Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Uzinduzi wa Mpango wa Kuendeleza Usambazaji Umeme Vijijini
Aodax K. Nshala 9115

Uzinduzi wa Mpango wa Kuendeleza Usambazaji Umeme Vijijini

Ulifanyika Katika Kijiji cha Kwedizinga, Wilaya ya Handeni, Mkoa wa Tanga

Event date: 8/15/2016 Export event

Serikali imezindua Mpango wa Kuendeleza Usambazaji Umeme Vijijini (Tanzania Rural Electrification Expansion Program - TREEP) ambao umefadhiliwa na Benki ya Dunia kwa gharama ya dola za Marekani Milioni 200.

Lengo kuu la Mradi wa TREEP ni kuongeza upatikanaji wa umeme vijijini kwa kuongeza miundombinu ya usambazaji wa umeme pamoja na miundombinu ya uzalishaji hasa wa nishati jadidifu vijijini.

TREEP ni kati ya Programu za kwanza kabisa kutumia mpango mpya wa Benki ya Dunia ujulikanao kama Program-for-Results (PforR), mpango unaojikita kwenye utekelezaji na matokeo. Miradi ya nishati vijijini inayotekelezwa katika mpango wa PforR pia imepata ufadhiri kutoka Serikali za Norway (Norad), Sweden (Sida), Uingereza (DFID) pamoja na Umoja wa Ulaya. Miradi ya wafadhili hawa wote inaratibiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Akizindua mradi huo, Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Prof. Sospeter M. Muhongo (Mb) Katika Kijiji cha Kwedizinga, Wilaya ya Handeni – Mkoa wa Tanga aliwahimiza wananchi wa vijijini kutumia umeme kwa ajili ya shughuli za uzalishaji mali ili wajikwamue kutoka katika umaskini.

Awali akitoa maelezo ya mradi huo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga alisema kaya zisizopungua 500,000 zitaunganishwa na umeme wakati wa utekelezaji wa mradi huo. Aidha aliongeza kuwa takribani kilomita 24,000 zitafikiwa na miundombinu ya usafirishaji na usambazaji umeme na inakisiwa kuwa watu 310,000 watafikiwa na huduma ya umeme (access level) kupitia mifumo ya nje ya gridi (off-grid) na gridi ndogo (mini-grids).


Imeandaliwa na:

Jaina D. Msuya
Afisa Habari na Elimu kwa Umma
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«April 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
311234
CALL FOR PROPOSAL - Supply and Installation of Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions

CALL FOR PROPOSAL - Supply and Installation of Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions

The Rural Energy Agency issue the Second Call for applications from qualified suppliers to Supply and install Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions through on-call basis.

Read more
56
789
Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24

Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24

Please find the attached Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24:

Read more
10111213
14
Wabia wa Maendeleo Waahidi Kuendelea Kushirikiana na Serikali ya Tanzania Kuboresha Maisha ya Wananchi

Wabia wa Maendeleo Waahidi Kuendelea Kushirikiana na Serikali ya Tanzania Kuboresha Maisha ya Wananchi

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego amuopengeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kazi kubwa ya kufikisha umeme vijijini hali iliyobadili maisha ya wananchi vijijini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top