Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030
Frank A. Mugogo 775

Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Imeelezwa kuwa hadi kufikia mwaka 2030 vitongoji vyote Tanzania Bara vitakuwa vimefikishiwa nishati ya umeme kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa na kusimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Umeme Vijijini kutoka REA, Mhandisi Jones Olotu Julai 05, 2025 katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) Jijini Dar es Salaam ndani ya Banda la Maonesho la Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

"Tayari tumefikisha umeme katika vijiji vyote 12,318 Tanzania Bara sawa na asilimia 100 na sasa hivi ni zamu ya vitongoji, leo hii ninavyozungumza vitongoji 33,657 kati ya vitongoji 64,359 kote nchini vimefikishiwa umeme ambayo ni sawa na asilimia 52.3," alisema Mhandisi Olotu.

Mhandisi Olotu aliweka bayana namna ambavyo Serikali imejizatiti katika kuhakikisha umeme unafika katika kila kona ya nchi kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa kwa usimamizi wa REA ili kuwaletea maendeleo wananchi wake.

Alisema kuwa vitongoji 30,702 havijafikiwa na umeme, hata hivyo alibainisha hatua mbalimbali zilizochukuliwa na zinazoendelea kupitia miradi inayotekelezwa ya kuhakikisha umeme unafika katika vitongoji hivyo.

"Katika vitongoji ambavyo havijafikiwa; vitongoji 7,736 vipo katika miradi inayoendelea kutekelezwa na vitongoji 22,966 kati ya hivi  tumetangaza zabuni kubwa ya kufikisha umeme kwenye vitongoji 9,009 hivyo tutabakiwa na vitongoji 13,957 ambavyo tunatarajia ndani ya miaka mitano navyo vitakuwa vimefikiwa kulingana na upatikanaji wa fedha," alibainisha Mha. Olotu.

Mhandisi Olotu alitoa wito kwa wananchi katika maeneo yaliyofikiwa na umeme kutumia umeme kuboresha hali ya maisha yao kwa kubuni miradi inayotumia umeme ili kujiongezea vipato vyao badala ya kutumia umeme kwa ajili tu ya mwanga wakati wa usiku.

Amewasihi kuiga mfano wa baadhi ya wananchi ambao wamevumbua fursa katika maeneo yao baada ya kufikishiwa umeme jambo ambalo limeanza kuleta manufaa katika maisha yao ya kila siku.

"Baadhi ya wanufaika tumeshuhudia namna ambavyo wamechangamkia uwepo wa umeme kwenye maeneo yao, tumekuta wanatumia umeme kwa shughuli mbalimbali za kiuchumi ikiwemo saluni, wamefungua kumbi za kuonyesha sinema na mpira, karakana za kuchomelea na wengine wamefungua biashara ya kuuza vinywaji baridi," alisema.

Alisema kuwa katika maeneo mengi ya vijiji miji hali ya maisha imebadilika baada ya kufikishiwa umeme kwani fursa za ajira zimeongezeka kutokana na kuibuliwa kwa viwanda vidogo vidogo vingi vya kuchakata mazao.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«October 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
293012345
REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

REA Yaanza Uhamasishaji Kwa Wananchi Kujiunga na Huduma ya Umeme Kwenye Vitongoji Mkoani Simiyu

Timu ya wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na timu ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) tarehe 03 Oktoba, 2025 wameanza zoezi la uhamasishaji kwa Wananchi ili wajiunge na huduma ya umeme kwenye vitongoji mbalimbali vya mkoa wa Simiyu.

Read more
6789101112
13141516171819
Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Zaidi ya Vitongoji 2,350 Mkoani Mtwara Vyafikishiwa Umeme

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefikisha umeme katika vitongoji 2,354 kati ya vitongoji 3,421 Mkoani Mtwara huku ukiendelea kutekeleza miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji vilivyosalia mkoani humo.

Read more
20
Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Newala Waipa Kongole REA Mradi wa Kusambaza Umeme Vitongojini

Wakazi wa vitongoji vya Chihanga, Mpilipili, Mkwedu na Majengo Wilayani Newala Mkoani Mtwara wameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kufikisha umeme katika vitongoji hivyo.

Read more
2122
Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Tangazo Kwa Taasisi Zinazohudumia Watu Zaidi ya 100 Kuhusu Uhamasishaji wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA), chini ya Wizara ya Nishati, una jukumu la kuhamasisha na kuwezesha upatikanaji wa nishati bora na salama kwa wananchi walioko maeneo ya vijijini upande wa Tanzania Bara.

Read more
23242526
272829303112
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top