Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia
Frank A. Mugogo 69

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti Machi 6, 2025 mara baada ya kutembelea Banda la REA na kushuhudia teknolojia mbalimbali za majiko ya Nishati Safi ya Kupikia; wananchi hao wamepongeza uwepo wa teknolojia hiyo ambayo wamesema licha ya kulinda mazingira lakini pia inarahisisha suala zima la kupika na hivyo kurahisisha maisha.

"Tumefurahi kuona majiko yaliyoboreshwa, teknolojia iliyotumika ni nzuri, majiko haya tumeyapenda," amesema Ester Mwasigo mkazi wa Dodoma ambaye yupo Jijini humo kushiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Kimataifa 2025.

Mwasigo alitoa wito kwa wananchi kutembea banda la REA ili kujifunza na kuchangamkia bidhaa hizo za Nishati Safi  ikiwa ni hatua moja wapo ya kuunga mkono jitihada na dhamira ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia.

"Tunatumia gharama kubwa kununua mkaa huu wa kawaida; mimi ni balozi wa teknolojia hii; Serikali imefanya jambo kubwa muhimu ni kuendelea kutoa elimu kwa wananchi kama hivi," amesema.

Akizungumzia kwa ujumla mwenendo wa kuhama kutoka kwenye utamaduni wa zamani kwenda kwenye utamaduni mpya wa Nishati Safi ya Kupikia, Mwajuma Tarek Mkazi wa Muriet Jijini Arusha alisema kwa kampeni inayoendelea kutolewa dhamira ya Serikali itafikiwa kikamilifu hasa ikizingatiwa kila mwanamke amehamasika.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«April 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
311234
CALL FOR PROPOSAL - Supply and Installation of Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions

CALL FOR PROPOSAL - Supply and Installation of Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions

The Rural Energy Agency issue the Second Call for applications from qualified suppliers to Supply and install Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions through on-call basis.

Read more
56
789
Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24

Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24

Please find the attached Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24:

Read more
10111213
14
Wabia wa Maendeleo Waahidi Kuendelea Kushirikiana na Serikali ya Tanzania Kuboresha Maisha ya Wananchi

Wabia wa Maendeleo Waahidi Kuendelea Kushirikiana na Serikali ya Tanzania Kuboresha Maisha ya Wananchi

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego amuopengeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kazi kubwa ya kufikisha umeme vijijini hali iliyobadili maisha ya wananchi vijijini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top