Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mkurugenzi Mkuu REA Aisisitiza Bodi Mpya ya Zabuni Kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu
Frank A. Mugogo 81

Mkurugenzi Mkuu REA Aisisitiza Bodi Mpya ya Zabuni Kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy ameielekeza Bodi mpya ya Zabuni (Tender Board) ya Wakala kuhakikisha inatekeleza majukumu yake kwa kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu ili kuleta tija katika kazi zake.

Ametoa wito huo Mei 15, 2025 Jijini Dodoma wakati wa hafla fupi ya kuiaga Bodi ya Zabuni iliyomaliza muda wake baada ya kutumikia kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo.

"Ninawapongeza walioteuliwa katika Bodi mpya ya Zabuni lakini niwasisitize mhakikishe mnatekeleza majukumu yenu kwa weledi ikiwemo kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu za Ununuzi wa Umma," alisisitiza Mhandisi Saidy.

Aidha, aliishukuru na kuipongeza Bodi ya Zabuni iliyomaliza muda wake kwa kazi nzuri iliyofanya kipindi chote cha muda wake.

Alisema Bodi ya Zabuni ni chombo na nyenzo muhimu katika utekelezaji wa majukumu ya taasisi na aliwasihi walioteuliwa kuhakikisha wanatambua thamani waliyopewa.

"Bodi ya Zabuni ni muhimu sana katika uendeshaji wa shughuli mbalimbali za Ununuzi za taasisi na ukiona umeteuliwa basi elewa kuwa wewe ni mtu sahihi na hakikisha hautoki nje ya taratibu," alisisitiza Mkurugenzi Saidy.

Vilevile alikipongeza Kitengo cha Ununuzi kwa kazi nzuri kinayofanya na aliwasisitiza kuielewa kwa undani Sheria ya Ununuzi ili kuwa na ununuzi wenye tija na uliyozingatia taratibu zote muhimu.

Aidha, akizungumza kwa niaba ya Bodi, Mwenyekiti wa Bodi iliyomaliza muda wake ambaye pia anaendelea kuhudumu katika Bodi mpya, Mhandisi Advera Mwijage alimshukuru Mkurugenzi Mkuu kwa sapoti aliyotoa muda wote alipohitajika pamoja na Kitengo cha Ununuzi ambao walifanya kazi kwa karibu na Bodi.

"Ninawashukuru Wajumbe wa Bodi waliomaliza muda wao, tumefanya kazi kwa ushirikiano mkubwa kuhakikisha suala la Ununuzi kwa ujumla linafanyika kwa kuzingatia Sheria na miongozo iliyopo," alisema Mhandisi Advera.

Awali akizungumza wakati wa hafla hiyo, Katibu wa Bodi ya Zabuni REA ambaye pia ni Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi, Ndg. Mapesi Manyama alifafanua Sheria zinazoelekeza uundaji wa Bodi ya Zabuni kwa taasisi.

"Bodi ya Zabuni inaundwa na kuendeshwa kwa mujibu wa Kifungu Namba 32 pamoja na Jedwali Namba 2 ndani ya Sheria ya Ununuzi wa Umma ya Mwaka 2023 na Kanuni zake za Mwaka 2025," alifafanua Manyama.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma
 

Share

Print
«June 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
2627
Umoja Wa Ulaya Waipa Kongole REA

Umoja Wa Ulaya Waipa Kongole REA

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unaendelea kuhamasisha wananchi kutumia Nishati Safi ya Kupikia ili ifikapo mwaka 2034, asilimia 80 ya wananchi wawe wanatumia nishati safi ya kupikia kama inavyoelekezwa katika Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 2024-2034.

Read more
28
Lesotho Wavutiwa na REA

Lesotho Wavutiwa na REA

Serikali ya Lesotho imevutiwa na namna ambavyo Serikali ya Tanzania kupitia Wakala wa Nishati Vijijiji (REA) imepiga hatua katika suala zima la usambazaji wa nishati safi maeneo ya vijijini.

Read more
293031
REA Yahamasisha Wananchi Kutumia Mkaa Mbadala

REA Yahamasisha Wananchi Kutumia Mkaa Mbadala

Wakala wa Nishati Vijijini unahamasisha wananchi kote nchini kutumia nishati safi ya kupikia ikiwemo Mkaa mbadala ambao umeelezwa kuwa na gharama nafuu na ni salama kwa afya ya mtumiaji na mazingira.

Read more
1
23
The National Clean Cooking Communication Strategy launched

The National Clean Cooking Communication Strategy launched

Tanzania is embarking on a bold and transformative journey that places clean cooking at the heart of public health, environmental protection, and inclusive development. Global data shows that over 2.1 billion people lack access to clean cooking solutions. In Sub-Saharan Africa, nearly one billion people remain reliant on polluting fuels, and Tanzania stands among the countries most in need of an accelerated transition.

Read more
45678
9101112131415
161718
Waendelezaji wa Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Lupali Mkoani Njombe Waelekezwa Kuimarisha Ulinzi na Usalama wa Mradi

Waendelezaji wa Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Lupali Mkoani Njombe Waelekezwa Kuimarisha Ulinzi na Usalama wa Mradi

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu Jacob Kingu ameelekeza waendelezaji wa mradi wa kuzalisha umeme wa kilowati 317 kwa kutumia maporomoko ya Mto Lupali kuimarisha ulinzi na usalama wa mradi ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza.

Read more
1920
Waendelezaji Miradi ya Nishati Jadidifu Watakiwa Kuchangamkia Fursa za Uwezeshwaji Kutoka REA

Waendelezaji Miradi ya Nishati Jadidifu Watakiwa Kuchangamkia Fursa za Uwezeshwaji Kutoka REA

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Mhe. Balozi Meja Jenerali Mstaafu, Jacob Kingu ametoa wito kwa waendelezaji wa miradi ya nishati jadidifu kote nchini kuchangamkia fursa za uwezeshwaji zinazotolewa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ili kuwa na miradi yenye tija kwa Taifa.

Read more
2122
23242526272829
30123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top