TAARIFA KWA WAKANDARASI / NOTICE TO CONTRACTORS
MIRADI YA KUSAMBAZA UMEME VIJIJINI / RURAL ELECTRIFICATION PROJECTS
KISWAHILI
Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unatambua kuwa baadhi ya wakandarasi wanaotekeleza miradi ya kusambaza umeme vijijini hawajakamilisha miradi kwa mujibu wa MIKATABA waliyosaini na Wakala (REA). Aidha, kuna baadhi ya wakandarasi wamekamilisha miradi lakini hawajakabidhi rasmi miradi hiyo na vifaa au hawajafanya marekebisho kasoro zilizobainishwa na wasimamizi wa miradi kutoka (TANESCO na REA).
Kwa tangazo hili, Wakala unawataarifu wakandarasi wote ambao hawajakamilisha matakwa hayo ya kimikataba kufanya hivyo mara moja. Wakandarasi watakaoshindwa kutimiza masharti hayo hawataruhusiwa kushiriki katika zabuni zitakazotangazwa na Wakala (REA) baada ya TANGAZO hili na hatua nyingine zitachukuliwa juu yao kwa mujibu wa mikataba hiyo.
ENGLISH
The Rural Energy Agency (REA) has noted that some of the contractors engaged in the rural electrification projects have not completed their projects and handed over materials to TANESCO respective regions accordingly. The contractors have not also finalised rectification of snags as instructed by REA and TANESCO supervisors.
In view of the above, REA hereby informs all contractors who have not fulfilled the above obligations to do so immediately. All contractors who have not fulfilled these obligations WILL NOT BE ALLOWED TO PARTICIPATE in the forthcoming TENDERS to be advertised by the Agency.
Director General
Rural Energy Agency (REA)
Mawasiliano Towers, 2nd Floor
Sam Nujoma Road, 14414
P. O. Box 7990
Dar es Salaam, Tanzania
E-Mail: info@rea.go.tz
Tel: +255 22 2412001, +255 22 2412002, +255 22 2412003
Fax: +255 22 2412007