Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Dkt. Biteko Azindua Jengo la Ofisi za REA
Frank A. Mugogo 14

Dkt. Biteko Azindua Jengo la Ofisi za REA

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kukamilisha ujenzi wa jengo la kisasa la Ofisi zake Jijini Dodoma.

Ametoa pongezi hizo baada ya kuzindua Jengo hilo Septemba 13, 2024 Jijini Dodoma katika hafla iliyohudhuriwa na viongozi wa Serikali na wananchi wa maeneo ya jirani. 

Dkt.Biteko amesema Jengo hilo litawawezesha watumishi kutoa huduma kwa wananchi na kuwapongeza REA kwa kujenga jengo hilo la kisasa lenye ghorofa tano kwa gharama ya shilingi bilioni 9.8 kwa miezi 18 badala ya shilingi bilioni 13 zilizopangwa awali.

Pamoja na pongezi hizo, Dkt. Biteko amewakumbusha kuhakikisha uwepo wa jengo hilo unakwenda sambamba na utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko ameagiza Watendaji wa Wizara ya Nishati kuhakikisha kuwa majengo ya Wizara ya Nishati na Taasisi zake yanafungwa mfumo wa umeme jua ikiwa ni kuonesha kwa vitendo matumizi ya nishati safi yenye gharama nafuu.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy alisema kuhamia katika jengo hilo kumeiwezesha REA kuokoa kiasi cha shilingi milioni 650 zilizokuwa zikitumika kwa mwaka kulipia kodi ya pango ambazo sasa zinaelekezwa kwenye maendeleo. 


Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«September 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
26
REA yamtaka mwendelezaji wa mradi wa kufua umeme wa Maguta mkoani Iringa kuongeza kasi

REA yamtaka mwendelezaji wa mradi wa kufua umeme wa Maguta mkoani Iringa kuongeza kasi

Serikali imemtaka Mwendelezaji wa Mradi wa kufua umeme kwa kutumia maporomoko ya maji wa Maguta  uliopo katika Kijiji cha Masisiwe Wilayani Kilolo Mkoani Iringa kuukamilisha kwa wakati.

Read more
27
Wananchi waaswa kutunza mazingira

Wananchi waaswa kutunza mazingira

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewaasa wananchi kutunza mazingira na kulinda miundombinu pamoja na vyanzo vya maji ili kuendelea kupata huduma ya umeme pamoja na kuwa na miradi endelevu ya kufua umeme.

Read more
282930311
2345678
9101112
EXTENDED DEADLINE FOR INVITATION FOR PROPOSALS - Supply of Starter Packs of LPG for Prison Staffs in Areas of Rural Mainland Tanzania

EXTENDED DEADLINE FOR INVITATION FOR PROPOSALS - Supply of Starter Packs of LPG for Prison Staffs in Areas of Rural Mainland Tanzania

The Government of Tanzania through the Rural Energy Agency (REA) in collaboration with Tanzania Prisons Services (TPS) in response to attainment of sustainable development goals, has opened a   financing   window to support distribution of 15,920 units of 15kg LPG Starter Packs to earmarked Staffs in all Tanzania Prisons. This is part of the Clean Cooking Packages that the parties have agreed to cooperate inorder to enable these institutions to stop using environmentally and healthily harmful cooking solutions.

Read more
131415
16171819202122
23242526272829
30123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top