Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
ZIARA YA VIONGOZI WA WAKALA WA NISHATI VIJIJINI (REA) KATIKA WILAYA YA KILOLO
Admin.Frank Mugogo 9540

ZIARA YA VIONGOZI WA WAKALA WA NISHATI VIJIJINI (REA) KATIKA WILAYA YA KILOLO

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati vijijini (REA), Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga aliongoza ujumbe wa viongozi wa Wakala ziara ya siku moja iliyofanyika tarehe 17/06/2017 katika Wilaya ya Kilolo, Mkoa wa Iringa.

Lengo la ziara hiyo ilikuwa ni kutathmini matokeo chanya yaliyotokana na utekelezwaji wa miradi ya kusambaza umeme vijijini katika wilaya ya Kilolo ambapo wilaya hiyo ni mojawapo ya wilaya zilizopatiwa miradi ya awali ya Wakala ambayo ilitekelezwa katika kipindi cha kuanzia Mwaka 2008 hadi Mwaka 2010.

Wilaya ya Kilolo, ambayo ina jumla ya wateja waliounganishiwa umeme 2,961, imeendelea kunufaika na awamu nyingine za miradi ya Wakala. Miongoni mwa wateja hao waliounganishwa ni shule za msingi 10, shule za sekondari 10, zahanati 9 na pampu ya maji. Pia mashine za kusaga na kukoboa nafaka, mashine za kuranda mbao na kuchomelea vyuma zimeunganishwa na huduma za umeme.

Miradi ya kusambaza umeme vijijini katika Wilaya ya Kilolo imechochea shughuli za uzalishaji mali na biashara katika nyanja za kilimo na ufugaji ambapo kuna mashamba makubwa kama ya Ndoto Farm, Makota Farm na Bill Clinton Foundation yanaendeshwa kwa kutumia huduma za umeme. Pia viwanda vidogo vidogo vya kusindika mazao ya kilimo vimeunganishwa na huduma ya umeme.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627
Mhandisi Saidy Awapongeza Watumishi wa REA

Mhandisi Saidy Awapongeza Watumishi wa REA

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy amewapongeza Watumishi wa Wakala huo kwa kufanya kazi kwa bidii na kujituma hali iliyopelekea kukamilika kwa miradi inayotekelezwa na REA kwa wakati na katika ubora ulikusudiwa.

Read more
282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top