Serikali kupitia Wakala na Mfuko wa Nishati Vijijini (REA/REF) inafadhili miradi ya kusambaza umeme vijijini katika mikoa yote ya Tanzania Bara. Miradi ya Awamu ya Pili ya Usambazaji Umeme Vijijini inatekelezwa na wakandarasi kutoka sekta binafsi ambao uhusika na ujenzi wa miundombinu.
The Government of United Republic of Tanzania and Sweden through Swedish International Development Agency (Sida) in Collaboration with the UK Government, through its Department for International Development – DFID, signed a Specific Agreement in which the Swedish and UK Governments will finance the development of rural energy modern services through the Rural Energy Fund (REF) which is managed by the Rural Energy Board (REB).
Gesi asilia iligunduliwa kwa mara ya kwanza hapa nchini Mwaka 1974 kwenye Kisiwa cha Songo Songo, Mkoani Lindi. Ugunduzi mwingine umefanyiaka katika maeneo ya Mtwara Vijijini (Mnazi Bay, 1982 na Ntorya, 2012), Mkuranga (Pwani, 2007) na Kiliwani (Lindi, 2008). Kiasi cha gesi asilia iliyogunduliwa katika maeneo haya inakadiriwa kuwa futi za ujazo trilioni 8. Katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita, kumekuwa na kasi kubwa ya utafutaji mafuta na gesi asilia uliojikita zaidi kwenye maji ya kina kirefu cha bahari. Kiasi cha gesi asilia iliyogunduliwa katika kina kirefu cha maji ni takribani futi za ujazo trilioni 33.7. Jumla ya gesi asilia iliyogunduliwa nchi kavu na baharini inafikia takribani futi za ujazo trilioni 41.7.
Wizara ya Nishati na Madini inapenda kutoa ufafanuzi wa miradi ya Gesi Asilia ambayo itatekelezwa kwa kushirikiana na wawekezaji katika Sekta ndogo ya Gesi Asilia na kueleza manufaa makubwa yatakayopatikana kwa wananchi wote wa Tanzania wakiwemo wale wa Mikoa ya Mtwara na Lindi.