Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Zaidi ya Bilioni 14 Kutekeleza Mradi wa Umeme Vitongojini Kagera
Frank A. Mugogo 101

Zaidi ya Bilioni 14 Kutekeleza Mradi wa Umeme Vitongojini Kagera

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Fatma Mwassa amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa zaidi ya Bilioni 14 kwa ajili ya kutekeleza Mradi wa  Umeme kwenye vitongoji 135 Mkoani humo katika majimbo yote.

Ametoa shukrani hizo Septemba 18, 2024 alipotembelea kitongoji cha Bushweka kijiji cha Mulahya Kata ya Katerero, kuzungumza na wananchi kwa niaba ya wakazi wa Mkoa wa Kagera akiwa pia ameambatana na ujumbe wa Wakala Wa Nishati Vijijini (REA) pamoja na CCC International Nigeria Engineering Ltd Ambaye Ndie Mkandarasi wa mradi huo. 

Mhe. Fatma Mwassa amewasihi na kuwaasa wananchi wa Mkoa wa Kagera kutoa ushirikiano wa kutosha kwa mkandarasi ili aweze kukamilisha utekelezaji wa mradi ndani ya wakati na kwa viwango vinavyokubalika.

Vilevile Mhe. Mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa wakala  kumsimamia Mkandarasi vema ili akamilishe mradi kwa wakati na  kwa viwango kama mkataba unavyomtaka ili kwa haraka huduma za umeme ziweze kuwafikia wananchi. 
 
Mhe. Fatma Mwassa amesema Mhe. Rais anaendelea kuboresha maisha ya wananchi wake kwa kasi ndio maana amemaliza kupeleka huduma za umeme kwenye vijiji vyote nchini na sasa anaelekeza nguvu kwenye vitongoji kwa kuhakikisha wanapata nishati safi.

Awali, Msimamizi wa miradi ya Wakala wa Nishati vijijini (REA) Kanda ya ziwa  Mhandisi Ernest Makale amesema mradi huo kwenye vitongoji unadhihirisha na kubainisha nia ya serikali ya kuhakikisha kila  kitongoji nchini kinakua na umeme ifikapo  2030.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«April 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
311234
CALL FOR PROPOSAL - Supply and Installation of Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions

CALL FOR PROPOSAL - Supply and Installation of Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions

The Rural Energy Agency issue the Second Call for applications from qualified suppliers to Supply and install Clean Cooking Solutions to Households, Public and Private Institutions through on-call basis.

Read more
56
789
Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24

Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24

Please find the attached Sector Performance Reports for Financial Year 2023-24:

Read more
10111213
14
Wabia wa Maendeleo Waahidi Kuendelea Kushirikiana na Serikali ya Tanzania Kuboresha Maisha ya Wananchi

Wabia wa Maendeleo Waahidi Kuendelea Kushirikiana na Serikali ya Tanzania Kuboresha Maisha ya Wananchi

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendego amuopengeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kazi kubwa ya kufikisha umeme vijijini hali iliyobadili maisha ya wananchi vijijini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top