Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
UJERUMANI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI YA TANZANIA KATIKA UZALISHAJI WA UMEME VIJIJINI
Host 11979

UJERUMANI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI YA TANZANIA KATIKA UZALISHAJI WA UMEME VIJIJINI

Serikali imesema ipo tayari kushirikiana na Ujerumani katika kuzalisha umeme vijijini kwa kutumia nishati mbadala hususan upepo na jua. Hayo yalisemwa na Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Prof. Sospeter Muhongo alipokutana na Ujumbe wa Wabunge kutoka Ujerumani.

Ujumbe wa Wabunge hao uliongozwa na Mhe. Josef Goeppel ambaye aliongozana na Mhe. Dorothea Steiner, Mhe. Marco Brulow, Mhe. Sabine Stuber pamoja na balozi wa Ujerumani nchini Mhe. Klaus-Peter Brandes.

Wabunge hao walimtembelea Waziri Prof. Muhongo ofisini kwake kwa lengo la kujadili naye namna Ujerumani inavyoweza kushirikiana na Tanzania katika kuwezesha wananchi wengi kupata huduma za umeme hususan kwa waishio maeneo ya vijijini kwa kutumia vyanzo vya nishati mbadala.

Mhe. Prof. Muhongo alieleza Ujumbe huo kuwa Tanzania ipo tayari kushirikiana na Serikali ya Ujerumani katika sekta ya nishati hususan nishati mbadala, katika jitihada zake za kuwapatia wananchi nishati hiyo. “Sisi tupo tayari kushirikiana nanyi katika suala hili la uzalishaji umeme, kwani lengo letu ni kuwa na umeme wa kutosha na wa uhakika” alisisitiza Prof. Muhongo.

Naye Mhe. Joseph Goeppel ambaye pia ni Kiongozi wa Ujumbe wa Wabunge hao alisema amefurahishwa na namna Tanzania ilivyojipanga katika kuwawezesha wananchi wengi kupata huduma ya umeme ambayo ni kichocheo cha maendeleo.

Aliahidi kupeleka ujumbe huo katika bunge la Ujerumani ili kuanza rasmi ushirikiano baina ya serikali hiyo na serikali ya Tanzania katika uzalishaji umeme kwa kutumia nishati mbadala.

Mhe. Goeppel alimuomba Waziri Muhongo kuwa ushirikiano huo uanze mapema mwezi Januari baada ya kukamilisha taratibu zote za kiofisi zinazohusu ushirikiano wa kimataifa. Prof. Muhongo alikubali ushauri huo na kusema Serikali ya Tanzania ipo tayari kuanza ushirikiano huo mapema iwezekanavyo.


Imeandaliwa na:

Mohamed Saif
Afisa Habari
Wizara ya Nisahati na Madini
mohamed.saif@mem.go.tz
 

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
17181920212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top