Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini
Frank A. Mugogo 4

Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Wakazi wa vitongoji vya Chihanga, Mpilipili, Mkwedu na Majengo Wilayani Newala Mkoani Mtwara wameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vitongoji hivyo.

Wametoa pongezi hizo Oktoba 19, 2025 kwa nyakati tofauti wakati wa kampeni maalum ya kuhamasisha wananchi vitongojini kujiunga na huduma ya umeme inayoratibiwa na REA.

“Tunashukuru kufikishiwa umeme kitongojini hapa, maisha yetu kwa sasa yameboreshwa ukilinganisha na hali ilivyokuwa hapo kabla ya kufikishiwa huduma hii muhimu ya umeme,” alisema Litehu Rashid Mkazi wa Kitongoji cha Chihanga.

Kwa upande wake Bi. Skina Kunkatila Mkazi wa Kitongoji cha Mpilipili alifafanua namna ambavyo umeme umekuwa mkombozi katika maisha yake na alieleza adha mbalimbali zilizokuwepo kabla ya kufikishiwa nishati ya umeme na hali ilivyo sasa ambapo alisema kwa sasa kitongoji hakina tofauti na mji kwani huduma muhimu zote zinazohitaji umeme zinapatikana.

Naye Mwanahamisi Hassan maarufu kama Binti Nankomwanga Mkazi wa kitongoji cha Majengo alisema hapo zamani iliwalazimu kutembea umbali mrefu kusaga mahindi jambo ambalo kwa sasa halipo tena.

“Kitongoji chetu kimenoga, mwaka wa nyuma tulikuwa tunasafiri kwenda kusaga mahindi lakini sasa hivi kijiji kimechangamka, wananchi wanafanya biashara ya vinywaji baridi na suala la afya liko vizuri vifaa tiba vinavyotumia umeme vinafanya kazi,” alisema Binti Nankomwanga.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa vitongoji hivyo, Msimamizi wa miradi ya REA Mkoa wa Mtwara, Mhandisi Daniel Mwandupe alisema lengo la kampeni hiyo ya uhamasishaji ni kutoa elimu kwa wananchi ili kuelewa hatua za utekelezaji wa mradi unaoendelea wa kusambaza umeme, elimu ya kuomba kuunganishiwa umeme kwa kaya ambazo bado hazijafikiwa sambamba na kujadili changamoto zinazowakabili wananchi kwenye sekta ya umeme ili kupata ufumbuzi wa pamoja.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii Mwandamizi kutoka REA, Jaina Msuya alitoa wito kwa wananchi ambao hawajaunganishwa na huduma ya umeme kuchangamkia fursa ya kuunganishiwa kwa gharama ya shilingi 27,000 pekee.

Msuya aliwasisitiza kuhakikisha wanatunza na kulinda miundombinu ya umeme ili waendelee kunufaika na kupiga hatua zaidi kimaendeleo hasa ikizingatiwa kuwa Serikali imewekeza fedha nyingi kwenye miundombinu hiyo kwa lengo la kuwakwamua kimaendeleo wananchi wake.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«October 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
293012345
REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

Timu ya wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na timu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) tarehe 03 Oktoba, 2025 wameanza zoezi la uhamasishaji kwa Wananchi ili wajiunge na huduma ya umeme kwenye vitongoji mbalimbali vya mkoa wa Simiyu.

Read more
6789101112
13141516171819
Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefikisha umeme katika vitongoji 2,354 kati ya vitongoji 3,421 Mkoani Mtwara huku ukiendelea kutekeleza miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji vilivyosalia mkoani humo.

Read more
20
Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Wakazi wa vitongoji vya Chihanga, Mpilipili, Mkwedu na Majengo Wilayani Newala Mkoani Mtwara wameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vitongoji hivyo.

Read more
212223242526
272829303112
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top