Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Semina ya Fursa za Uwekezaji Katika Sekta ya Nishati Nchini
Aodax K. Nshala 7587

Semina ya Fursa za Uwekezaji Katika Sekta ya Nishati Nchini

Imeandaliwa na Ubalozi wa Norway Nchini Tanzania

Event date: 9/20/2016 Export event

Ubalozi wa Norway nchini umeandaa semina ya siku moja iliyofanyika katika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam tarehe 20 Septemba, 2016 kwa ajili kuelezea fursa za uwekezaji katika sekta ya nishati nchini. Semina hiyo ilihudhuriwa na washiriki kutoka makampuni 14 kutoka Norway na wadau wengine mbalimbali.

Akifungua semina hiyo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Dk. Juliana Pallangyo alisema ni fursa nzuri kwa washiriki kujifunza na kubadilishana uzoefu. Naibu Katibu Mkuu aliwahimiza wadau kutoka nchini Tanzania kushirikiana na wenzao wa Norway ambao wana uzoefu wa miaka mingi katika sekta ya nishati.

Akizungumza katika semina hiyo, Balozi wa Norway nchini, Hanne-Marie Kaarstad alisema kuwa ushirikiano wa Norway na Tanzania ni wa muda mrefu na umekuwa wa mafanikio ambapo shughuli mbalimbali za maendeleo zimetekelezwa kutokana na ushirikiano huo.

Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga aliwahimiza waendelezaji wa miradi ya nishati kuchangamkia fursa hiyo na kueleza kuwa zipo fursa mbalimbali za uwekezaji katika sekta ya nishati ambazo zikitumiwa vizuri zitawezesha upatikanaji wa nishati hiyo vijijini.


Imeandaliwa na:

Jaina D. Msuya
Afisa Habari na Elimu kwa Umma
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«October 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
301
REA Kushiriki Samia Kilimo Biashara Expo 2024 Morogoro

REA Kushiriki Samia Kilimo Biashara Expo 2024 Morogoro

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) itashiriki katika Maonesho ya Samia KILIMO Biashara Expo 2024 kwa msimu wa tatu yanayotarajiwa kuanza tarehe 6 Oktoba, 2024 wilaya ya Gairo Mkoani Morogoro. 

Read more
23456
78910
Bukombe Waunga Mkono Jitihada za Rais Samia Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia

Bukombe Waunga Mkono Jitihada za Rais Samia Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi kote Nchini wametakiwa kuendelea kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kutumia Nishati Safi ya Kupikia ili kuimarisha afya zao sambamba na kutunza mazingira.

Read more
111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top