Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
SUMA JKT WAPONGEZWA KWA KUJENGA MIUNDOMBINU YA KUSAMBAZA UMEME
Admin.Frank Mugogo 4050

SUMA JKT WAPONGEZWA KWA KUJENGA MIUNDOMBINU YA KUSAMBAZA UMEME

Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Wakili Julius Kalolo amekipongeza kikosi cha Suma JKT ambacho kimepewa kazi kujenga miundombinu ya kusambaza umeme katika kata ya Kwa Mtoro na Farkwa na ameonesha nia ya kufanya nao kazi katika miradi mingine inayotekelezwa na Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Wakili Kalolo alitoa pongezi hizo tarehe 25/08/2020 wakati Bodi yake ilipofanya ziara ya siku moja kukagua ujenzi wa Miundombinu ya umeme katika kata ya Farkwa ambapo kikosi kutoka Suma JKT kilikuwa kinaendelea kujenga miundombinu ya kusambaza umeme.

“Ni muda mfupi lakini mmefanya kazi nzuri ambayo inaleta matumaini kwetu tuendelee kushirikiana na kuwe na mawasiliano ya karibu. Kukiwa na jambo lolote gumu msisite kusema ili lipatiwe ufumbuzi haraka. Tunawashukuru na tumeona mnaweza kufanya kazi hizi za miradi ya kusambaza umeme vijijini, hivyo kwenu ni fursa tunapotangaza zabuni na nyie muombe ili muweze kushindanishwa,” alisema Wakili Kalolo.

Aidha, Wakili Kalolo aliwataka Suma JKT waongeze idadi ya watu ili waweze kukamilisha kazi hiyo kwa muda mfupi wananchi waweze kunufaika na umeme.

Aidha, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Amos Maganga alisisitiza kwa kusema “kama Mwenyekiti alivyosema sasa Suma JKT wameingia katika industry ya umeme, pamoja na kuwa hii kazi ni ya dharura tumepata kipimo cha kuweza kuwaona kwamba tunaweza kufanya nao kazi. Tutaendelea kushirikiana nao”.

Naye Kapteni James Mhame, anayesimamia kikosi hicho cha Suma JKT, alisema kuwa wamedhamiria kukamilisha kazi hiyo yenye urefu wa kilomita 14 ya ujenzi wa miundombinu ya kusambaza umeme kwa muda waliopewa.

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini (REA)
Jengo la PSSSF, Ghorofa ya 7
Barabara ya Makole
S. L. P 2153
Dodoma, Tanzania
Barua pepe: info@rea.go.tz

Simu: +255 262323504, +255 262323506, +255 262323507

Share

Print
«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top