Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Kufunga Mifumo ya Nishati Safi ya Kupikia Shule ya Ruhinda
Frank A. Mugogo 247

REA Kufunga Mifumo ya Nishati Safi ya Kupikia Shule ya Ruhinda

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeahidi kujenga mifumo ya nishati safi ya kupikia pamoja na jiko katika shule ya Sekondari ya mchanganyiko ya Ruhinda iliyopo Wilaya ya Karagwe Mkoani Kagera.
 
Ahadi hiyo imetolewa leo Novemba 7, 2024 na Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Hassan Saidy wakati wa muendelezo wa ziara ya viongozi mbalimbali wa Serikali waliambatana na Wabia hao wa Maendeleo ambao Serikali imekuwa ikishirikiana na kuwezesha upatikanaji wa nishati bora vijijini. Wabia hao ni Benki ya Dunia, Serikali ya Norway, Serikali ya Sweden, Umoja wa Ulaya, AFD na ADB.
 
Wakati wa ziara hiyo ambayo ililenga kutembelea miradi inayotekelezwa na Wakala huo, viongozi hao walitembelea Shule ya Sekondari ya Mchanganyiko ya Ruhinda ambapo katika risala yao, waliomba kupatiwa mfumo wa nishati safi ya kupikia.
 
“Tumeskia ombi lenu la kutamani kuwa na nishati safi ya kupikia hapa shuleni. Tutaenda kufanya tathmini na kuangalia nishati safi ipi itakayofaa zaidi. Tunaweza kuwa na mifumo hata miwili; mfumo wa gesi na mfumo wa majiko banifu ambayo yanatumia kuni kidogo na ni rafiki kwa mazingira.
 
Lakini pia kwa kuwa mifumo hii tunayotarajia kwenda kuifunga ni ya thamani na ya gharama kubwa. Pia tutawajengea na jengo la jiko zuri,” amesema Mkurugenzi Mkuu huyo.
 
Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali (mstaafu), Jacob Kingu amesema Wakala huo umekuwa ukiishi kwa vitendo maelekezo ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk, Samia Suluhu Hassan ambaye pia ni kinara wa nishati safi wa kupikia Afrika na Duniani kwa ujumla na kuongeza kuwa ujenzi wa mifumo ya kupikia katika shule hiyo ni kielelezo tosha cha utayari wa REA kupambana na nishati zisizo safi katika jamii.
 
“Tunajua shule ikibadilika kwa kutumia nishati safi ya kupikia hata wananchi wanaoizunguka shule hii pia watabadilika,” amesema Mwenyekiti Kingu.
 
Awali akisoma taarifa ya shule hiyo, Mkuu wa Shule hiyo, Ambruce Katorogo amesema kuwa shule hiyo inatumia Zaidi ya shilingi 800,000/= kila mwezi kwa ajili ya kununua kuni zinazotumika kupikia chakula cha wanafunzi shuleni hapo.
 
Awali Mkuu huyo wa shule pia aliishukuru Serikali kupitia REA kwa kuwezesha kufikisha nishati ya umeme katika shule hiyo ambapo imesaidia kuongeza usalama hasa kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum katika shule hiyo.
 
Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano kutoka REA, Bi. Martha Chassama ameendelea kuhamasisha wananchi kuendelea kutumia nishati safi ya kupikia na kusisitiza kuwa Wakala huo unaendelea na kampeni zake mbalimbali kuhamasisha wananchi wanajua madhara yatokanayo na nishati chafu ya kupikia.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«September 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
25262728293031
1234
Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

Deadline for submission of Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts has been extended up to 15th September 2025.

The Rural Energy Agency (REA) is seeking proposals from qualified service providers for the supply, installation, and testing of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in eight remote villages across Geita, Ludewa and Mbulu districts. Those villages are located in remote areas with challenging geographical conditions, hence, impractical for grid extension.

Please find the attached documents:

•    Application Form for Supply and Installation of SA-SHS; and
•    Call for Proposals for Result Based Financing Installation of Stand Alone Solar Home Systems.

Read more
567
Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Ahamasisha Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Ahamasisha Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru wa Kitaifa, Ismail Ali Ussi amewahamasisha wananchi kuunga mkono kampeni ya nishati safi ya kupikia ili kulinda afya pamoja kuokoa mazingira.

Read more
8910
Dkt. Biteko Aimwagia Sifa REA, Ataka Taasisi Zingine Ziige

Dkt. Biteko Aimwagia Sifa REA, Ataka Taasisi Zingine Ziige

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Mashaka Biteko ameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kukamilisha lengo la usambazaji Umeme katika Vijiji 12,318 Nchini na kwa umahiri wake katika kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
11121314
15161718192021
22232425262728
293012345

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top