Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Zaidi ya Bilioni 14 Kutekeleza Mradi wa Umeme Vitongojini Kagera
Frank A. Mugogo 84

Zaidi ya Bilioni 14 Kutekeleza Mradi wa Umeme Vitongojini Kagera

Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Fatma Mwassa amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutoa zaidi ya Bilioni 14 kwa ajili ya kutekeleza Mradi wa  Umeme kwenye vitongoji 135 Mkoani humo katika majimbo yote.

Ametoa shukrani hizo Septemba 18, 2024 alipotembelea kitongoji cha Bushweka kijiji cha Mulahya Kata ya Katerero, kuzungumza na wananchi kwa niaba ya wakazi wa Mkoa wa Kagera akiwa pia ameambatana na ujumbe wa Wakala Wa Nishati Vijijini (REA) pamoja na CCC International Nigeria Engineering Ltd Ambaye Ndie Mkandarasi wa mradi huo. 

Mhe. Fatma Mwassa amewasihi na kuwaasa wananchi wa Mkoa wa Kagera kutoa ushirikiano wa kutosha kwa mkandarasi ili aweze kukamilisha utekelezaji wa mradi ndani ya wakati na kwa viwango vinavyokubalika.

Vilevile Mhe. Mkuu wa Mkoa ametoa wito kwa wakala  kumsimamia Mkandarasi vema ili akamilishe mradi kwa wakati na  kwa viwango kama mkataba unavyomtaka ili kwa haraka huduma za umeme ziweze kuwafikia wananchi. 
 
Mhe. Fatma Mwassa amesema Mhe. Rais anaendelea kuboresha maisha ya wananchi wake kwa kasi ndio maana amemaliza kupeleka huduma za umeme kwenye vijiji vyote nchini na sasa anaelekeza nguvu kwenye vitongoji kwa kuhakikisha wanapata nishati safi.

Awali, Msimamizi wa miradi ya Wakala wa Nishati vijijini (REA) Kanda ya ziwa  Mhandisi Ernest Makale amesema mradi huo kwenye vitongoji unadhihirisha na kubainisha nia ya serikali ya kuhakikisha kila  kitongoji nchini kinakua na umeme ifikapo  2030.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«February 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
27
Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Mkutano wa Nishati Afrika (M300) Kuchochea Maendeleo ya Afrika

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa Nchi za Afrika - Misheni 300 ni kichocheo cha maendeleo ya nchi za Afrika na kichocheo cha utekelezaji wa Sera yake ya Taifa ya Nishati inayolenga kuendeleza nishati endelevu, uhifadhi na ufanisi.

Read more
2829303112
3456789
1011121314
REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

REA Yaanza Kusambaza Mitungi ya Gesi 13,020 Mkoani Songwe

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na kampuni ya Oryx Gas Tanzania, tarehe 12 Februari, 2025 imeanza rasmi kusambaza mitungi ya gesi ya kilo 6 kwa wakazi wa mkoa wa Songwe na kwa kuanzia Wananchi wa wilaya ya Mbozi wameanza kununua mitungi hiyo kwa nusu bei.

Read more
1516
17181920212223
242526272812
3456789

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top