Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama
Frank A. Mugogo 808

Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewasihi Watanzania kote nchini kuachana na dhana ya kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni gharama ikilinganishwa na matumizi ya kuni na mkaa.

Mkurugenzi wa Umeme Vijijini kutoka REA, Mhandisi Jones Olotu ametoa rai hiyo Julai 04, 2025 katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) Jijini Dar es Salaam ndani ya Banda la Maonesho la Wakala wa Nishati Vijijini (REA).
"Kumekuwepo na dhana kwamba kutumia nishati safi ya kupikia ikiwemo umeme ni gharama ikilinganishwa na kutumia kuni, dhana hii ni potofu haina ukweli kwani sasa hivi teknolojia imeboreshwa," alisisitiza Mhandisi Olotu.

Alisema kuwa kwa sasa teknolojia imeboreshwa ikilinganishwa na hapo zamani na alisisitiza kuwa hivi sasa yapo majiko ya umeme ambayo yanatumia umeme kidogo.
Alitoa wito kwa wananchi kutembelea Banda la REA ili kushuhudia teknolojia hizo zilizoboreshwa na kujionea kwa vitendo namna ambavyo majiko hayo yanafanya kazi.
"Wananchi watembelee banda la REA kujionea namna ambavyo chakula kinapikwa kwa kutumia nishati Safi ya Kupikia, ladha haibadiliki na pia muda wa kupika ni mchache ikilinganishwa na chakula kinachopikwa kwa kuni ama mkaa," alisema.

Akizungumzia kuhusiana na uhamasishaji na uwezeshwaji kwa waendelezaji wa teknojia za Nishati safi ya Kupikia, Mhandisi Olotu alisema lengo ni kuwawezesha Watanzania kutumia nishati safi kuepuka madhara ya afya ikiwemo changamoto kwenye mifumo ya upumuaji sambamba na kulinda mazingira.

Alifafanua kuwa kwa mujibu wa takwimu za Wizara ya Afya; kwa mwaka mmoja takriban watu 33,000 hupoteza maisha kutokana na matumizi ya nishati isiyo salama na kwamba REA ni miongoni mwa washika dau wa kuhakikisha idadi ya vifo vinavyosababishwa na athari ya moshi ya kuni na mkaa inapungua.

"Tunataka kuachana kabisa na matumizi ya kuni na mkaa lakini jambo hili linafanyika kwa utaratibu kwani ni ngumu kumbadilisha kila mtu mara moja; inachukua muda na ni hatua kwa baadhi ya maeneo na ndio maana kuna majiko tunasambaza yanayotumia kuni ama mkaa kwa kiwango kidogo," alisema.

Alisema kwa kuanzia REA ilianza na mpango wa kugawa majiko ya gesi ya kilo sita ambapo mitungi 3,255 na vichomeo vyake yalitolewa kwa kila Wilaya Tanzania Bara kwa bei ya ruzuku ya 50% na kwamba zoezi hili linaendelea.

"Lengo ni kumhamasisha kila mwananchi kuhama kutoka kwenye matumizi ya kuni na mkaa kuja huku kwenye nishati safi ya kupikia na kwa wale ambao tunaona inachukua muda kubadilika tumewaletea teknolojia inayotumia mkaa kidogo tukitaraji taratibu watahama," alisema.

Vilevile alibainisha kuwa REA inatekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alivyoelekeza taasisi zinazolisha Zaidi ya watu mia kutumia nishati safi ya kupikia.

"Tunatekeleza agizo hili la Mhe. Rais tumeanza kuhamasisha na kuwezesha hizi taasisi kuhama ikiwemo Jeshi la Magereza ambapo maeneo 211 yakiwemo magereza 129, kambi za magereza 47, ofisi za mikoa za Magereza 26, nyumba za watumishi wa Magereza, vyuo, shule na hospitali zinasambaziwa nishati safi mbalimbali za kupikia," alisema.

Alizitaja nishati zilizosambazwa katika taasisi hizo kuwa ni pamoja na mifumo ya bayogesi, mifumo ya gesi ya mitungi (LPG), mifumo ya gesi asilia, mkaa unaotokana na makaa ya mawe na mashine za kutengenezea mkaa mbadala.

Aidha, alisema wakala vilevile unawajengea uwezo Maafisa wa Magereza wapatao 280 kuhusu suala zima la nishati safi ya kupikia.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma
 

Share

Print
«September 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
31123456
789
Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

IRINGA, Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini kwa kuendesha mafunzo maalum ya wiki moja yaliyolenga kujenga uwezo wa waendelezaji wa miradi midogo ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower).

Mafunzo hayo yaliyoanza tarehe 7 Septemba, 2026 katika Hoteli ya Sunset mkoani Iringa, yamewakutanisha waendelezaji wa miradi (Developers) zaidi ya 15, hususan kutoka maeneo ya Nyanda za Juu Kusini. Lengo kuu ni kuwajengea uwezo wa kiufundi ili kuongeza ubora wa miradi yao ili iweze kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, tarehe 9 Septemba, 2026, Kaimu Meneja wa Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi kutoka REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya, alisema kuwa REA haishii tu kutoa msaada wa upatikanaji wa nishati vijijini, bali inajikita pia katika kuongeza ujuzi wa wataalamu wa ndani.

"Kuongeza ujuzi kwa waendelezaji hawa kutasaidia kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu na ubora unaohitajika. Hatua hii itaongeza idadi ya miradi inayofikia vigezo vya kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa, kuongeza uzalishaji wa umeme, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii vijijini," alisema Mhandisi Yesaya.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ushirikiano kati ya REA na Wataalamu kutoka Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia (CoET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Maeneo yaliyofundishwa ni pamoja na usanifu wa miradi, upembuzi yakinifu, sayansi ya maji (hydrology), uhandisi wa umeme na elektroniki, pamoja na uendeshaji na matengenezo ya mitambo.

Mbali na mafunzo, REA imebainisha kuwa imekuwa ikisaidia waendelezaji hao kupitia ruzuku za ujenzi, maandalizi ya maandiko ya miradi na usanifu.

Aidha, Wakala huo upo katika mchakato wa kuandaa mfumo wa mikataba ya muda mrefu (Framework Contract) na taasisi za elimu ili kutoa mafunzo endelevu kwenye nishati jadidifu ikiwemo nishati ya jua na mifumo ya gesi vunde.

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wamepongeza mafunzo hayo; akizungumza na Wanahabari, Mhandisi Denis Makoyi kutoka kampuni ya Africa Power Investment, alisema mafunzo hayo yameongeza uelewa mkubwa wa kiufundi katika hatua za utekelezaji wa miradi. Naye Lutengano Kigola kutoka mradi wa Nyalawa Hydropower, aliongeza kuwa mafunzo hayo yanathibitisha kuwa Tanzania ina wataalamu wa ndani wenye uwezo mkubwa wa kuendeleza miradi ya umeme wa maji.

  • MWISHO –

 

Read more
10111213
14
REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuwezesha waendelezaji wadogo wa miradi ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kwa kutoa fedha, msaada wa kitaalamu na mafunzo, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa nishati nchini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top