Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Majiko Banifu Teknolojia ya Kisasa Inayotumia Mkaa Kidogo
Frank A. Mugogo 220

Majiko Banifu Teknolojia ya Kisasa Inayotumia Mkaa Kidogo

Imeelezwa kuwa majiko banifu yanayotolewa kwa bei ya ruzuku na Wakala wa Nishati Vijijini (REA), ni majiko yanayotumia kiasi kidogo cha mkaa kulinganisha na majiko mengine ya mkaa. 
 
Hayo yamebainishwa na Wataalam kutoka REA wanaoendelea kutoa elimu kwa wananchi katika Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan mkoani Geita. 
 
Aidha, majiko banifu yametengenezwa kwa teknolojia ya kisasa yenye uwezo wa kupunguza sumu ya mkaa (carbon monoxide) hivyo inasaidia kupunguza madhara ya kiafya yatokanayo na nishati ya mkaa. 
 
Halikadhalika, majiko banifu yanasaidia utunzaji wa mazingira, ni rahisi kwa matumizi yanadumu kwa muda mrefu bila kupata changamoto ya kuharibika kwa watumiaji. 
 
Katika mkoa wa Geita kampuni inayosambaza majiko banifu kwa bei ya ruzuku ni Geita Millenium Star Company Limited.
 
Majiko banifu yanatolewa kwa bei ya ruzuku ya shilingi 6,195 kwa kuwa Serikali imeweka ruzuku ya bei katika majiko hayo ili wananchi waweze kuyatumia na kuyapata kwa urahisi ambapo kabla ya ruzuku yalikuwa yanauzwa kwa shilingi 41,300.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«November 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
272829303112
3456789
10111213141516
17181920212223
24252627282930
1234567

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top