Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
ZIARA YA VIONGOZI WA WAKALA WA NISHATI VIJIJINI (REA) KATIKA WILAYA YA KILOLO
Admin.Frank Mugogo 9510

ZIARA YA VIONGOZI WA WAKALA WA NISHATI VIJIJINI (REA) KATIKA WILAYA YA KILOLO

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati vijijini (REA), Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga aliongoza ujumbe wa viongozi wa Wakala ziara ya siku moja iliyofanyika tarehe 17/06/2017 katika Wilaya ya Kilolo, Mkoa wa Iringa.

Lengo la ziara hiyo ilikuwa ni kutathmini matokeo chanya yaliyotokana na utekelezwaji wa miradi ya kusambaza umeme vijijini katika wilaya ya Kilolo ambapo wilaya hiyo ni mojawapo ya wilaya zilizopatiwa miradi ya awali ya Wakala ambayo ilitekelezwa katika kipindi cha kuanzia Mwaka 2008 hadi Mwaka 2010.

Wilaya ya Kilolo, ambayo ina jumla ya wateja waliounganishiwa umeme 2,961, imeendelea kunufaika na awamu nyingine za miradi ya Wakala. Miongoni mwa wateja hao waliounganishwa ni shule za msingi 10, shule za sekondari 10, zahanati 9 na pampu ya maji. Pia mashine za kusaga na kukoboa nafaka, mashine za kuranda mbao na kuchomelea vyuma zimeunganishwa na huduma za umeme.

Miradi ya kusambaza umeme vijijini katika Wilaya ya Kilolo imechochea shughuli za uzalishaji mali na biashara katika nyanja za kilimo na ufugaji ambapo kuna mashamba makubwa kama ya Ndoto Farm, Makota Farm na Bill Clinton Foundation yanaendeshwa kwa kutumia huduma za umeme. Pia viwanda vidogo vidogo vya kusindika mazao ya kilimo vimeunganishwa na huduma ya umeme.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«October 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
301
REA Kushiriki Samia Kilimo Biashara Expo 2024 Morogoro

REA Kushiriki Samia Kilimo Biashara Expo 2024 Morogoro

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) itashiriki katika Maonesho ya Samia KILIMO Biashara Expo 2024 kwa msimu wa tatu yanayotarajiwa kuanza tarehe 6 Oktoba, 2024 wilaya ya Gairo Mkoani Morogoro. 

Read more
23456
78910
Bukombe Waunga Mkono Jitihada za Rais Samia Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia

Bukombe Waunga Mkono Jitihada za Rais Samia Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi kote Nchini wametakiwa kuendelea kuunga mkono jitihada za Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kutumia Nishati Safi ya Kupikia ili kuimarisha afya zao sambamba na kutunza mazingira.

Read more
111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top