Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
BODI YA NISHATI VIJIJINI HAIJARIDHISHWA NA KAZI YA MKANDARASI MKOA WA SINGIDA
Admin.Frank Mugogo 4542

BODI YA NISHATI VIJIJINI HAIJARIDHISHWA NA KAZI YA MKANDARASI MKOA WA SINGIDA

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) haijaridhishwa na kasi ya utekelezaji wa mradi wa kusambaza umeme vijijini katika Wilaya ya Iramba na Mkalama mkoani Singida unayotekelezwa na Kampuni ya Emerc and Dynamic Engineering.

Mwenyekiti wa REB, Wakili Julius Kalolo alionesha wasiwasi huo kwa mkandarasi huyo kushindwa kukamilisha kazi hiyo wakati Bodi yake ilipofanya ziara ya siku mbili, tarehe 26 hadi 27 Agosti 2020 ya kukagua utekelezaji wa mradi wa kusambaza umeme vijijini katika wilaya za SingidaVijijini, Iramba na Mkalama.

“Tumeona kwa kiasi fulani ametimiza maukumu yake, lakini bado yupo chini ya matarajio kwa sababu maeneo mengi hayajajengwa miundombinu ya umeme mkubwa, hata miundombinu ya umeme mdogo kwa ajili ya kuingiza majumbani hajakamilika” alisema.

Kutokana na kusuasua kwa mkandarasi huyo, Bodi ilimuagiza aongeze magenge ya kazi ili aweze kukamilisha mradi huo ifikapo tarehe 10/09/2020. Hata hivyo, Wakili Kalolo alisema mkandarasi amepewa siku tatu kuanzia tarehe 28 hadi 30 Agosti, 2020 ambapo kama hatajirekebisha kwa kuongeza kasi ya utekelezaji wa mradi, atapunguziwa wigo wa mradi wake ili kazi hiyo ikamilike kwa wakati uliopangwa.

“Atakuwa katika uangalizi wa siku tatu kama hataonesha mabadiliko atapunguziwa kazi ili asicheleweshe wananchi kupata huduma ya nishati ya umeme” alisema Wakili Kalolo.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi wa Huduma za Ufundi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Jones Olotu amemtaka mkandarasi kuzingatia maelekezo aliyopewa na Bodi na kutahadharisha kuwa ndani ya siku tatu kama hataonesha mabadiliko ya utendaji wake wa kazi atapunguziwa baadhi ya maeneo.

“Tumempa tahadhari baada ya siku tatu baadhi ya maeneo ambayo atakuwa hajaanza kazi TANESCO wataingia na mafundi wao kukamilisha ili wananchi waweze kuwashiwa umeme,” alisema.

Mhandisi Olotu alimuagiza mkandarasi kutumia nguvu kazi ya vijana wa vijiji ambavyo viko katika wigo wa mradi katika kazi ambazo hazihitaji utaalamu kama vile kufyeka vichaka, kuchimba mashimo na kubeba nguzo.

Akizungumza kwa niaba ya mkandarasi, Mhandisi anayesimamia mradi huo, James Kinyila alisema kuwa wamepanga magenge ya kutosha ili kukamilisha kazi hiyo kwa muda waliopewa.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz

Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top