Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA
Frank A. Mugogo 292

Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA

Wabia wa Maendeleo ambao wanafadhili miradi ya kusambaza nishati vijijini wamepongeza Wakala wa Nishati Vijijini kwa utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini ambayo inaleta tija kwa ustawi wa wananchi.

Pongezi hizo zimetolewa na Mwenyekiti wa Wabia hao ambaye ni Naibu Balozi wa Norway na Mkuu wa Idara ya Ushirikiano, Kjetil Schie wakati wa Mkutano wa Kwanza wa Mwaka kati ya REA na Wabia wa Maendeleo ambao umefanyika tarehe 05 Aprili 2024 katika hoteli ya Tanga Beach Resort and Spar iliyopo katika Mkoa wa Tanga.

Schie alisema kuwa wanatambua jitihada za Serikali za kusambaza nishati vijijini ikiwa ni pamoja na nishati safi ya kupikia na miradi ya kusambaza umeme vijijini pamoja na tija iliyopatikana, hivyo wataendelea kushirikiana na REA katika utekelezaji wa miradi hiyo.

Awali akifungua Mkutano huo, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Batilda Buriani alisema utekelezaji wa miradi ya kusambaza umeme vijijini umechangia kuleta mabadiliko ya kiuchumi na kijamii katika Mkoa wa Tanga na aliwataka wananchi wa Mkoa huo kuanzisha miradi ya uzalishaji mali ili waongeze kipato na kukuza ajira.

Aidha, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini, Balozi Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Gideon Kingu aliwashukuru Wabia wa Maendeleo kwa ushirikiano wao katika utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini na kuwahakikishia kuwa wataendelea kusimamia fedha zinazotolewa ili ziweze kuleta tija na ufanisi.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
28 Mtaa wa Medeli
41104 Tambukareli
Dodoma

Share

Print
«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top