 ni fedha za Serikali na Euro Milioni 6.5 ni ufadhili kutoka Umoja wa Ulaya.


Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini - REA
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Share

Print
«August 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
272829303112
3456789
1011121314
REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefanikiwa kusambaza takribani mitungi laki saba ya gesi ya kupikia (LPG) nchini kote, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa kasi wa Mkakati wa Kitaifa wa Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
1516
1718

Maombi ya Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unakaribisha waombaji wenye vigezo kuomba mkopo wa kuwezesha ujenzi wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) ili kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini.

Pamoja na tangazo hili, tumeweka viambatanisho vifuatavyo:
•    Tangazo la fursa ya mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta ya Petroli na Dizeli vijijini.
•    Mwongozo wa utoaji mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta vijijini.
•    Fomu ya Maombi ya Mkopo.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la REA
Mtaa wa Medeli
P. O. Box 2153,
DODOMA, TANZANIA.

Read more
1920212223
2425262728
Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Yaridhishwa na Usambazaji wa Umeme Kisiwani Jibondo

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) Yaridhishwa na Usambazaji wa Umeme Kisiwani Jibondo

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) imeeleza kuridhishwa kwake na kasi ya usambazaji wa nishati ya umeme katika vitongoji vya Kisiwa cha Jibondo, kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mafia, mkoani Pwani.

Hayo yamebainishwa na Mwenyekiti wa REB, Mhe. Balozi na Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu, tarehe 27 Agosti, 2026 alipoambatana na Menejimenti ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kisiwani humo kukagua maendeleo ya mradi huo mkubwa ambao tayari umegharimu kiasi cha shilingi bilioni 8.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Meja Jenerali Kingu amesema kuwa kwa mara ya kwanza katika historia, vitongoji vya Kisiwa cha Jibondo vinatarajia kupata huduma hiyo ya nishati hivi karibuni. Alifafanua kuwa kazi kubwa iliyobaki kwa sasa ni ya usafirishaji wa umeme kwa kutumia waya maalum wa chini ya maji (Submarine cable) kutoka kisiwa kidogo cha Juani kwenda Jibondo, kazi inayotarajiwa kuanza kesho, tarehe 29 Agosti 2026, na kukamilika baada ya siku tano.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy, amesema kuwa maandalizi yote ya miundombinu ikiwemo ujenzi wa njia za kusafirisha umeme ndani ya kisiwa hicho yamekamika kwa asilimia 90 na ameongeza kuwa mara baada ya nyaya hizo za chini ya maji kuunganishwa, wananchi wataanza kuunganishiwa huduma hiyo mara moja.

Mhandisi Saidy amebainisha kuwa mradi huo umefanikiwa kwa ushirikiano wa REA iliyochangia shilingi bilioni 6.8 na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) lililochangia shilingi bilioni 2.

Katika hatua nyingine, Mhandisi Saidy ametoa wito kwa wakazi wa Jibondo kujiandaa kiuchumi ili kuutumia umeme huo katika kuboresha maisha yao na kuendesha shughuli za kimaendeleo, hasa ikizingatiwa kuwa sehemu kubwa ya wakazi wa eneo hilo wamejiajiri kwenye sekta za uvuvi, usindikaji wa mazao ya bahari, na kilimo cha mwani.

Wilaya ya Mafia ina jumla ya vitongoji 136, ambapo vitongoji 111 tayari vimeshafikishiwa huduma ya umeme. Vitongoji vingine 19 vipo kwenye mpango wa utekelezaji kupitia Mradi wa HEP II (B), huku vitongoji 6 vilivyobaki vikiwa ni hivyo vya Kisiwa cha Jibondo vinavyosubiri kuwashwa kwa umeme huo hivi karibuni.

Naye mmoja wa wakazi wa kisiwa hicho, Mzee Abdalah Hassan, ameishukuru Serikali kwa uwekezaji huo mkubwa na kueleza kuwa umeme huo utakuwa mkombozi mkubwa kwao.

"Umeme unahitajika kila mahali. Shuleni utasaidia kuchapisha mitihani na kujifunza kwa njia ya kompyuta, lakini pia utatupa wepesi wa kuandaa chakula na kuleta mwanga majumbani. Tumefarijika sana, ni faraja kubwa isiyo na kifani," amesema Mzee Abdalah.

-         MWISHO –

 

 

Read more
2930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top