Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini
Frank A. Mugogo 131

Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Wakazi wa vitongoji vya Chihanga, Mpilipili, Mkwedu na Majengo Wilayani Newala Mkoani Mtwara wameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vitongoji hivyo.

Wametoa pongezi hizo Oktoba 19, 2025 kwa nyakati tofauti wakati wa kampeni maalum ya kuhamasisha wananchi vitongojini kujiunga na huduma ya umeme inayoratibiwa na REA.

“Tunashukuru kufikishiwa umeme kitongojini hapa, maisha yetu kwa sasa yameboreshwa ukilinganisha na hali ilivyokuwa hapo kabla ya kufikishiwa huduma hii muhimu ya umeme,” alisema Litehu Rashid Mkazi wa Kitongoji cha Chihanga.

Kwa upande wake Bi. Skina Kunkatila Mkazi wa Kitongoji cha Mpilipili alifafanua namna ambavyo umeme umekuwa mkombozi katika maisha yake na alieleza adha mbalimbali zilizokuwepo kabla ya kufikishiwa nishati ya umeme na hali ilivyo sasa ambapo alisema kwa sasa kitongoji hakina tofauti na mji kwani huduma muhimu zote zinazohitaji umeme zinapatikana.

Naye Mwanahamisi Hassan maarufu kama Binti Nankomwanga Mkazi wa kitongoji cha Majengo alisema hapo zamani iliwalazimu kutembea umbali mrefu kusaga mahindi jambo ambalo kwa sasa halipo tena.

“Kitongoji chetu kimenoga, mwaka wa nyuma tulikuwa tunasafiri kwenda kusaga mahindi lakini sasa hivi kijiji kimechangamka, wananchi wanafanya biashara ya vinywaji baridi na suala la afya liko vizuri vifaa tiba vinavyotumia umeme vinafanya kazi,” alisema Binti Nankomwanga.

Akizungumza kwa nyakati tofauti na wananchi wa vitongoji hivyo, Msimamizi wa miradi ya REA Mkoa wa Mtwara, Mhandisi Daniel Mwandupe alisema lengo la kampeni hiyo ya uhamasishaji ni kutoa elimu kwa wananchi ili kuelewa hatua za utekelezaji wa mradi unaoendelea wa kusambaza umeme, elimu ya kuomba kuunganishiwa umeme kwa kaya ambazo bado hazijafikiwa sambamba na kujadili changamoto zinazowakabili wananchi kwenye sekta ya umeme ili kupata ufumbuzi wa pamoja.

Naye Afisa Maendeleo ya Jamii Mwandamizi kutoka REA, Jaina Msuya alitoa wito kwa wananchi ambao hawajaunganishwa na huduma ya umeme kuchangamkia fursa ya kuunganishiwa kwa gharama ya shilingi 27,000 pekee.

Msuya aliwasisitiza kuhakikisha wanatunza na kulinda miundombinu ya umeme ili waendelee kunufaika na kupiga hatua zaidi kimaendeleo hasa ikizingatiwa kuwa Serikali imewekeza fedha nyingi kwenye miundombinu hiyo kwa lengo la kuwakwamua kimaendeleo wananchi wake.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«December 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526
Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya  Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Rais Samia Atoa Ruzuku ya Kufanya Wiring Miradi ya Umeme Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaanza kutekeleza mradi wa kutandaza nyaya za umeme (wiring) kwa wananchi kupitia miradi ya kusambaza umeme inayotekelezwa na wakala kote nchini.

Read more
27282930
123
Hafla ya Utiaji Saini Mikataba ya Nishati Safi

Hafla ya Utiaji Saini Mikataba ya Nishati Safi

Karibu katika Hafla ya Kusaini Mikataba ya Kufunga Miundombinu ya Nishati Safi katika Shule za Sekondari 52 pamoja na Chuo cha VETA.

Read more
45
Shule za Sekondari 52; Chuo cha VETA Kufungiwa Miundombinu ya Nishati Safi

Shule za Sekondari 52; Chuo cha VETA Kufungiwa Miundombinu ya Nishati Safi

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imesaini mikataba ya kufunga miundombinu ya nishati safi ya kupikia kwa shule za Sekondari 52 na Chuo cha VETA kimoja hapa nchini.

Read more
67
891011121314
1516
Mkurugenzi Mkuu REA Awafunda Watumishi

Mkurugenzi Mkuu REA Awafunda Watumishi

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amewataka watumishi kufanya kazi kwa bidii, uadilifu na maarifa ili kuleta tija katika kuwatumikia wananchi.

Read more
1718192021
22232425262728
2930311234

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top