Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Aodax K. Nshala 9282

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI: UTEKELEZAJI WA MIRADI YA KUSAMBAZA UMEME VIJIJINI

DAR ES SALAAM, 07 JANUARI 2016

Serikali kupitia Wakala na Mfuko wa Nishati Vijijini (REA/REF) inafadhili miradi ya kusambaza umeme vijijini katika mikoa yote ya Tanzania Bara. Miradi ya Awamu ya Pili ya Usambazaji Umeme Vijijini inatekelezwa na wakandarasi kutoka sekta binafsi ambao huhusika na ujenzi wa miundombinu ya usafirishaji na usambazaji umeme chini ya usimamizi wa TANESCO.

Malipo ya Huduma kwa Wakandarasi, Wakandarasi Wadogo na Vibarua

Kumekuwepo na malalamiko ya Kucheleweshwa kwa malipo ya wafanyakazi na vibarua pamoja na watoa huduma ambao wanashiriki katika ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme vijijini. Tunapenda kuwafahamisha wananchi kuwa katika utekelezaji wa miradi ya kusambaza umeme vijijini, Wakala umeingia mikataba na wakandarasi binafsi ambao wana jukumu la kununua vifaa na kujenga miundombinu ya kusambaza umeme na wanawajibika kuwalipa vibarua pamoja na gharama nyingine zinazohitajika katika utekelezaji wa miradi husika.

Madai ya Rushwa kwa Huduma ya Kuunganisha Umeme

Aidha kumekuwepo malalamiko ua rushwa kwa huduma mbalimbali za umeme Wakala unawahimiza wananchi kuwa malipo yote ya kuunganishiwa umeme yafanyike katika ofisi za TANESCO pekee na kwamba stakabadhi zitatolewa kwa malipo hayo. Wakala unawaagiza wananchi wajiepushe kulipa fedha kwa mtu yeyote atakayewadai rushwa au kutaka malipo yoyote ya kuunganishiwa umeme yafanyike nje ofisi za  TANESCO. Aidha, Wakala unawataka viongozi pamoja na wananchi katika maeneo ya miradi kukemea na kutoa taarifa za madai ya rushwa kutoka kwa wakandarasi wakubwa na wadogo pamoja na wafanyakazi au vibarua wao pindi yanapobainika kwenye ofisi za TANESCO, Polisi na Taasisi za Kuzuia na Kupambana Rushwa (TAKUKURU) na vyombo vingine vya dola. Aidha, Serikali itachukua hatua kali za kisheria kwa wakandarasi wakubwa na wadogo, wafanyakazi na vibarua wao pindi watakapobainika kujihusisha na vitendo vya rushwa.

Kwa taarifa hii, Wakala unawaonya wakandarasi wote kutokujihusisha na vitendo vya rushwa na kuhakikisha wanawadhibiti wakandarasi wadogo, wafanyakazi na vibarua wao kutokujihusisha na vitendo vya rushwa. Wakandarasi watakaoshindwa  kutekeleza agizo hili,  mikataba yao itasitishwa  na watanyimwa fursa ya kushiriki kwenye zabuni za miradi mingine ya kusambaza umeme vijijini.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S.L.P. 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Parua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top