Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Uzinduzi wa Mpango wa Kuendeleza Usambazaji Umeme Vijijini
Aodax K. Nshala 9113

Uzinduzi wa Mpango wa Kuendeleza Usambazaji Umeme Vijijini

Ulifanyika Katika Kijiji cha Kwedizinga, Wilaya ya Handeni, Mkoa wa Tanga

Event date: 8/15/2016 Export event

Serikali imezindua Mpango wa Kuendeleza Usambazaji Umeme Vijijini (Tanzania Rural Electrification Expansion Program - TREEP) ambao umefadhiliwa na Benki ya Dunia kwa gharama ya dola za Marekani Milioni 200.

Lengo kuu la Mradi wa TREEP ni kuongeza upatikanaji wa umeme vijijini kwa kuongeza miundombinu ya usambazaji wa umeme pamoja na miundombinu ya uzalishaji hasa wa nishati jadidifu vijijini.

TREEP ni kati ya Programu za kwanza kabisa kutumia mpango mpya wa Benki ya Dunia ujulikanao kama Program-for-Results (PforR), mpango unaojikita kwenye utekelezaji na matokeo. Miradi ya nishati vijijini inayotekelezwa katika mpango wa PforR pia imepata ufadhiri kutoka Serikali za Norway (Norad), Sweden (Sida), Uingereza (DFID) pamoja na Umoja wa Ulaya. Miradi ya wafadhili hawa wote inaratibiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Akizindua mradi huo, Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Prof. Sospeter M. Muhongo (Mb) Katika Kijiji cha Kwedizinga, Wilaya ya Handeni – Mkoa wa Tanga aliwahimiza wananchi wa vijijini kutumia umeme kwa ajili ya shughuli za uzalishaji mali ili wajikwamue kutoka katika umaskini.

Awali akitoa maelezo ya mradi huo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga alisema kaya zisizopungua 500,000 zitaunganishwa na umeme wakati wa utekelezaji wa mradi huo. Aidha aliongeza kuwa takribani kilomita 24,000 zitafikiwa na miundombinu ya usafirishaji na usambazaji umeme na inakisiwa kuwa watu 310,000 watafikiwa na huduma ya umeme (access level) kupitia mifumo ya nje ya gridi (off-grid) na gridi ndogo (mini-grids).


Imeandaliwa na:

Jaina D. Msuya
Afisa Habari na Elimu kwa Umma
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top