Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia
Frank A. Mugogo 401

Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA), chini ya Wizara ya Nishati, una jukumu la kuhamasisha na kuwezesha upatikanaji wa nishati bora na salama kwa wananchi walioko maeneo ya vijijini upande wa Tanzania Bara.

Kwa kuzingatia maelekezo ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, pamoja na Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia, Wakala unaandaa mpango maalum wa kuwezesha taasisi zinazoandaa chakula na kulisha watu zaidi ya 100 kwa siku kuhamia katika matumizi ya nishati safi ya kupikia.

Kupitia mpango huu, REA inakusudia kuchangia gharama za uwekezaji wa mifumo ya kisasa ya kupikia kwa njia ya ruzuku.

Wito kwa Taasisi Zote:
Ili kuandaa mpango huo, REA inaomba taasisi zote nchini kuwasilisha taarifa zao kwa kujaza fomu iliyoambatishwa na tangazo hili ambazo zitajumuisha:-
1.    Jina na aina ya taasisi pamoja na eneo ilipo;
2.    Idadi ya watu wanaohudumiwa kwa siku;
3.    Aina ya nishati ya kupikia inayotumika kwa sasa; kiasi kinachotumika pamoja na gharama ya nishati hiyo kwa mwezi;
4.    Changamoto zinazokabili taasisi katika matumizi ya nishati hiyo;
5.    Mapendekezo ya mfumo au aina ya nishati safi ya kupikia inayohitajika; na
6.    Mtu wa mawasiliano.

Jinsi ya Kuwasilisha Maombi:
Taasisi zinaweza kuwasilisha maombi kwa anwani iliyowekwa chini kwa kutumia njia moja kati ya zifuatazo:
•    Kupitia barua pepe (clean.cooking@rea.go.tz);
•    Kwa nakala ngumu (hard copy) zinazopelekwa katika ofisi za REA makao makuu au ofisi za REA za mikoa; na
•    Kujaza fomu ya kielektroniki inayopatikana kwenye tovuti ya Wakala www.rea.go.tz  

Muda wa Kuwasilisha Taarifa:
Ili kuwezesha Wakala kuanza kutekeleza mpango huo mapema, Taasisi husika zinatakiwa kuwasilisha taarifa zao si zaidi ya tarehe 30 Novemba 2025.

Utekelezaji wa Mpango:
Katika kutekeleza mpango huu, REA inakusudia kuchangia gharama za uwekezaji wa mifumo ya kisasa ya kupikia kwa njia ya ruzuku. Kiwango cha ruzuku kitategemea, uwezo wa taasisi husika, upatikanaji wa fedha na vipaumbele vya serikali.

Aidha, REA itaanza na taasisi zilizopo vijijini, na itapanua huduma hizo kwa maeneo mengine kwa kadri ya upatikanaji wa fedha za mpango huu kwa kuzingatia mipaka ya utekelezaji wa majukumu yake.

Taasisi zitakazoleta taarifa mapema zitafikiriwa katika awamu za mwanzo za utekelezaji wa mpango huu.

Anuani ya kutuma maombi:

Mkurugenzi Mkuu,
Wakala wa Nishati Vijijini, 
Jengo la REA,
S.L.P 2153, Dodoma,
Barua pepe: clean.cooking@rea.go.tz 
Tovuti: www.rea.go.tz

Kwa maelelezo zaidi wasiliana na: 
1.    Omari Haji Bakari
Barua Pepe: omari.bakari@rea.go.tz 
Simu Namba: +255 687 013 990
2.    Francis Manyama
Barua Pepe:francis.manyama@rea.go.tz
Simu Namba: +255 756 931 292

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«September 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
31123456
789
Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

IRINGA, Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini kwa kuendesha mafunzo maalum ya wiki moja yaliyolenga kujenga uwezo wa waendelezaji wa miradi midogo ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower).

Mafunzo hayo yaliyoanza tarehe 7 Septemba, 2026 katika Hoteli ya Sunset mkoani Iringa, yamewakutanisha waendelezaji wa miradi (Developers) zaidi ya 15, hususan kutoka maeneo ya Nyanda za Juu Kusini. Lengo kuu ni kuwajengea uwezo wa kiufundi ili kuongeza ubora wa miradi yao ili iweze kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, tarehe 9 Septemba, 2026, Kaimu Meneja wa Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi kutoka REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya, alisema kuwa REA haishii tu kutoa msaada wa upatikanaji wa nishati vijijini, bali inajikita pia katika kuongeza ujuzi wa wataalamu wa ndani.

"Kuongeza ujuzi kwa waendelezaji hawa kutasaidia kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu na ubora unaohitajika. Hatua hii itaongeza idadi ya miradi inayofikia vigezo vya kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa, kuongeza uzalishaji wa umeme, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii vijijini," alisema Mhandisi Yesaya.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ushirikiano kati ya REA na Wataalamu kutoka Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia (CoET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Maeneo yaliyofundishwa ni pamoja na usanifu wa miradi, upembuzi yakinifu, sayansi ya maji (hydrology), uhandisi wa umeme na elektroniki, pamoja na uendeshaji na matengenezo ya mitambo.

Mbali na mafunzo, REA imebainisha kuwa imekuwa ikisaidia waendelezaji hao kupitia ruzuku za ujenzi, maandalizi ya maandiko ya miradi na usanifu.

Aidha, Wakala huo upo katika mchakato wa kuandaa mfumo wa mikataba ya muda mrefu (Framework Contract) na taasisi za elimu ili kutoa mafunzo endelevu kwenye nishati jadidifu ikiwemo nishati ya jua na mifumo ya gesi vunde.

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wamepongeza mafunzo hayo; akizungumza na Wanahabari, Mhandisi Denis Makoyi kutoka kampuni ya Africa Power Investment, alisema mafunzo hayo yameongeza uelewa mkubwa wa kiufundi katika hatua za utekelezaji wa miradi. Naye Lutengano Kigola kutoka mradi wa Nyalawa Hydropower, aliongeza kuwa mafunzo hayo yanathibitisha kuwa Tanzania ina wataalamu wa ndani wenye uwezo mkubwa wa kuendeleza miradi ya umeme wa maji.

  • MWISHO –

 

Read more
10111213
14151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top