Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
SUMA JKT WAPONGEZWA KWA KUJENGA MIUNDOMBINU YA KUSAMBAZA UMEME
Admin.Frank Mugogo 4085

SUMA JKT WAPONGEZWA KWA KUJENGA MIUNDOMBINU YA KUSAMBAZA UMEME

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Wakili Julius Kalolo amekipongeza kikosi cha Suma JKT ambacho kimepewa kazi kujenga miundombinu ya kusambaza umeme katika kata ya Kwa Mtoro na Farkwa na ameonesha nia ya kufanya nao kazi katika miradi mingine inayotekelezwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Wakili Kalolo alitoa pongezi hizo tarehe 25/08/2020 wakati Bodi yake ilipofanya ziara ya siku moja kukagua ujenzi wa Miundombinu ya umeme katika kata ya Farkwa ambapo kikosi kutoka Suma JKT kilikuwa kinaendelea kujenga miundombinu ya kusambaza umeme.

“Ni muda mfupi lakini mmefanya kazi nzuri ambayo inaleta matumaini kwetu tuendelee kushirikiana na kuwe na mawasiliano ya karibu. Kukiwa na jambo lolote gumu msisite kusema ili lipatiwe ufumbuzi haraka. Tunawashukuru na tumeona mnaweza kufanya kazi hizi za miradi ya kusambaza umeme vijijini, hivyo kwenu ni fursa tunapotangaza zabuni na nyie muombe ili muweze kushindanishwa,” alisema Wakili Kalolo.

Aidha, Wakili Kalolo aliwataka Suma JKT waongeze idadi ya watu ili waweze kukamilisha kazi hiyo kwa muda mfupi wananchi waweze kunufaika na umeme.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Amos Maganga alisisitiza kwa kusema “kama Mwenyekiti alivyosema sasa Suma JKT wameingia katika industry ya umeme, pamoja na kuwa hii kazi ni ya dharura tumepata kipimo cha kuweza kuwaona kwamba tunaweza kufanya nao kazi. Tutaendelea kushirikiana nao”.

Naye Kapteni James Mhame, anayesimamia kikosi hicho cha Suma JKT, alisema kuwa wamedhamiria kukamilisha kazi hiyo yenye urefu wa kilomita 14 ya ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme kwa muda waliopewa.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz

Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«August 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
28293031123
45
Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

Call for Proposal for Deployment of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in Remote Villages in Geita, Ludewa and Mbulu Districts

The Rural Energy Agency (REA) is seeking proposals from qualified service providers for the supply, installation, and testing of Stand-Alone Solar Home Systems (SA-SHS) in eight remote villages across Geita, Ludewa and Mbulu districts. Those villages are located in remote areas with challenging geographical conditions, hence, impractical for grid extension.

Please find the attached documents:

•    Application Form for Supply and Installation of SA-SHS; and
•    Call for Proposals for Result Based Financing Installation of Stand Alone Solar Home Systems.

Read more
678910
111213
Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Kaya 3,255 kunufaika na majiko ya gesi ya ruzuku Wilaya ya Mlele

Wananchi Kijiji cha Usevya Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi wamepongeza hatua zinazochukuliwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) katika kuhakikisha wanafikiwa na nishati safi ya kupikia kwa bei ya ruzuku.

Read more
1415
Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Viongozi wa Dini Mabalozi Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umetoa wito kwa viongozi wa dini nchini kushiriki kikamilifu katika kampeni ya kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa lengo la kulinda afya na kuokoa mazingira.

Read more
1617
181920
Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Nishati Safi ya Kupikia Suluhu ya Mabadiliko ya Tabia Nchi

Watanzania wameendelea kuhamasishwa kutumia nishati safi ya kupikia ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Read more
21222324
25262728293031
1234567

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top