Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
SUMA JKT WAPONGEZWA KWA KUJENGA MIUNDOMBINU YA KUSAMBAZA UMEME
Admin.Frank Mugogo 4441

SUMA JKT WAPONGEZWA KWA KUJENGA MIUNDOMBINU YA KUSAMBAZA UMEME

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Wakili Julius Kalolo amekipongeza kikosi cha Suma JKT ambacho kimepewa kazi kujenga miundombinu ya kusambaza umeme katika kata ya Kwa Mtoro na Farkwa na ameonesha nia ya kufanya nao kazi katika miradi mingine inayotekelezwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Wakili Kalolo alitoa pongezi hizo tarehe 25/08/2020 wakati Bodi yake ilipofanya ziara ya siku moja kukagua ujenzi wa Miundombinu ya umeme katika kata ya Farkwa ambapo kikosi kutoka Suma JKT kilikuwa kinaendelea kujenga miundombinu ya kusambaza umeme.

“Ni muda mfupi lakini mmefanya kazi nzuri ambayo inaleta matumaini kwetu tuendelee kushirikiana na kuwe na mawasiliano ya karibu. Kukiwa na jambo lolote gumu msisite kusema ili lipatiwe ufumbuzi haraka. Tunawashukuru na tumeona mnaweza kufanya kazi hizi za miradi ya kusambaza umeme vijijini, hivyo kwenu ni fursa tunapotangaza zabuni na nyie muombe ili muweze kushindanishwa,” alisema Wakili Kalolo.

Aidha, Wakili Kalolo aliwataka Suma JKT waongeze idadi ya watu ili waweze kukamilisha kazi hiyo kwa muda mfupi wananchi waweze kunufaika na umeme.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Amos Maganga alisisitiza kwa kusema “kama Mwenyekiti alivyosema sasa Suma JKT wameingia katika industry ya umeme, pamoja na kuwa hii kazi ni ya dharura tumepata kipimo cha kuweza kuwaona kwamba tunaweza kufanya nao kazi. Tutaendelea kushirikiana nao”.

Naye Kapteni James Mhame, anayesimamia kikosi hicho cha Suma JKT, alisema kuwa wamedhamiria kukamilisha kazi hiyo yenye urefu wa kilomita 14 ya ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme kwa muda waliopewa.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz

Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«August 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
272829303112
3456789
1011121314
REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

REA Yaeleza Utekelezaji Wa Mkakati Wa Nishati Safi Kwenye Tamasha La Kizimkazi Mwaka 2026

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umefanikiwa kusambaza takribani mitungi laki saba ya gesi ya kupikia (LPG) nchini kote, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa kasi wa Mkakati wa Kitaifa wa Nishati Safi ya Kupikia.

Read more
1516
1718

Maombi ya Mkopo Nafuu wa Uwezeshaji wa Ujenzi na Uendeshaji wa Vituo Vidogo vya Bidhaa za Mafuta (Petroli na Dizeli) Vijijini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unakaribisha waombaji wenye vigezo kuomba mkopo wa kuwezesha ujenzi wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petroli na dizeli) ili kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu maeneo ya vijijini.

Pamoja na tangazo hili, tumeweka viambatanisho vifuatavyo:
•    Tangazo la fursa ya mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta ya Petroli na Dizeli vijijini.
•    Mwongozo wa utoaji mkopo wa ujenzi wa vituo vidogo vya mafuta vijijini.
•    Fomu ya Maombi ya Mkopo.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la REA
Mtaa wa Medeli
P. O. Box 2153,
DODOMA, TANZANIA.

Read more
1920212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top