Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mkurugenzi Mkuu REA Aisisitiza Bodi Mpya ya Zabuni Kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu
Frank A. Mugogo 120

Mkurugenzi Mkuu REA Aisisitiza Bodi Mpya ya Zabuni Kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy ameielekeza Bodi mpya ya Zabuni (Tender Board) ya Wakala kuhakikisha inatekeleza majukumu yake kwa kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu ili kuleta tija katika kazi zake.

Ametoa wito huo Mei 15, 2025 Jijini Dodoma wakati wa hafla fupi ya kuiaga Bodi ya Zabuni iliyomaliza muda wake baada ya kutumikia kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo.

"Ninawapongeza walioteuliwa katika Bodi mpya ya Zabuni lakini niwasisitize mhakikishe mnatekeleza majukumu yenu kwa weledi ikiwemo kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu za Ununuzi wa Umma," alisisitiza Mhandisi Saidy.

Aidha, aliishukuru na kuipongeza Bodi ya Zabuni iliyomaliza muda wake kwa kazi nzuri iliyofanya kipindi chote cha muda wake.

Alisema Bodi ya Zabuni ni chombo na nyenzo muhimu katika utekelezaji wa majukumu ya taasisi na aliwasihi walioteuliwa kuhakikisha wanatambua thamani waliyopewa.

"Bodi ya Zabuni ni muhimu sana katika uendeshaji wa shughuli mbalimbali za Ununuzi za taasisi na ukiona umeteuliwa basi elewa kuwa wewe ni mtu sahihi na hakikisha hautoki nje ya taratibu," alisisitiza Mkurugenzi Saidy.

Vilevile alikipongeza Kitengo cha Ununuzi kwa kazi nzuri kinayofanya na aliwasisitiza kuielewa kwa undani Sheria ya Ununuzi ili kuwa na ununuzi wenye tija na uliyozingatia taratibu zote muhimu.

Aidha, akizungumza kwa niaba ya Bodi, Mwenyekiti wa Bodi iliyomaliza muda wake ambaye pia anaendelea kuhudumu katika Bodi mpya, Mhandisi Advera Mwijage alimshukuru Mkurugenzi Mkuu kwa sapoti aliyotoa muda wote alipohitajika pamoja na Kitengo cha Ununuzi ambao walifanya kazi kwa karibu na Bodi.

"Ninawashukuru Wajumbe wa Bodi waliomaliza muda wao, tumefanya kazi kwa ushirikiano mkubwa kuhakikisha suala la Ununuzi kwa ujumla linafanyika kwa kuzingatia Sheria na miongozo iliyopo," alisema Mhandisi Advera.

Awali akizungumza wakati wa hafla hiyo, Katibu wa Bodi ya Zabuni REA ambaye pia ni Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi, Ndg. Mapesi Manyama alifafanua Sheria zinazoelekeza uundaji wa Bodi ya Zabuni kwa taasisi.

"Bodi ya Zabuni inaundwa na kuendeshwa kwa mujibu wa Kifungu Namba 32 pamoja na Jedwali Namba 2 ndani ya Sheria ya Ununuzi wa Umma ya Mwaka 2023 na Kanuni zake za Mwaka 2025," alifafanua Manyama.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma
 

Share

Print
«August 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
28293031123
45
Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

The Rural Energy Agency (REA) is seeking proposals from qualified service providers for the supply, installation, and testing of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in eight remote villages across Geita, Ludewa and Mbulu districts. Those villages are located in remote areas with challenging geographical conditions, hence, impractical for grid extension.

Please find the attached documents:

•    Application Form for Supply and Installation of SA-SHS; and
•    Call for Proposals for Result Based Financing Installation of Stand Alone Solar Home Systems.

Read more
678910
111213
Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Wananchi Kijiji cha Usevya Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi wamepongeza hatua zinazochukuliwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kuhakikisha wanafikiwa na nishati safi ya kupikia kwa bei ya ruzuku.

Read more
1415
Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetoa wito kwa viongozi wa dini nchini kushiriki kikamilifu katika kampeni ya kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa lengo la kulinda afya na kuokoa mazingira.

Read more
1617
181920
Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Watanzania wameendelea kuhamasishwa kutumia nishati safi ya kupikia ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Read more
21222324
25262728293031
1234567

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top