Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Yaanza Kusambaza Umeme Vitongoji Morogoro
Frank A. Mugogo 244

REA Yaanza Kusambaza Umeme Vitongoji Morogoro

Serikali kupitia Wakala  wa Nishati Vijijini (REA) imeanza kusambaza Umeme kwenye Vitongoji 166 vilivyopo Mkoa wa Morogoro baada ya kukamilisha nishati hiyo kwenye Vijiji 652 kati ya 669  sawa na Asilimia 97.5.
 
Mradi huo wenye gharama ya shilingi bilioni 17.9 unatarajiwa kutekelezwa katika kipindi cha miezi 24 na utakapokamilika utanufaisha zaidi ya Kaya 5,478.
 
Akizungumza wakati wa hafla fupi ya kumtambulisha Mkandarasi huyo ambaye ni kampuni ya SINOTEC CO. LTD, Mkuu wa Mkoa wa Morogoro, Mhe. Adam Kighoma Malima amemshukuru Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha hizo pamoja na kuwapongeza REA kwa kusimamia vyema maono ya Mhe. Rais kuhakikisha wananchi vijijini nao wanapata maendeleo kupitia upatikanaji wa nishati ya umeme.
 
“Mkoa wa Morogoro ni mkoa wa kimkakati, Mkoa wa uzalishaji na tumejipanga kuwa Mkoa namba moja katika kilimo nchini. Na kuwepo kwa umeme maeneo ya vijijini kutasaidia kuongeza thamani ya mazao ya kilimo. Umeme ndio nguzo namba moja katika kuongeza thamani mazao ya kilimo. Tuendelee kumpongeza na kumshkuru Mhe. Rais kwa kutoa fedha zinazoenda kuwezesha zaidi ya Vitongoji 166 vinapata umeme,” amesema Mhe. Malima.
 
Mhe. Malima pia ameendelea kuwasisitiza wananchi kutunza miundombinu ya umeme na kumtaka pia mkandarasi huyo kuhakikisha anatekeleza mradi huo ndani ya muda uliopangwa na kwa viwango vya ubora vinavyokubalika.
 
Awali akitoa taarifa ya upelekaji wa umeme Vijijini, Mhandisi Msimamizi wa Miradi ya REA Kanda ya Kati, Mhandisi Aneth Malingumu amesema kuwa kati ya Vijiji 669 katika Mkoa wa Morogoro, Vijiji 652 ambavyo ni sawa na asilimia 97.5 vimefikiwa na nishati ya umeme na kuongeza kuwa vijiji 17 vilivyobaki viko kwenye hatua za miwisho za ukamilishaji na kabla ya Oktoba 20 vitakuwa vimepata umeme.
 
Kwa upande wa Vitongoji, Mhandisi Malingumu amesema kuwa Mkoa wa Morogoro unajumla ya Vitongoji 3,369 na katika hivyo, Vitongoji 1,655 sawa na asilimia 49 tayari vimepatiwa umeme.
 
“Katika kipindi cha miaka miwili tunategemea vitongoji 455 vya Mkoa wa Morogoro vitapatiwa umeme. Ndani ya hivyo, 289 mkandarasi tayari yuko site na anaendelea na kazi kupitia mradi wa ujazilizi yaani Densification IIB. Aidha, vitongoji 166 vitapatiwa umeme kupitia mradi huu tunaotambulisha mkandarasi wake leo kwa gharama ya shilingi Bilioni 17.9.” Amefafanua Mhandisi Malingumu.
 
Mhandisi Malingumu pia amemuhakikishia Mkuu huyo wa Mkoa kuwa REA imejipanga vyema kuhakikisha umeme unafika kwenye vijiji vyote na safari ya kupeleka umeme katika vitongoji inaendelea kulingana na upatikanaji wa fedha.
 
Kwa upande wake Mwakilishi wa Kampuni SINOTEC CO. LTD, Zhang Jianguang ameahidi kutekeleza mradi huo kwa wakati na kwa ubora na kwamba tayari ameanza maandalizi yote muhimu.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la REA
Mtaa wa Medeli
P. O. Box 2153,
DODOMA, TANZANIA.

Share

Print
«August 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
28293031123
45
Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

The Rural Energy Agency (REA) is seeking proposals from qualified service providers for the supply, installation, and testing of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in eight remote villages across Geita, Ludewa and Mbulu districts. Those villages are located in remote areas with challenging geographical conditions, hence, impractical for grid extension.

Please find the attached documents:

•    Application Form for Supply and Installation of SA-SHS; and
•    Call for Proposals for Result Based Financing Installation of Stand Alone Solar Home Systems.

Read more
678910
111213
Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Wananchi Kijiji cha Usevya Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi wamepongeza hatua zinazochukuliwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kuhakikisha wanafikiwa na nishati safi ya kupikia kwa bei ya ruzuku.

Read more
1415
Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetoa wito kwa viongozi wa dini nchini kushiriki kikamilifu katika kampeni ya kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa lengo la kulinda afya na kuokoa mazingira.

Read more
1617
181920
Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Watanzania wameendelea kuhamasishwa kutumia nishati safi ya kupikia ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Read more
21222324
25262728293031
1234567

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top