Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mkurugenzi Mkuu REA Aisisitiza Bodi Mpya ya Zabuni Kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu
Frank A. Mugogo 590

Mkurugenzi Mkuu REA Aisisitiza Bodi Mpya ya Zabuni Kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy ameielekeza Bodi mpya ya Zabuni (Tender Board) ya Wakala kuhakikisha inatekeleza majukumu yake kwa kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu ili kuleta tija katika kazi zake.

Ametoa wito huo Mei 15, 2025 Jijini Dodoma wakati wa hafla fupi ya kuiaga Bodi ya Zabuni iliyomaliza muda wake baada ya kutumikia kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo.

"Ninawapongeza walioteuliwa katika Bodi mpya ya Zabuni lakini niwasisitize mhakikishe mnatekeleza majukumu yenu kwa weledi ikiwemo kufuata Sheria, Kanuni na Taratibu za Ununuzi wa Umma," alisisitiza Mhandisi Saidy.

Aidha, aliishukuru na kuipongeza Bodi ya Zabuni iliyomaliza muda wake kwa kazi nzuri iliyofanya kipindi chote cha muda wake.

Alisema Bodi ya Zabuni ni chombo na nyenzo muhimu katika utekelezaji wa majukumu ya taasisi na aliwasihi walioteuliwa kuhakikisha wanatambua thamani waliyopewa.

"Bodi ya Zabuni ni muhimu sana katika uendeshaji wa shughuli mbalimbali za Ununuzi za taasisi na ukiona umeteuliwa basi elewa kuwa wewe ni mtu sahihi na hakikisha hautoki nje ya taratibu," alisisitiza Mkurugenzi Saidy.

Vilevile alikipongeza Kitengo cha Ununuzi kwa kazi nzuri kinayofanya na aliwasisitiza kuielewa kwa undani Sheria ya Ununuzi ili kuwa na ununuzi wenye tija na uliyozingatia taratibu zote muhimu.

Aidha, akizungumza kwa niaba ya Bodi, Mwenyekiti wa Bodi iliyomaliza muda wake ambaye pia anaendelea kuhudumu katika Bodi mpya, Mhandisi Advera Mwijage alimshukuru Mkurugenzi Mkuu kwa sapoti aliyotoa muda wote alipohitajika pamoja na Kitengo cha Ununuzi ambao walifanya kazi kwa karibu na Bodi.

"Ninawashukuru Wajumbe wa Bodi waliomaliza muda wao, tumefanya kazi kwa ushirikiano mkubwa kuhakikisha suala la Ununuzi kwa ujumla linafanyika kwa kuzingatia Sheria na miongozo iliyopo," alisema Mhandisi Advera.

Awali akizungumza wakati wa hafla hiyo, Katibu wa Bodi ya Zabuni REA ambaye pia ni Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi, Ndg. Mapesi Manyama alifafanua Sheria zinazoelekeza uundaji wa Bodi ya Zabuni kwa taasisi.

"Bodi ya Zabuni inaundwa na kuendeshwa kwa mujibu wa Kifungu Namba 32 pamoja na Jedwali Namba 2 ndani ya Sheria ya Ununuzi wa Umma ya Mwaka 2023 na Kanuni zake za Mwaka 2025," alifafanua Manyama.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma
 

Share

Print
«February 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
2627
Rais Samia Apeleka Neema ya Umeme Katika Vitongoji Lindi

Rais Samia Apeleka Neema ya Umeme Katika Vitongoji Lindi

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa shilingi bilioni 25.8 wa kusambaza umeme katika vitongoji 159 utakaonufaisha kaya 5,116 Mkoani Lindi.

Read more
2829
Shangwe Mtwara - Bilioni 15.3 Kusambaza Umeme Vitongoji 175

Shangwe Mtwara - Bilioni 15.3 Kusambaza Umeme Vitongoji 175

Wananchi wa vitongoji vya Msokole na Funguni Kijiji cha Mnazi Kata ya Nalingu Mkoani Mtwara wameishukuru Serikali kwa kuwapelekea mradi wa Umeme unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ambao wamesema unakwenda kubadili maisha yao.

Read more
3031
Mkandarasi Northern Engineering Atakiwa Kuongeza Kasi Ya Ujenzi Wa Mradi Mtwara

Mkandarasi Northern Engineering Atakiwa Kuongeza Kasi Ya Ujenzi Wa Mradi Mtwara

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemtaka Mkandarasi anayetekeleza Mradi wa Kusambaza umeme katika Vitongoji 150 vya Majimbo 10 Mkoani Mtwara kuongeza kasi ya ujenzi ili kukamilisha Mradi kwa wakati.

Read more
1
2
Ukaguzi wa Mradi wa Kusambaza Umeme Mkoani Ruvuma

Ukaguzi wa Mradi wa Kusambaza Umeme Mkoani Ruvuma

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umemtaka Mkandarasi Kampuni ya CCC International Engineering Nigeria Ltd anayetekeleza Mradi wa Kusambaza umeme katika Vitongoji 135 vya Majimbo 9 ya uchaguzi Mkoani Ruvuma kuongeza kasi ya ujenzi ili kukamilisha Mradi huo kwa wakati.

Read more
345678
9101112131415
16171819202122
2324252627281
2345678

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top