Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KITAIFA YALIYOFANYIKA KIJIJI CHA , BUTIAMA, MKOA WA MARA
Admin.Frank Mugogo 10294

MAADHIMISHO YA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KITAIFA YALIYOFANYIKA KIJIJI CHA , BUTIAMA, MKOA WA MARA

Tarehe 5 Juni, kila mwaka Watanzania wanaungana na mataifa mengine kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani. Kitaifa maadhimisho haya yalifanyika katika Kijiji cha Butiama, Mkoani Mara ambako Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ulishiriki.

Katika maadhimisho hayo, Wakala ulipata fursa ya kuonesha mpango wake wa kusambaza umeme vijijini katika Mkoa wa Mara na mikoa mingine pamoja na kupokea maoni na mahitaji ya wananchi wa Mkoa wa Mara ambao hawajafikiwa na huduma ya umeme.

Katika kuonesha uhalisia wa miradi ambayo inatekelezwa na Wakala, wakandarasi na waendelezaji wa miradi ya nishati vijijini walishiriki katika maadhimisho hayo kupitia banda la Wakala ambao ni pamoja na:

i. DERM Electric – Mkandarasi wa kusambaza umeme vijijini katika Mkoa wa Mara (Mradi Kabambe Awamu ya II);

ii. Angelique International Ltd – Mkandarasi wa kusambaza umeme vijijini katika Mkoa wa Mara (Mradi Kabambe Awamu ya III, kipengele cha Densification); na

iii. PowerGen Renewable Energy – Mradi wa umeme-jua (Solar Mini grid - LRTC 2014) katika eneo la Raranya, mkoani Mara.

Madhumuni ya maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ni kuhamasisha jamii kuelewa masuala yahusuyo mazingira na kuchukua hatua za kuhifadhi na kulinda mazingira. Kauli Mbiu iliyoongoza maadhimisho haya kitaifa ni “Hifadhi ya Mazingira: Muhimili kwa Tanzania ya viwanda”, lengo likiwa ni kuhamasisha utunzaji wa mazingira wakati tunapokuza maendeleo ya viwanda nchini.

Wakati wa maadhmisho hayo, banda la Wakala wa Nishati Vijijini lilitembelewa na wageni mbalimbali ikiwa ni pamoja na mgeni rasmi wakati wa kilele cha maadhmisho hayo ambaye alikuwa ni Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan. Pia wakazi wa kijiji cha Butiama, vitongoji mbalimbali na maeneo mengine ya Mkoa wa Mara walitembelea banda la Wakala wakiwa na shauku ya kujua utekelezwaji wa miradi mbalimbali.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S. L. P 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Barua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627
Mhandisi Saidy Awapongeza Watumishi wa REA

Mhandisi Saidy Awapongeza Watumishi wa REA

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy amewapongeza Watumishi wa Wakala huo kwa kufanya kazi kwa bidii na kujituma hali iliyopelekea kukamilika kwa miradi inayotekelezwa na REA kwa wakati na katika ubora ulikusudiwa.

Read more
282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top