Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
ZIARA YA VIONGOZI WA WAKALA WA NISHATI VIJIJINI (REA) KATIKA WILAYA YA KILOLO
Admin.Frank Mugogo 9534

ZIARA YA VIONGOZI WA WAKALA WA NISHATI VIJIJINI (REA) KATIKA WILAYA YA KILOLO

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati vijijini (REA), Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga aliongoza ujumbe wa viongozi wa Wakala ziara ya siku moja iliyofanyika tarehe 17/06/2017 katika Wilaya ya Kilolo, Mkoa wa Iringa.

Lengo la ziara hiyo ilikuwa ni kutathmini matokeo chanya yaliyotokana na utekelezwaji wa miradi ya kusambaza umeme vijijini katika wilaya ya Kilolo ambapo wilaya hiyo ni mojawapo ya wilaya zilizopatiwa miradi ya awali ya Wakala ambayo ilitekelezwa katika kipindi cha kuanzia Mwaka 2008 hadi Mwaka 2010.

Wilaya ya Kilolo, ambayo ina jumla ya wateja waliounganishiwa umeme 2,961, imeendelea kunufaika na awamu nyingine za miradi ya Wakala. Miongoni mwa wateja hao waliounganishwa ni shule za msingi 10, shule za sekondari 10, zahanati 9 na pampu ya maji. Pia mashine za kusaga na kukoboa nafaka, mashine za kuranda mbao na kuchomelea vyuma zimeunganishwa na huduma za umeme.

Miradi ya kusambaza umeme vijijini katika Wilaya ya Kilolo imechochea shughuli za uzalishaji mali na biashara katika nyanja za kilimo na ufugaji ambapo kuna mashamba makubwa kama ya Ndoto Farm, Makota Farm na Bill Clinton Foundation yanaendeshwa kwa kutumia huduma za umeme. Pia viwanda vidogo vidogo vya kusindika mazao ya kilimo vimeunganishwa na huduma ya umeme.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top