Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Admin.Frank Mugogo 11751

UFAFANUZI WA REA KUHUSU TAARIFA ZILIZOTOLEWA KWENYE MAGAZETI YA JAMBO LEO NA MWANAHALISI YA IJUMAA TAREHE 15 APRILI 2016, NA HABARI LEO LA JUMAMOSI TAREHE 16 APRILI 2016

Wakala wa Nishati Vijijini unatoa ufafanuzi kuhusiana na taarifa zilizoandikwa kwenye magazeti ya Jambo Leo na Mwanahalisi ya Ijumaa Tarehe 15 Aprili 2016 pamoja na Gazeti la Habari Leo la Jumamosi Tarehe 16 Aprili 2016.

Tunapenda kuwafahamisha wananchi kuwa Wakala wa Nishati Vijijini haujawahi kuingia mkataba wa kuagiza mashine-umba (Transformers) 200 kutoka TANELEC. Mashine-umba pamoja na vifaa vingine vyote vinavyotumika katika ujenzi wa miundombinu chini ya “Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini wa Awamu ya Pili” vinanunuliwa moja kwa moja na wakandarasi wanaotekeleza miradi hiyo baada ya kupewa zabuni na REA. Kwa kuwa miradi ya usambazaji umeme vijijini ina msamaha wa kodi ambao umetolewa kwa REA; kwa utaratibu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), vifaa vinaponunuliwa na mkandarasi ni lazima vioneshwe kuwa ni kwa ajili ya mradi wa REA ili viweze kupata msamaha huo wa kodi uliotolewa kwa miradi inayosimamiwa na REA.

Aidha, REA haijapeleka Mashine-umba za mradi huo unaotajwa kwa TANELEC kwa ajili ya matengenezo kama ilivyoripotiwa kwani wajibu wa kurekebisha hitilafu zozote kwenye vifaa na miundombinu inayojengwa na ambayo bado haijakabidhiwa kwa TANESCO ni la Mkandarasi. Hata baada ya kukabidhi mradi kwa TANESCO, Mkandarasi husika bado anawajibika kurekebisha kuharibika kwa vifaa na miundo-mbinu ya umeme aliyoijenga kwa muda wa mwaka mmoja baada ya kukabidhi mradi kwa TANESCO kwa mujibu wa mkataba.

Aidha, kampuni ya umeme nchini TANESCO, ambayo ndiyo msimamizi mkuu wa miradi iliyopo chini ya “Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini wa Awamu ya Pili”, inao wajibu wa kusimamia ubora wa vifaa na ujenzi wa miundombinu hiyo ya usambazaji umeme na kuhakikisha kuwa inajengwa kwa viwango vinavyolingana na vile vilivyofafanuliwa kwenye zabuni na mikataba. Hivyo basi; malipo yote yanayofanywa na REA kwenda kwa Wakandarasi wa miradi hiyo yanaidhinishwa na kulipwa pale tu REA inapopokea uthibitisho kutoka TANESCO kuwa kazi imefanyika kulingana na viwango vya ubora vinavyohitajika kulingana na mikataba.

Kuhusiana na masuala ya rushwa kwenye miradi; REA kupitia vyombo vya habari na kampeni za uelimishaji muda wote imesisitiza wananchi kukataa kutoa rushwa kwa ajili ya kuunganishiwa umeme na kuripoti kwenye vyombo vya dola pale wanapoombwa rushwa ili hatua stahiki ziweze kuchukuliwa. REA kupitia vyombo vya habari imekuwa ikitoa maonyo kwa wakandarasi wakubwa na wadogo, wafanyakazi pamoja na vibarua wao kutojihusisha kabisa na masuala ya rushwa.

Imetolewa na:
MKURUGENZI MKUU
WAKALA WA NISHATI VIJIJINI (REA)
20 SAM NUJOMA, 14414
P. O. BOX 7990
DAR-ES-SALAAM.

Rate article

No rating
Rate this article:
No rating

Share

Print
«May 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
293012345
6789101112
13141516171819
20212223242526
272829303112
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top