Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
UJERUMANI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI YA TANZANIA KATIKA UZALISHAJI WA UMEME VIJIJINI
Host 11938

UJERUMANI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI YA TANZANIA KATIKA UZALISHAJI WA UMEME VIJIJINI

Serikali imesema ipo tayari kushirikiana na Ujerumani katika kuzalisha umeme vijijini kwa kutumia nishati mbadala hususan upepo na jua. Hayo yalisemwa na Waziri wa Nishati na Madini, Mhe.Prof. Sospeter Muhongo alipokutana na Ujumbe wa Wabunge kutoka Ujerumani.

Ujumbe wa Wabunge hao uliongozwa na Mhe. Josef Goeppel ambaye aliongozana na Mhe. Dorothea Steiner, Mhe. Marco Brulow, Mhe. Sabine Stuber pamoja na balozi wa Ujerumani nchini Mhe. Klaus-Peter Brandes.

Wabunge hao walimtembelea Waziri Prof. Muhongo ofisini kwake kwa lengo la kujadili naye namna Ujerumani inavyoweza kushirikiana na Tanzania katika kuwezesha wananchi wengi kupata huduma za umeme hususan kwa waishio maeneo ya vijijini kwa kutumia vyanzo vya nishati mbadala.

Mhe. Prof. Muhongo alieleza Ujumbe huo kuwa Tanzania ipo tayari kushirikiana na Serikali ya Ujerumani katika sekta ya nishati hususan nishati mbadala, katika jitihada zake za kuwapatia wananchi nishati hiyo. “Sisi tupo tayari kushirikiana nanyi katika suala hili la uzalishaji umeme, kwani lengo letu ni kuwa na umeme wa kutosha na wa uhakika” alisisitiza Prof. Muhongo.

Naye Mhe. Joseph Goeppel ambaye pia ni Kiongozi wa Ujumbe wa Wabunge hao alisema amefurahishwa na namna Tanzania ilivyojipanga katika kuwawezesha wananchi wengi kupata huduma ya umeme ambayo ni kichocheo cha maendeleo.

Aliahidi kupeleka ujumbe huo katika bunge la Ujerumani ili kuanza rasmi ushirikiano baina ya serikali hiyo na serikali ya Tanzania katika uzalishaji umeme kwa kutumia nishati mbadala.

Mhe. Goeppel alimuomba Waziri Muhongo kuwa ushirikiano huo uanze mapema mwezi Januari baada ya kukamilisha taratibu zote za kiofisi zinazohusu ushirikiano wa kimataifa. Prof. Muhongo alikubali ushauri huo na kusema Serikali ya Tanzania ipo tayari kuanza ushirikiano huo mapema iwezekanavyo.


Imeandaliwa na:

Mohamed Saif
Afisa Habari
Wizara ya Nisahati na Madini
mohamed.saif@mem.go.tz
 

Rate article

No rating
Rate this article:
No rating

Share

Print
«July 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
24252627282930
1234
National Clean Cooking Strategy (2024 – 2034)

National Clean Cooking Strategy (2024 – 2034)

The Government of the United Republic of Tanzania, in collaboration with various stakeholders has prepared the National Clean Cooking Strategy. The strategy aims to ensure that 80 percent of Tanzanians use clean cooking solutions by the year 2034.

Read more
567
891011121314
15161718192021
Vijiji 151 Vimebaki Nchi Nzima Kupata Huduma ya Umeme – Kapinga

Vijiji 151 Vimebaki Nchi Nzima Kupata Huduma ya Umeme – Kapinga

Ni vijiji 151 tu nchi nzima ndio ambavyo bado havijafikiwa na huduma ya umeme kati ya Vijiji zaidi ya 12,000 ambapo wilayani Ludewa mkoani Njombe vimebaki Vijiji nane.

Read more
22232425262728
2930311234

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top