Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA
Frank A. Mugogo 238

Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA

Wabia wa Maendeleo ambao wanafadhili miradi ya kusambaza nishati vijijini wamepongeza Wakala wa Nishati Vijijini kwa utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini ambayo inaleta tija kwa ustawi wa wananchi.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Wabia hao ambaye ni Naibu Balozi wa Norway na Mkuu wa Idara ya Ushirikiano, Kjetil Schie wakati wa Mkutano wa Kwanza wa Mwaka kati ya REA na Wabia wa Maendeleo ambao umefanyika tarehe 05 Aprili 2024 katika hoteli ya Tanga Beach Resort and Spar iliyopo katika Mkoa wa Tanga.

Schie alisema kuwa wanatambua jitihada za Serikali za kusambaza nishati vijijini ikiwa ni pamoja na nishati safi ya kupikia na miradi ya kusambaza umeme vijijini pamoja na tija iliyopatikana, hivyo wataendelea kushirikiana na REA katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Awali akifungua Mkutano huo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Batilda Buriani alisema utekelezaji wa miradi ya kusambaza umeme vijijini umechangia kuleta mabadiliko ya kiuchumi na kijamii katika Mkoa wa Tanga na aliwataka wananchi wa Mkoa huo kuanzisha miradi ya uzalishaji mali ili waongeze kipato na kukuza ajira.

Aidha, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini, Balozi Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Gideon Kingu aliwashukuru Wabia wa Maendeleo kwa ushirikiano wao katika utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini na kuwahakikishia kuwa wataendelea kusimamia fedha zinazotolewa ili ziweze kuleta tija na ufanisi.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
28 Mtaa wa Medeli
41104 Tambukareli
Dodoma

Rate article

3.2
Rate this article:
3.2

Share

Print
«July 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
24252627282930
1234
National Clean Cooking Strategy (2024 – 2034)

National Clean Cooking Strategy (2024 – 2034)

The Government of the United Republic of Tanzania, in collaboration with various stakeholders has prepared the National Clean Cooking Strategy. The strategy aims to ensure that 80 percent of Tanzanians use clean cooking solutions by the year 2034.

Read more
567
891011121314
15161718192021
Vijiji 151 Vimebaki Nchi Nzima Kupata Huduma ya Umeme – Kapinga

Vijiji 151 Vimebaki Nchi Nzima Kupata Huduma ya Umeme – Kapinga

Ni vijiji 151 tu nchi nzima ndio ambavyo bado havijafikiwa na huduma ya umeme kati ya Vijiji zaidi ya 12,000 ambapo wilayani Ludewa mkoani Njombe vimebaki Vijiji nane.

Read more
22232425262728
2930311234

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top