Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Kituo cha Kupoza Umeme Mtera Kuboresha Upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma
Mohamed Saif 133

Kituo cha Kupoza Umeme Mtera Kuboresha Upatikanaji wa Umeme Iringa na Dodoma

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imezindua Kituo cha Kupoza na Kusambaza Umeme cha Mtera (2x10MVA, 220/33kV) ambacho kitaongeza ubora wa umeme, kupunguza changamoto ya umeme mdogo na kuboresha huduma za kijamii, afya, elimu, maji na mawasiliano.

Akizungumza katika hafla hiyo Januari 16, 2026 mkoani Iringa, Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amesema upanuzi wa kituo cha Mtera ni sehemu ya jitihada za Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuhakikisha nishati ya umeme inapatikana kwa uhakika na kwa gharama nafuu kwa wananchi katika maeneo ya vijijini. 

Halikadhalika ameongeza kuwa, mradi huo utawanufaisha wananchi wa wilaya za Mpwapwa na Kongwa mkoani Dodoma, pamoja na wilaya ya Kilolo mkoani Iringa, kwa kuboresha shughuli za kiuchumi na kijamii.

"Umeme upo wa kutosha, niwaombe wananchi wajitokeze kuunganishiwa umeme ili waweze kunufaika na fursa za kiuchumi zinazotokana na upatikanaji wa nishati ya uhakika,” amesema Mhe. Ndejembi

Naye, Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Felchesmi Mramba, amesema REA imeleta mapinduzi makubwa katika kufikisha umeme vijijini, akibainisha kuwa mwaka 2014 ni asilimia 7 pekee ya wananchi wa vijijini waliokuwa na umeme, huku mwaka 2026 kiwango hicho kimefikia asilimia 78.

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Simon Lusengekile, amepongeza mikakati ya Serikali kupitia REA katika kuwahudumia wananchi kupitia miradi ya nishati, huku akiwataka wananchi kulinda miundombinu ya umeme ili iweze kudumu kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho. 

Aidha, Mwakilishi wa Wabia  wa Maendeleo ambao ni Norway na Sweden, Stephen Mwakifwamba, ambao wamechangia gharama za ujenzi wa Kituo  cha Kupoza Umeme cha Mtera amesema kuwa wamefurahishwa na mafanikio ya utekeleza wa mradi ambao umeanza kuwanufaisha wananchi wa mikoa ya Iringa na Dodoma.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB), Meja Jenerali Mstaafu Mhe. Balozi Jacob Kingu, ameipongeza Menejimenti na watendaji wa REA kwa kukamilisha mradi huo kwa mafanikio, akisisitiza kuwa wakala una mchango mkubwa katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo ya nishati nchini.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy, amebainisha kuwa Kituo cha Mtera kimejengwa kwa gharama ya shilingi bilioni 9.2 na Serikali ya Tanzania kupitia REA kwa ushirikiano na Serikali za Sweden na Norway.

Akizungumza kwa niaba ya Wakuu wa Mikoa ya Dodoma na Iringa, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Mhe. Rosemary Senyamule, amesema mradi huo utawanufaisha kwa kiasi kikubwa wananchi wa mikoa hiyo, huku akiipongeza REA kwa kazi kubwa ya kufikisha umeme vijijini.

Amesema licha ya kuwepo kwa umeme wa kutosha, matumizi ya sayansi na teknolojia ni muhimu katika kuhakikisha umeme haukatiki mara kwa mara, akiongeza kuwa miradi kama hiyo inaonesha mchango wa sayansi katika kupunguza changamoto za umeme.

Aidha, amewahimiza wananchi wa wilaya za Kongwa na Mpwapwa kutumia fursa ya umeme wa uhakika kuongeza uzalishaji wa viwandani na kuboresha uchumi wa Mkoa wa Dodoma kwa ujumla.

 

Share

Print
«March 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
2324252627281
2345678
9101112131415
16171819
Wananchi Wanayo Matumaini Makubwa na REA – Mhandisi Saidy

Wananchi Wanayo Matumaini Makubwa na REA – Mhandisi Saidy

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi, Hassan Saidy amesema Wananchi hususan wanaoishi vijijini wana matumaini na Serikali kupitia REA katika kuwaboreshea hali ya maisha na amewataka Watumishi wa Wakala kuhakikisha wanafanya kazi kwa bidii, uadilifu na maarifa ili kutimiza malengo ya Serikali kuhudumia wananchi wake.

Read more
202122
23
REA Imebeba Ajenda Ya Maendeleo Ya Watu Wa Vijijini– Mwenyekiti Kamati Ya Bunge Ya Nishati Na Madini

REA Imebeba Ajenda Ya Maendeleo Ya Watu Wa Vijijini– Mwenyekiti Kamati Ya Bunge Ya Nishati Na Madini

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. Subira Mgalu, amesema Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya kusambaza umeme ili kuhakikisha wananchi wanaoishi pembezoni mwa miji na vijijini wanapata huduma hiyo muhimu kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Read more
242526272829
303112345

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top