Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Kufunga Mifumo ya Nishati Safi ya Kupikia Shule ya Ruhinda
Frank A. Mugogo 656

REA Kufunga Mifumo ya Nishati Safi ya Kupikia Shule ya Ruhinda

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeahidi kujenga mifumo ya nishati safi ya kupikia pamoja na jiko katika shule ya Sekondari ya mchanganyiko ya Ruhinda iliyopo Wilaya ya Karagwe Mkoani Kagera.
 
Ahadi hiyo imetolewa leo Novemba 7, 2024 na Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy wakati wa muendelezo wa ziara ya viongozi mbalimbali wa Serikali waliambatana na Wabia hao wa Maendeleo ambao Serikali imekuwa ikishirikiana na kuwezesha upatikanaji wa nishati bora vijijini. Wabia hao ni Benki ya Dunia, Serikali ya Norway, Serikali ya Sweden, Umoja wa Ulaya, AFD na ADB.
 
Wakati wa ziara hiyo ambayo ililenga kutembelea miradi inayotekelezwa na Wakala huo, viongozi hao walitembelea Shule ya Sekondari ya Mchanganyiko ya Ruhinda ambapo katika risala yao, waliomba kupatiwa mfumo wa nishati safi ya kupikia.
 
“Tumeskia ombi lenu la kutamani kuwa na nishati safi ya kupikia hapa shuleni. Tutaenda kufanya tathmini na kuangalia nishati safi ipi itakayofaa zaidi. Tunaweza kuwa na mifumo hata miwili; mfumo wa gesi na mfumo wa majiko banifu ambayo yanatumia kuni kidogo na ni rafiki kwa mazingira.
 
Lakini pia kwa kuwa mifumo hii tunayotarajia kwenda kuifunga ni ya thamani na ya gharama kubwa. Pia tutawajengea na jengo la jiko zuri,” amesema Mkurugenzi Mkuu huyo.
 
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali (mstaafu), Jacob Kingu amesema Wakala huo umekuwa ukiishi kwa vitendo maelekezo ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk, Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni kinara wa nishati safi wa kupikia Afrika na Duniani kwa ujumla na kuongeza kuwa ujenzi wa mifumo ya kupikia katika shule hiyo ni kielelezo tosha cha utayari wa REA kupambana na nishati zisizo safi katika jamii.
 
“Tunajua shule ikibadilika kwa kutumia nishati safi ya kupikia hata wananchi wanaoizunguka shule hii pia watabadilika,” amesema Mwenyekiti Kingu.
 
Awali akisoma taarifa ya shule hiyo, Mkuu wa Shule hiyo, Ambruce Katorogo amesema kuwa shule hiyo inatumia Zaidi ya shilingi 800,000/= kila mwezi kwa ajili ya kununua kuni zinazotumika kupikia chakula cha wanafunzi shuleni hapo.
 
Awali Mkuu huyo wa shule pia aliishukuru Serikali kupitia REA kwa kuwezesha kufikisha nishati ya umeme katika shule hiyo ambapo imesaidia kuongeza usalama hasa kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum katika shule hiyo.
 
Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano kutoka REA, Bi. Martha Chassama ameendelea kuhamasisha wananchi kuendelea kutumia nishati safi ya kupikia na kusisitiza kuwa Wakala huo unaendelea na kampeni zake mbalimbali kuhamasisha wananchi wanajua madhara yatokanayo na nishati chafu ya kupikia.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«September 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
31123456
789
Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

IRINGA, Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini kwa kuendesha mafunzo maalum ya wiki moja yaliyolenga kujenga uwezo wa waendelezaji wa miradi midogo ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower).

Mafunzo hayo yaliyoanza tarehe 7 Septemba, 2026 katika Hoteli ya Sunset mkoani Iringa, yamewakutanisha waendelezaji wa miradi (Developers) zaidi ya 15, hususan kutoka maeneo ya Nyanda za Juu Kusini. Lengo kuu ni kuwajengea uwezo wa kiufundi ili kuongeza ubora wa miradi yao ili iweze kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, tarehe 9 Septemba, 2026, Kaimu Meneja wa Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi kutoka REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya, alisema kuwa REA haishii tu kutoa msaada wa upatikanaji wa nishati vijijini, bali inajikita pia katika kuongeza ujuzi wa wataalamu wa ndani.

"Kuongeza ujuzi kwa waendelezaji hawa kutasaidia kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu na ubora unaohitajika. Hatua hii itaongeza idadi ya miradi inayofikia vigezo vya kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa, kuongeza uzalishaji wa umeme, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii vijijini," alisema Mhandisi Yesaya.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ushirikiano kati ya REA na Wataalamu kutoka Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia (CoET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Maeneo yaliyofundishwa ni pamoja na usanifu wa miradi, upembuzi yakinifu, sayansi ya maji (hydrology), uhandisi wa umeme na elektroniki, pamoja na uendeshaji na matengenezo ya mitambo.

Mbali na mafunzo, REA imebainisha kuwa imekuwa ikisaidia waendelezaji hao kupitia ruzuku za ujenzi, maandalizi ya maandiko ya miradi na usanifu.

Aidha, Wakala huo upo katika mchakato wa kuandaa mfumo wa mikataba ya muda mrefu (Framework Contract) na taasisi za elimu ili kutoa mafunzo endelevu kwenye nishati jadidifu ikiwemo nishati ya jua na mifumo ya gesi vunde.

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wamepongeza mafunzo hayo; akizungumza na Wanahabari, Mhandisi Denis Makoyi kutoka kampuni ya Africa Power Investment, alisema mafunzo hayo yameongeza uelewa mkubwa wa kiufundi katika hatua za utekelezaji wa miradi. Naye Lutengano Kigola kutoka mradi wa Nyalawa Hydropower, aliongeza kuwa mafunzo hayo yanathibitisha kuwa Tanzania ina wataalamu wa ndani wenye uwezo mkubwa wa kuendeleza miradi ya umeme wa maji.

  • MWISHO –

 

Read more
10111213
14
REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuwezesha waendelezaji wadogo wa miradi ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kwa kutoa fedha, msaada wa kitaalamu na mafunzo, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa nishati nchini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top