Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA
Frank A. Mugogo 309

Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA

Wabia wa Maendeleo ambao wanafadhili miradi ya kusambaza nishati vijijini wamepongeza Wakala wa Nishati Vijijini kwa utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini ambayo inaleta tija kwa ustawi wa wananchi.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Wabia hao ambaye ni Naibu Balozi wa Norway na Mkuu wa Idara ya Ushirikiano, Kjetil Schie wakati wa Mkutano wa Kwanza wa Mwaka kati ya REA na Wabia wa Maendeleo ambao umefanyika tarehe 05 Aprili 2024 katika hoteli ya Tanga Beach Resort and Spar iliyopo katika Mkoa wa Tanga.

Schie alisema kuwa wanatambua jitihada za Serikali za kusambaza nishati vijijini ikiwa ni pamoja na nishati safi ya kupikia na miradi ya kusambaza umeme vijijini pamoja na tija iliyopatikana, hivyo wataendelea kushirikiana na REA katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Awali akifungua Mkutano huo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Batilda Buriani alisema utekelezaji wa miradi ya kusambaza umeme vijijini umechangia kuleta mabadiliko ya kiuchumi na kijamii katika Mkoa wa Tanga na aliwataka wananchi wa Mkoa huo kuanzisha miradi ya uzalishaji mali ili waongeze kipato na kukuza ajira.

Aidha, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini, Balozi Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Gideon Kingu aliwashukuru Wabia wa Maendeleo kwa ushirikiano wao katika utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini na kuwahakikishia kuwa wataendelea kusimamia fedha zinazotolewa ili ziweze kuleta tija na ufanisi.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
28 Mtaa wa Medeli
41104 Tambukareli
Dodoma

Share

Print
«May 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
2829301234
567891011
12131415
Zaidi ya Bilioni 17 Kusambaza Umeme Vitongojini Singida

Zaidi ya Bilioni 17 Kusambaza Umeme Vitongojini Singida

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa Shilingi Bilioni 17.39 wa kusambaza umeme katika vitongoji 120 utakaonufaisha Kaya 3,960 Mkoani Singida.

Read more
16
Mkurugenzi Mkuu REA Aisisitiza Bodi Mpya ya Zabuni Kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu

Mkurugenzi Mkuu REA Aisisitiza Bodi Mpya ya Zabuni Kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy ameielekeza Bodi mpya ya Zabuni (Tender Board) ya Wakala kuhakikisha inatekeleza majukumu yake kwa kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu ili kuleta tija katika kazi zake.

Read more
1718
19
Benki ya Dunia Yaridhishwa na Utekelezwaji wa Miradi ya REA

Benki ya Dunia Yaridhishwa na Utekelezwaji wa Miradi ya REA

Benki ya Dunia (WB) yaihakikishia ushirikiano Serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika utekelezaji wa miradi ya Nishati kote nchini kwa ulinzi wa mazingira na ustawi wa Taifa kwa ujumla.

Read more
202122232425
2627282930311
2345678

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top