Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA
Frank A. Mugogo 298

Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA

Wabia wa Maendeleo ambao wanafadhili miradi ya kusambaza nishati vijijini wamepongeza Wakala wa Nishati Vijijini kwa utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini ambayo inaleta tija kwa ustawi wa wananchi.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Wabia hao ambaye ni Naibu Balozi wa Norway na Mkuu wa Idara ya Ushirikiano, Kjetil Schie wakati wa Mkutano wa Kwanza wa Mwaka kati ya REA na Wabia wa Maendeleo ambao umefanyika tarehe 05 Aprili 2024 katika hoteli ya Tanga Beach Resort and Spar iliyopo katika Mkoa wa Tanga.

Schie alisema kuwa wanatambua jitihada za Serikali za kusambaza nishati vijijini ikiwa ni pamoja na nishati safi ya kupikia na miradi ya kusambaza umeme vijijini pamoja na tija iliyopatikana, hivyo wataendelea kushirikiana na REA katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Awali akifungua Mkutano huo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Batilda Buriani alisema utekelezaji wa miradi ya kusambaza umeme vijijini umechangia kuleta mabadiliko ya kiuchumi na kijamii katika Mkoa wa Tanga na aliwataka wananchi wa Mkoa huo kuanzisha miradi ya uzalishaji mali ili waongeze kipato na kukuza ajira.

Aidha, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini, Balozi Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Gideon Kingu aliwashukuru Wabia wa Maendeleo kwa ushirikiano wao katika utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini na kuwahakikishia kuwa wataendelea kusimamia fedha zinazotolewa ili ziweze kuleta tija na ufanisi.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
28 Mtaa wa Medeli
41104 Tambukareli
Dodoma

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627
Mhandisi Saidy Awapongeza Watumishi wa REA

Mhandisi Saidy Awapongeza Watumishi wa REA

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy amewapongeza Watumishi wa Wakala huo kwa kufanya kazi kwa bidii na kujituma hali iliyopelekea kukamilika kwa miradi inayotekelezwa na REA kwa wakati na katika ubora ulikusudiwa.

Read more
282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top