Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini
Frank A. Mugogo 318

Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Wakazi wa vitongoji vya Chihanga, Mpilipili, Mkwedu na Majengo Wilayani Newala Mkoani Mtwara wameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vitongoji hivyo.

Wametoa pongezi hizo Oktoba 19, 2025 kwa nyakati tofauti wakati wa kampeni maalum ya kuhamasisha wananchi vitongojini kujiunga na huduma ya umeme inayoratibiwa na REA.

“Tunashukuru kufikishiwa umeme kitongojini hapa, maisha yetu kwa sasa yameboreshwa ukilinganisha na hali ilivyokuwa hapo kabla ya kufikishiwa huduma hii muhimu ya umeme,” alisema Litehu Rashid Mkazi wa Kitongoji cha Chihanga.

Kwa upande wake Bi. Skina Kunkatila Mkazi wa Kitongoji cha Mpilipili alifafanua namna ambavyo umeme umekuwa mkombozi katika maisha yake na alieleza adha mbalimbali zilizokuwepo kabla ya kufikishiwa nishati ya umeme na hali ilivyo sasa ambapo alisema kwa sasa kitongoji hakina tofauti na mji kwani huduma muhimu zote zinazohitaji umeme zinapatikana.

Naye Mwanahamisi Hassan maarufu kama Binti Nankomwanga Mkazi wa kitongoji cha Majengo alisema hapo zamani iliwalazimu kutembea umbali mrefu kusaga mahindi jambo ambalo kwa sasa halipo tena.

“Kitongoji chetu kimenoga, mwaka wa nyuma tulikuwa tunasafiri kwenda kusaga mahindi lakini sasa hivi kijiji kimechangamka, wananchi wanafanya biashara ya vinywaji baridi na suala la afya liko vizuri vifaa tiba vinavyotumia umeme vinafanya kazi,” alisema Binti Nankomwanga.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa vitongoji hivyo, Msimamizi wa miradi ya REA Mkoa wa Mtwara, Mhandisi Daniel Mwandupe alisema lengo la kampeni hiyo ya uhamasishaji ni kutoa elimu kwa wananchi ili kuelewa hatua za utekelezaji wa mradi unaoendelea wa kusambaza umeme, elimu ya kuomba kuunganishiwa umeme kwa kaya ambazo bado hazijafikiwa sambamba na kujadili changamoto zinazowakabili wananchi kwenye sekta ya umeme ili kupata ufumbuzi wa pamoja.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii Mwandamizi kutoka REA, Jaina Msuya alitoa wito kwa wananchi ambao hawajaunganishwa na huduma ya umeme kuchangamkia fursa ya kuunganishiwa kwa gharama ya shilingi 27,000 pekee.

Msuya aliwasisitiza kuhakikisha wanatunza na kulinda miundombinu ya umeme ili waendelee kunufaika na kupiga hatua zaidi kimaendeleo hasa ikizingatiwa kuwa Serikali imewekeza fedha nyingi kwenye miundombinu hiyo kwa lengo la kuwakwamua kimaendeleo wananchi wake.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«September 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
31123456
789
Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

IRINGA, Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini kwa kuendesha mafunzo maalum ya wiki moja yaliyolenga kujenga uwezo wa waendelezaji wa miradi midogo ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower).

Mafunzo hayo yaliyoanza tarehe 7 Septemba, 2026 katika Hoteli ya Sunset mkoani Iringa, yamewakutanisha waendelezaji wa miradi (Developers) zaidi ya 15, hususan kutoka maeneo ya Nyanda za Juu Kusini. Lengo kuu ni kuwajengea uwezo wa kiufundi ili kuongeza ubora wa miradi yao ili iweze kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, tarehe 9 Septemba, 2026, Kaimu Meneja wa Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi kutoka REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya, alisema kuwa REA haishii tu kutoa msaada wa upatikanaji wa nishati vijijini, bali inajikita pia katika kuongeza ujuzi wa wataalamu wa ndani.

"Kuongeza ujuzi kwa waendelezaji hawa kutasaidia kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu na ubora unaohitajika. Hatua hii itaongeza idadi ya miradi inayofikia vigezo vya kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa, kuongeza uzalishaji wa umeme, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii vijijini," alisema Mhandisi Yesaya.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ushirikiano kati ya REA na Wataalamu kutoka Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia (CoET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Maeneo yaliyofundishwa ni pamoja na usanifu wa miradi, upembuzi yakinifu, sayansi ya maji (hydrology), uhandisi wa umeme na elektroniki, pamoja na uendeshaji na matengenezo ya mitambo.

Mbali na mafunzo, REA imebainisha kuwa imekuwa ikisaidia waendelezaji hao kupitia ruzuku za ujenzi, maandalizi ya maandiko ya miradi na usanifu.

Aidha, Wakala huo upo katika mchakato wa kuandaa mfumo wa mikataba ya muda mrefu (Framework Contract) na taasisi za elimu ili kutoa mafunzo endelevu kwenye nishati jadidifu ikiwemo nishati ya jua na mifumo ya gesi vunde.

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wamepongeza mafunzo hayo; akizungumza na Wanahabari, Mhandisi Denis Makoyi kutoka kampuni ya Africa Power Investment, alisema mafunzo hayo yameongeza uelewa mkubwa wa kiufundi katika hatua za utekelezaji wa miradi. Naye Lutengano Kigola kutoka mradi wa Nyalawa Hydropower, aliongeza kuwa mafunzo hayo yanathibitisha kuwa Tanzania ina wataalamu wa ndani wenye uwezo mkubwa wa kuendeleza miradi ya umeme wa maji.

  • MWISHO –

 

Read more
10111213
14
REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuwezesha waendelezaji wadogo wa miradi ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kwa kutoa fedha, msaada wa kitaalamu na mafunzo, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa nishati nchini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top