Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
BODI YA NISHATI VIJIJINI HAIJARIDHISHWA NA KAZI YA MKANDARASI MKOA WA SINGIDA
Admin.Frank Mugogo 4488

BODI YA NISHATI VIJIJINI HAIJARIDHISHWA NA KAZI YA MKANDARASI MKOA WA SINGIDA

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) haijaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mradi wa kusambaza umeme vijijini katika Wilaya ya Iramba na Mkalama mkoani Singida unayotekelezwa na Kampuni ya Emerc and Dynamic Engineering.

Mwenyekiti wa REB, Wakili Julius Kalolo alionesha wasiwasi huo kwa mkandarasi huyo kushindwa kukamilisha kazi hiyo wakati Bodi yake ilipofanya ziara ya siku mbili, tarehe 26 hadi 27 Agosti 2020 ya kukagua utekelezaji wa mradi wa kusambaza umeme vijijini katika wilaya za SingidaVijijini, Iramba na Mkalama.

“Tumeona kwa kiasi fulani ametimiza maukumu yake, lakini bado yupo chini ya matarajio kwa sababu maeneo mengi hayajajengwa miundombinu ya umeme mkubwa, hata miundombinu ya umeme mdogo kwa ajili ya kuingiza majumbani hajakamilika” alisema.

Kutokana na kusuasua kwa mkandarasi huyo, Bodi ilimuagiza aongeze magenge ya kazi ili aweze kukamilisha mradi huo ifikapo tarehe 10/09/2020. Hata hivyo, Wakili Kalolo alisema mkandarasi amepewa siku tatu kuanzia tarehe 28 hadi 30 Agosti, 2020 ambapo kama hatajirekebisha kwa kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi, atapunguziwa wigo wa mradi wake ili kazi hiyo ikamilike kwa wakati uliopangwa.

“Atakuwa katika uangalizi wa siku tatu kama hataonesha mabadiliko atapunguziwa kazi ili asicheleweshe wananchi kupata huduma ya nishati ya umeme” alisema Wakili Kalolo.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Jones Olotu amemtaka mkandarasi kuzingatia maelekezo aliyopewa na Bodi na kutahadharisha kuwa ndani ya siku tatu kama hataonesha mabadiliko ya utendaji wake wa kazi atapunguziwa baadhi ya maeneo.

“Tumempa tahadhari baada ya siku tatu baadhi ya maeneo ambayo atakuwa hajaanza kazi TANESCO wataingia na mafundi wao kukamilisha ili wananchi waweze kuwashiwa umeme,” alisema.

Mhandisi Olotu alimuagiza mkandarasi kutumia nguvu kazi ya vijana wa vijiji ambavyo viko katika wigo wa mradi katika kazi ambazo hazihitaji utaalamu kama vile kufyeka vichaka, kuchimba mashimo na kubeba nguzo.

Akizungumza kwa niaba ya mkandarasi, Mhandisi anayesimamia mradi huo, James Kinyila alisema kuwa wamepanga magenge ya kutosha ili kukamilisha kazi hiyo kwa muda waliopewa.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz

Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Rate article

No rating
Rate this article:
No rating

Share

Print
«April 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
25
Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa  Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za  Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini unakaribisha maombi ya mkopo nafuu kuwezesha ujenzi wa vituo vidogo vya kuuzia bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) vijijini. Mkopo huu utasaidia uwezeshaji wa ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini ili kuhakikisha upatikanaji wa nishati ya mafuta kwa gharama nafuu, kwa njia salama, na isiyo na madhara kwa mazingira.

Wakala unawasisitiza waombaji walioomba katika awamu ya kwanza na kutokidhi vigezo kuomba tena baada ya kufanya marekebisho  ya  mapungufu yaliyobainishwa katika maombi yao. Aidha maombi mapya ya mkopo yanakaribishwa.

Read more
262728293031
12345
Call for Proposals for Results Based Financing (RBF) Application for Stand Alone Solar Home System (SA-SHS)

Call for Proposals for Results Based Financing (RBF) Application for Stand Alone Solar Home System (SA-SHS)

The Rural Energy Agency (REA) invites eligible firms to apply for grant per new SA-SHS installation in targeted rural communities. The grant includes end-user buying price system subsidization and firm’s performance incentive. The SA-SHS grant application is implemented through the program for Tanzania Rural Electrification Expansion Program Additional Financing (TREEP AF) which is supported by the World Bank.

Read more
67
891011121314
15
Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA

Wabia wa Maendeleo Waipongeza REA


Wabia wa Maendeleo ambao wanafadhili miradi ya kusambaza nishati vijijini wamepongeza Wakala wa Nishati Vijijini kwa utekelezaji wa miradi ya kusambaza nishati vijijini ambayo inaleta tija kwa ustawi wa wananchi.

Read more
161718192021
222324
Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25

Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25

Hotuba ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mheshimiwa Dkt. Doto Mashaka Biteko (Mb), Akiwasilisha Bungeni Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati kwa Mwaka 2024/25.

Read more
25262728
293012345

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top