Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Aodax K. Nshala 9220

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI: UTEKELEZAJI WA MIRADI YA KUSAMBAZA UMEME VIJIJINI

DAR ES SALAAM, 07 JANUARI 2016

Serikali kupitia Wakala na Mfuko wa Nishati Vijijini (REA/REF) inafadhili miradi ya kusambaza umeme vijijini katika mikoa yote ya Tanzania Bara. Miradi ya Awamu ya Pili ya Usambazaji Umeme Vijijini inatekelezwa na wakandarasi kutoka sekta binafsi ambao huhusika na ujenzi wa miundombinu ya usafirishaji na usambazaji umeme chini ya usimamizi wa TANESCO.

Malipo ya Huduma kwa Wakandarasi, Wakandarasi Wadogo na Vibarua

Kumekuwepo na malalamiko ya Kucheleweshwa kwa malipo ya wafanyakazi na vibarua pamoja na watoa huduma ambao wanashiriki katika ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme vijijini. Tunapenda kuwafahamisha wananchi kuwa katika utekelezaji wa miradi ya kusambaza umeme vijijini, Wakala umeingia mikataba na wakandarasi binafsi ambao wana jukumu la kununua vifaa na kujenga miundombinu ya kusambaza umeme na wanawajibika kuwalipa vibarua pamoja na gharama nyingine zinazohitajika katika utekelezaji wa miradi husika.

Madai ya Rushwa kwa Huduma ya Kuunganisha Umeme

Aidha kumekuwepo malalamiko ua rushwa kwa huduma mbalimbali za umeme Wakala unawahimiza wananchi kuwa malipo yote ya kuunganishiwa umeme yafanyike katika ofisi za TANESCO pekee na kwamba stakabadhi zitatolewa kwa malipo hayo. Wakala unawaagiza wananchi wajiepushe kulipa fedha kwa mtu yeyote atakayewadai rushwa au kutaka malipo yoyote ya kuunganishiwa umeme yafanyike nje ofisi za  TANESCO. Aidha, Wakala unawataka viongozi pamoja na wananchi katika maeneo ya miradi kukemea na kutoa taarifa za madai ya rushwa kutoka kwa wakandarasi wakubwa na wadogo pamoja na wafanyakazi au vibarua wao pindi yanapobainika kwenye ofisi za TANESCO, Polisi na Taasisi za Kuzuia na Kupambana Rushwa (TAKUKURU) na vyombo vingine vya dola. Aidha, Serikali itachukua hatua kali za kisheria kwa wakandarasi wakubwa na wadogo, wafanyakazi na vibarua wao pindi watakapobainika kujihusisha na vitendo vya rushwa.

Kwa taarifa hii, Wakala unawaonya wakandarasi wote kutokujihusisha na vitendo vya rushwa na kuhakikisha wanawadhibiti wakandarasi wadogo, wafanyakazi na vibarua wao kutokujihusisha na vitendo vya rushwa. Wakandarasi watakaoshindwa  kutekeleza agizo hili,  mikataba yao itasitishwa  na watanyimwa fursa ya kushiriki kwenye zabuni za miradi mingine ya kusambaza umeme vijijini.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Mawasiliano Towers, Ghorofa ya 2
Barabara ya Sam Nujoma
S.L.P. 7990
Dar es Salaam, Tanzania

Parua Pepe: info@rea.go.tz
Simu: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Nukushi: +255 22 2412007

Rate article

No rating
Rate this article:
No rating

Share

Print
«May 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
293012345
6789101112
13141516171819
20212223242526
272829303112
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top