Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
UJERUMANI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI YA TANZANIA KATIKA UZALISHAJI WA UMEME VIJIJINI
Host 12481

UJERUMANI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI YA TANZANIA KATIKA UZALISHAJI WA UMEME VIJIJINI

Serikali imesema ipo tayari kushirikiana na Ujerumani katika kuzalisha umeme vijijini kwa kutumia nishati mbadala hususan upepo na jua. Hayo yalisemwa na Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Prof. Sospeter Muhongo alipokutana na Ujumbe wa Wabunge kutoka Ujerumani.

Ujumbe wa Wabunge hao uliongozwa na Mhe. Josef Goeppel ambaye aliongozana na Mhe. Dorothea Steiner, Mhe. Marco Brulow, Mhe. Sabine Stuber pamoja na balozi wa Ujerumani nchini Mhe. Klaus-Peter Brandes.

Wabunge hao walimtembelea Waziri Prof. Muhongo ofisini kwake kwa lengo la kujadili naye namna Ujerumani inavyoweza kushirikiana na Tanzania katika kuwezesha wananchi wengi kupata huduma za umeme hususan kwa waishio maeneo ya vijijini kwa kutumia vyanzo vya nishati mbadala.

Mhe. Prof. Muhongo alieleza Ujumbe huo kuwa Tanzania ipo tayari kushirikiana na Serikali ya Ujerumani katika sekta ya nishati hususan nishati mbadala, katika jitihada zake za kuwapatia wananchi nishati hiyo. “Sisi tupo tayari kushirikiana nanyi katika suala hili la uzalishaji umeme, kwani lengo letu ni kuwa na umeme wa kutosha na wa uhakika” alisisitiza Prof. Muhongo.

Naye Mhe. Joseph Goeppel ambaye pia ni Kiongozi wa Ujumbe wa Wabunge hao alisema amefurahishwa na namna Tanzania ilivyojipanga katika kuwawezesha wananchi wengi kupata huduma ya umeme ambayo ni kichocheo cha maendeleo.

Aliahidi kupeleka ujumbe huo katika bunge la Ujerumani ili kuanza rasmi ushirikiano baina ya serikali hiyo na serikali ya Tanzania katika uzalishaji umeme kwa kutumia nishati mbadala.

Mhe. Goeppel alimuomba Waziri Muhongo kuwa ushirikiano huo uanze mapema mwezi Januari baada ya kukamilisha taratibu zote za kiofisi zinazohusu ushirikiano wa kimataifa. Prof. Muhongo alikubali ushauri huo na kusema Serikali ya Tanzania ipo tayari kuanza ushirikiano huo mapema iwezekanavyo.


Imeandaliwa na:

Mohamed Saif
Afisa Habari
Wizara ya Nisahati na Madini
mohamed.saif@mem.go.tz
 

Share

Print
«August 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
272829303112
3456789
1011121314
REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefanikiwa kusambaza takribani mitungi laki saba ya gesi ya kupikia (LPG) nchini kote, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa kasi wa Mkakati wa Kitaifa wa Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
1516
1718

Maombi ya Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unakaribisha waombaji wenye vigezo kuomba mkopo wa kuwezesha ujenzi wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) ili kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini.

Pamoja na tangazo hili, tumeweka viambatanisho vifuatavyo:
•    Tangazo la fursa ya mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta ya Petroli na Dizeli vijijini.
•    Mwongozo wa utoaji mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta vijijini.
•    Fomu ya Maombi ya Mkopo.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la REA
Mtaa wa Medeli
P. O. Box 2153,
DODOMA, TANZANIA.

Read more
1920212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top