Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Uzinduzi wa Mpango wa Kuendeleza Usambazaji Umeme Vijijini
Aodax K. Nshala 9125

Uzinduzi wa Mpango wa Kuendeleza Usambazaji Umeme Vijijini

Ulifanyika Katika Kijiji cha Kwedizinga, Wilaya ya Handeni, Mkoa wa Tanga

Event date: 8/15/2016 Export event

Serikali imezindua Mpango wa Kuendeleza Usambazaji Umeme Vijijini (Tanzania Rural Electrification Expansion Program - TREEP) ambao umefadhiliwa na Benki ya Dunia kwa gharama ya dola za Marekani Milioni 200.

Lengo kuu la Mradi wa TREEP ni kuongeza upatikanaji wa umeme vijijini kwa kuongeza miundombinu ya usambazaji wa umeme pamoja na miundombinu ya uzalishaji hasa wa nishati jadidifu vijijini.

TREEP ni kati ya Programu za kwanza kabisa kutumia mpango mpya wa Benki ya Dunia ujulikanao kama Program-for-Results (PforR), mpango unaojikita kwenye utekelezaji na matokeo. Miradi ya nishati vijijini inayotekelezwa katika mpango wa PforR pia imepata ufadhiri kutoka Serikali za Norway (Norad), Sweden (Sida), Uingereza (DFID) pamoja na Umoja wa Ulaya. Miradi ya wafadhili hawa wote inaratibiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Akizindua mradi huo, Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Prof. Sospeter M. Muhongo (Mb) Katika Kijiji cha Kwedizinga, Wilaya ya Handeni – Mkoa wa Tanga aliwahimiza wananchi wa vijijini kutumia umeme kwa ajili ya shughuli za uzalishaji mali ili wajikwamue kutoka katika umaskini.

Awali akitoa maelezo ya mradi huo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga alisema kaya zisizopungua 500,000 zitaunganishwa na umeme wakati wa utekelezaji wa mradi huo. Aidha aliongeza kuwa takribani kilomita 24,000 zitafikiwa na miundombinu ya usafirishaji na usambazaji umeme na inakisiwa kuwa watu 310,000 watafikiwa na huduma ya umeme (access level) kupitia mifumo ya nje ya gridi (off-grid) na gridi ndogo (mini-grids).


Imeandaliwa na:

Jaina D. Msuya
Afisa Habari na Elimu kwa Umma
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«May 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
2829301234
567891011
12131415
Zaidi ya Bilioni 17 Kusambaza Umeme Vitongojini Singida

Zaidi ya Bilioni 17 Kusambaza Umeme Vitongojini Singida

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa Shilingi Bilioni 17.39 wa kusambaza umeme katika vitongoji 120 utakaonufaisha Kaya 3,960 Mkoani Singida.

Read more
16
Mkurugenzi Mkuu REA Aisisitiza Bodi Mpya ya Zabuni Kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu

Mkurugenzi Mkuu REA Aisisitiza Bodi Mpya ya Zabuni Kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy ameielekeza Bodi mpya ya Zabuni (Tender Board) ya Wakala kuhakikisha inatekeleza majukumu yake kwa kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu ili kuleta tija katika kazi zake.

Read more
1718
19
Benki ya Dunia Yaridhishwa na Utekelezwaji wa Miradi ya REA

Benki ya Dunia Yaridhishwa na Utekelezwaji wa Miradi ya REA

Benki ya Dunia (WB) yaihakikishia ushirikiano Serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika utekelezaji wa miradi ya Nishati kote nchini kwa ulinzi wa mazingira na ustawi wa Taifa kwa ujumla.

Read more
202122232425
2627282930311
2345678

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top