Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA yawaneemesha wananchi kwa kukamilisha kituo cha kupoza umeme Ifakara
Frank A. Mugogo 352

REA yawaneemesha wananchi kwa kukamilisha kituo cha kupoza umeme Ifakara

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imekamilisha Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Kupoza Umeme kilichopo Ifakara (Ifakara Substation) na kuleta neema ya umeme wa uhakika kwa wananchi wa wilaya za Kilombero na Ulanga mkoani Morogoro, ambao walikuwa na changamoto ya kupata umeme mdogo na wenye kukatika mara kwa mara.

Kukamilika kwa Mradi wa ujenzi wa Kituo hicho chenye uwezo wa MVA 20 wa Msongo wa Kilovoti 220, kumetokana na mikakati mahsusi ya Serikali kupitia REA, inayolenga kuhakikisha wananchi wote wakiwemo waishio vijijini wanapatiwa umeme wa uhakika.

Akizungumza usiku wa Agosti 28 mwaka huu, wakati wa kuhitimisha zoezi la kuunga Kituo hicho kwenye Gridi ya Taifa, Meneja wa Mradi kutoka REA, Mhandisi Romanus Lwena alieleza kuwa azma ya kutekeleza Mradi huo ilifikiwa baada ya Wakala kubaini changamoto ya umeme mdogo waliyokuwa wakiipata wananchi wa maeneo hayo na hivyo kudhamiria kuitatua.

Mhandisi Lwena alisema, changamoto hiyo ya umeme mdogo imesababisha hali ya uwekezaji katika wilaya hizo kuwa chini pamoja na uwezo mzuri unaotokana na uwepo wa bidhaa za kilimo katika eneo hilo.

“Kwa hivyo, kukamilika kwa Mradi huu, kutawezesha sasa kufungua fursa za uwekezaji kutokana na kuwepo umeme wa uhakika. Pia, kutatatua changamoto ya kukatika umeme mara kwa mara na zaidi, wananchi sasa wataweza kufanya kazi za ujasiriamali za aina mbalimbali kwa ajili ya kukuza uchumi na kujiongezea kipato,” alisema Mhandisi Lwena.

Aidha, manufaa mengine yanayotokana na kukamilika kwa Mradi huu ni kwa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuweza kupeleka umeme wa Gridi katika maeneo mengine yaliyo jirani ikiwemo Ulanga. Hii ni kufuatia REA kukamilisha kazi yake ya kujenga Mradi na kuukabidhi kwa TANESCO ambayo ndiyo huhusika na usimamizi na uendeshaji wa miundombinu yote ya umeme nchini.

Mradi wa Kituo cha Kupoza Umeme Ifakara, ulikuwa na mafungu mawili, moja likiwa ni ujenzi wa Kituo hicho na jingine linahusisha usambazaji wa nishati ya umeme kwa wananchi ambayo yote yamekamilika na kubaki kazi ndogo ya kukamilisha kuhakiki vifaa vilivyoungwa ili kuhakikisha viko sawa tayari kwa kuanza kutumika.

Mradi umegharimu jumla ya Euro Milioni 8.75 ambazo ni takribani shilingi bilioni 22 za Tanzania ambapo kati yake, Euro Milioni 2.25 ni fedha za Serikali na Euro Milioni 6.5 ni ufadhili kutoka Umoja wa Ulaya.


Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini - REA
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Share

Print
«July 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
30
REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

Serikali imesambaza kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza (Gereza la Ukonga) mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko yake 464 ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kama njia ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia nchini ambapo msisitizo ni angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia Nishati Safi ifikapo Mwaka 2034.

Read more
1
Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa vitendo.

Read more
2
REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

Katika kuendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imegawa jumla ya mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko ya sahani mbili 461 kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Mara.

Read more
3
REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mpango wa kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petrol na dizeli) maeneo ya vijijini ili kuondoa madhara yatokanayo na njia zisizo salama.

Read more
4
Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewasihi Watanzania kote nchini kuachana na dhana ya kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni gharama ikilinganishwa na matumizi ya kuni na mkaa.

Read more
5
Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Imeelezwa kuwa hadi kufikia mwaka 2030 vitongoji vyote Tanzania Bara vitakuwa vimefikishiwa nishati ya umeme kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa na kusimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Read more
6
78
REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema Wakala umejizatiti kuhakikisha 80% ya Watanzania wanatumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo mwaka 2034 kama ilivyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
910111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top