Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Zaidi ya Bilioni 17 Kusambaza Umeme Vitongojini Singida
Frank A. Mugogo 117

Zaidi ya Bilioni 17 Kusambaza Umeme Vitongojini Singida

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa Shilingi Bilioni 17.39 wa kusambaza umeme katika vitongoji 120 utakaonufaisha Kaya 3,960 Mkoani Singida.

Mkurugenzi wa Umeme Vijijini (REA), Mhandisi Jones Olotu amebainisha hayo Mei 14, 2025 Mkoani Singida wakati wa kumtambulisha Mkandarasi aliyeshinda zabuni ya kutekeleza mradi huo Kampuni ya M/s Transpower Limited na Whitecity International Contractor Ltd JV kwa Mkuu wa Mkoa huo, Halima Dendego.

“Tunamshukuru Rais wetu Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia kiasi cha shilingi 17,394,214,690.85 kitumike kusambaza umeme katika vitongoji 120 Mkoani hapa, leo hii tumefika hapa kumtambulisha Mkandarasi na maandalizi ya awali ya kutekeleza mradi yameanza,” alisema Mhandisi Olotu.

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Halima Dendego alimshukuru Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha nyingi za kutekeleza miradi ya kufikisha huduma ya umeme kwa wananchi mkoani humo hasa ikizingatiwa kuwa umeme ni miongoni mwa mahitaji muhimu kwa maendeleo ya jamii.

“Ninayo furaha kubwa leo hii kumpokea mkandarasi huyu kwani kama mtakumbuka Serikali iliahidi ifikapo 2025 itakuwa imekamilisha kufikisha umeme kwenye vijiji vyote Tanzania Bara na sasa tumeshuhudia kabla hata ya 2025 vijiji vyote vilikuwa vimefikiwa na umeme na sasa tunatekeleza vitongojini,” alisema Mhe. Dendego.

Mhe. Dendego aliipongeza REA kwa kuendelea kutekeleza miradi yake kwa ufanisi na uwazi na pia alimpongeza mkandarasi kwa ahadi yake aliyoitoa ya kukamilisha mradi huo kwa miezi 12 badala ya 24 kama ilivyo katika mkataba wake.

“Nimefarijika, tumepata mkandarasi mzuri kwani ametuahidi hapa atakamilisha kazi ndani ya miezi 12 nasi tutampatia ushirikiano na tutamsimamia ipasavyo ili ahadi hii ikamilike kwa kupata mradi bora,” alisema.

Akizungumzia utekelezaji wa mradi wa kufikisha umeme katika vitongoji Mkoani humo, Mhandisi Olotu alisema kati ya vitongoji 2,289 vilivyopo mkoani humo, vitongoji 1,052 vimefikishiwa umeme na kwamba vitongoji 120 vitakavyopata umeme awamu hii vitaongeza idadi ya vitongoji vitakavyokuwa na umeme Mkoani humo.

Alisema mradi unatekelezwa katika vitongoji vya Wilaya za Singida DC, Ikungi, Manyoni, Mkalama na Iramba na kwamba vitongoji vitakavyobaki vitaendelea kusambaziwa umeme kulingana na upatikanaji wa fedha.

“Kwa mujibu wa mkataba, mradi huu unapaswa kutekelezwa ndani ya miezi 24 lakini mkandarasi ametuahidi na kutuhakikishia kuwa ndani ya kipindi cha miezi 12 atakuwa amekamilisha mradi,” alibainisha Mhandisi Olotu.

Kwa upande wake Meneja Usimamizi wa Miradi kutoka REA, Mhandisi Romanus Lwena alisisitiza kuwa umeme ni hitaji la muhimu na kwa kutambua hilo Serikali imewekeza fedha nyingi kuhakikisha wananchi wote wanafikiwa.

“Serikali imetoa fedha nyingi kutekeleza miradi ya kusambaza umeme kote nchini, wito wetu kwa wananchi ni kuwapa ushirikiano wakandarasi na kuwa walinzi wa miundombinu hii,” alisisitiza Mhandisi Lwena.

Kwa upande wake mwakilishi wa Mkandarasi ambaye ni Meneja Mradi kutoka Kampuni ya Transpower Ltd, Mhandisi Jackline Mushi aliahidi kufanya kazi kwa weledi na kukamilisha mradi kwa muda mfupi na kwa ubora unaopaswa.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«July 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
30
REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

Serikali imesambaza kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza (Gereza la Ukonga) mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko yake 464 ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kama njia ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia nchini ambapo msisitizo ni angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia Nishati Safi ifikapo Mwaka 2034.

Read more
1
Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa vitendo.

Read more
2
REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

Katika kuendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imegawa jumla ya mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko ya sahani mbili 461 kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Mara.

Read more
3
REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mpango wa kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petrol na dizeli) maeneo ya vijijini ili kuondoa madhara yatokanayo na njia zisizo salama.

Read more
4
Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewasihi Watanzania kote nchini kuachana na dhana ya kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni gharama ikilinganishwa na matumizi ya kuni na mkaa.

Read more
5
Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Imeelezwa kuwa hadi kufikia mwaka 2030 vitongoji vyote Tanzania Bara vitakuwa vimefikishiwa nishati ya umeme kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa na kusimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Read more
6
78
REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

REA Yajizatiti Kufikisha Lengo la Taifa Kwenye Nishati Safi ya Kupikia

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amesema Wakala umejizatiti kuhakikisha 80% ya Watanzania wanatumia Nishati Safi ya Kupikia ifikapo mwaka 2034 kama ilivyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
910111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top