Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA Yasambaza Majiko na Mitungi ya Gesi Kilo 15 Kwa Jeshi la Magereza Mkoani Shinyanga
Frank A. Mugogo 424

REA Yasambaza Majiko na Mitungi ya Gesi Kilo 15 Kwa Jeshi la Magereza Mkoani Shinyanga

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) tarehe 24 Septemba, 2025 imesambaza kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza 221 mkoa wa Shinyanga majiko ya gesi ya sahani (2) na mitungi ya kilo 15 kwa ajili ya Maafisa na Watumishi wa Jeshi hilo huku wito ukitolewa wa kuwataka wawe mabalozi wa nishati safi kwa mkoa huo.

Katika hafla hiyo ya ugawaji wa majiko na mitungi ya gesi, Mjumbe wa Bodi ya Nishati Vijijini (REB); Mhandisi, Ahmed Chinemba ametoa wito kwa Watumishi wa Jeshi hilo huku akieleza mkataba wa kusambaza teknolojia mbalimbali za nishati safi kati ya Wakala na Jeshi hilo, ulisainiwa mwezi Septemba, mwaka 2024 kwa gharama ya shilingi bilioni 35 kwa Magereza 129 Tanzania Bara.

Chinemba amesema Maafisa wa Magereza wanatakiwa kuwa mabalozi katika utumiaji wa teknolojia za nishati safi kama majiko ya gesi na kuongeza kuwa Wananchi wengi wa maeneo ya vijijini wanakata miti hovyo kwa ajili ya matumizi ya kuni na mkaa.

“Ninawapongeza Jeshi la Magereza kwani wamekuwa vinara wa matumizi ya nishati safi kwenye Magereza yote ukilinganisha na Taasisi nyengine sawa sawa na agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu kuzitaka Taasisi zinazohudumia Watu zaidi ya 100 kutumia nishati safi kama gesi; gesi vunde, mkaa na kuni mbadala”. Alisema Mhandisi, Chinemba.

Chinemba amesema katika utekelezaji wa Mradi huo, REA imechangia shilingi bilioni 26 na Jeshi la Magereza limetoa shilingi bilioni 8 ambapo ushirikiano huo umelenga katika maeneo kadhaa ikiwemo ujenzi wa miundombinu 126 ya bayogesi na majiko banifu 377; Ujenzi wa miundombinu 64 ya LPG na majiko banifu 256; Usambazaji wa mitungi ya gesi 15,126 ya kilo 15 pamoja na majiko ya gesi ya sahani mbili kwa watumishi wote wa Magereza; Usambazaji wa mkaa unaotokana na makaa ya mawe (Rafiki briquettes) tani 850 na majiko banifu 344 kwa kambi 129 za Magereza na maeneo mengineyo.

Naye, Mkuu wa Magereza mkoa wa Shinyanga, Kamishna Msaidizi Mwandamizi, Nobert Ntacho ameishukuru Serikali kupitia REA na kukiri kupokea mitungi ya gesi na majiko ya sahani mbili na kusema familia za Watumishi wa Jeshi hilo, wanakwenda kunufaika ambapo tayari wamepatiwa mafunzo ya matumizi ya nishati safi.

Kwa upande wake, Mkuu wa Gereza wilaya ya Shinyanga; Kamishina Msaidizi, Martin Kunambi amesema Gereza linahudumia mahabusi 263 na kuongeza kuwa walishajenga miundombinu ya kupikia tangu Rais Samia Suluhu Hassan atoe maelekezo ya kuzitaka Taasisi zenye kuhudumia Watu zaidi ya 100 kuacha matumizi ya nishati zisizo safi na salama kama kuni na mkaa na kuhamia kwenye matumizi ya nishati safi na salama

“Tunaipongeza na kuishukuru Serikali, leo tumepokea majiko na mitungi ya gesi ipatayo 221 sawa na idadi ya askari na Watumishi waliopo hapa mkoa wa Shinyanga” amesema Bwana Kunambi.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«September 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
31123456
789
Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

IRINGA, Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini kwa kuendesha mafunzo maalum ya wiki moja yaliyolenga kujenga uwezo wa waendelezaji wa miradi midogo ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower).

Mafunzo hayo yaliyoanza tarehe 7 Septemba, 2026 katika Hoteli ya Sunset mkoani Iringa, yamewakutanisha waendelezaji wa miradi (Developers) zaidi ya 15, hususan kutoka maeneo ya Nyanda za Juu Kusini. Lengo kuu ni kuwajengea uwezo wa kiufundi ili kuongeza ubora wa miradi yao ili iweze kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, tarehe 9 Septemba, 2026, Kaimu Meneja wa Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi kutoka REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya, alisema kuwa REA haishii tu kutoa msaada wa upatikanaji wa nishati vijijini, bali inajikita pia katika kuongeza ujuzi wa wataalamu wa ndani.

"Kuongeza ujuzi kwa waendelezaji hawa kutasaidia kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu na ubora unaohitajika. Hatua hii itaongeza idadi ya miradi inayofikia vigezo vya kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa, kuongeza uzalishaji wa umeme, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii vijijini," alisema Mhandisi Yesaya.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ushirikiano kati ya REA na Wataalamu kutoka Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia (CoET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Maeneo yaliyofundishwa ni pamoja na usanifu wa miradi, upembuzi yakinifu, sayansi ya maji (hydrology), uhandisi wa umeme na elektroniki, pamoja na uendeshaji na matengenezo ya mitambo.

Mbali na mafunzo, REA imebainisha kuwa imekuwa ikisaidia waendelezaji hao kupitia ruzuku za ujenzi, maandalizi ya maandiko ya miradi na usanifu.

Aidha, Wakala huo upo katika mchakato wa kuandaa mfumo wa mikataba ya muda mrefu (Framework Contract) na taasisi za elimu ili kutoa mafunzo endelevu kwenye nishati jadidifu ikiwemo nishati ya jua na mifumo ya gesi vunde.

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wamepongeza mafunzo hayo; akizungumza na Wanahabari, Mhandisi Denis Makoyi kutoka kampuni ya Africa Power Investment, alisema mafunzo hayo yameongeza uelewa mkubwa wa kiufundi katika hatua za utekelezaji wa miradi. Naye Lutengano Kigola kutoka mradi wa Nyalawa Hydropower, aliongeza kuwa mafunzo hayo yanathibitisha kuwa Tanzania ina wataalamu wa ndani wenye uwezo mkubwa wa kuendeleza miradi ya umeme wa maji.

  • MWISHO –

 

Read more
10111213
14
REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuwezesha waendelezaji wadogo wa miradi ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kwa kutoa fedha, msaada wa kitaalamu na mafunzo, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa nishati nchini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top