Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
SUMA JKT WAPONGEZWA KWA KUJENGA MIUNDOMBINU YA KUSAMBAZA UMEME
Admin.Frank Mugogo 4054

SUMA JKT WAPONGEZWA KWA KUJENGA MIUNDOMBINU YA KUSAMBAZA UMEME

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Wakili Julius Kalolo amekipongeza kikosi cha Suma JKT ambacho kimepewa kazi kujenga miundombinu ya kusambaza umeme katika kata ya Kwa Mtoro na Farkwa na ameonesha nia ya kufanya nao kazi katika miradi mingine inayotekelezwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Wakili Kalolo alitoa pongezi hizo tarehe 25/08/2020 wakati Bodi yake ilipofanya ziara ya siku moja kukagua ujenzi wa Miundombinu ya umeme katika kata ya Farkwa ambapo kikosi kutoka Suma JKT kilikuwa kinaendelea kujenga miundombinu ya kusambaza umeme.

“Ni muda mfupi lakini mmefanya kazi nzuri ambayo inaleta matumaini kwetu tuendelee kushirikiana na kuwe na mawasiliano ya karibu. Kukiwa na jambo lolote gumu msisite kusema ili lipatiwe ufumbuzi haraka. Tunawashukuru na tumeona mnaweza kufanya kazi hizi za miradi ya kusambaza umeme vijijini, hivyo kwenu ni fursa tunapotangaza zabuni na nyie muombe ili muweze kushindanishwa,” alisema Wakili Kalolo.

Aidha, Wakili Kalolo aliwataka Suma JKT waongeze idadi ya watu ili waweze kukamilisha kazi hiyo kwa muda mfupi wananchi waweze kunufaika na umeme.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Amos Maganga alisisitiza kwa kusema “kama Mwenyekiti alivyosema sasa Suma JKT wameingia katika industry ya umeme, pamoja na kuwa hii kazi ni ya dharura tumepata kipimo cha kuweza kuwaona kwamba tunaweza kufanya nao kazi. Tutaendelea kushirikiana nao”.

Naye Kapteni James Mhame, anayesimamia kikosi hicho cha Suma JKT, alisema kuwa wamedhamiria kukamilisha kazi hiyo yenye urefu wa kilomita 14 ya ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme kwa muda waliopewa.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz

Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top