Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mkurugenzi Mkuu REA Awafunda Wahandisi wa Mikoa
Mohamed Saif 288

Mkurugenzi Mkuu REA Awafunda Wahandisi wa Mikoa

Awakumbusha kuzingatia Sheria, Kanuni na Miongozo

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy amewaelekeza Wasimamizi wa Miradi wa Mikoa kuhakikisha wanaimarisha Mawasiliano na Ushirikiano na wadau mbalimbali kwenye maeneo ya miradi ili kurahisisha utekelezaji wake.

Ametoa maelekezo hayo leo Januari 19, 2026 jijini Dodoma katika kikao chake na Watumishi wa REA wanaohusika na Usimamizi wa Miradi wa Mikoa mara baada ya Kusaini mikataba ya kusambaza umeme katika Vitongoji 9,009 Tanzania Bara.

"Tarehe 17 Januari, 2026 tulisaini mikataba na Wakandarasi ya kusambaza umeme kwenye vitongoji 9,009 na tunaelekea kwenye hatua ya utekelezaji, nimewaiteni hapa ili tukumbushane namna bora ya kuimarisha utendajikazi wetu," amesisitiza Mha. Saidy.

Amesema Watanzania wanayo matumaini na REA na kwamba ni wajibu wao kuhakikisha hawawaangushi kwa kufanya kazi kwa kuzingatia Sheria, Taratibu na Miongozo ya Serikali.

"Imarisheni mawasiliano na ushirikiano na Wabunge, Viongozi wa Mikoa, Wilaya, TANESCO, Wakandarasi, Serikali za Vijiji na Vitongoji pamoja na wanufaika wa miradi," amesisitiza Mha. Saidy

Halikadhalika Mha. Saidy amewasisitiza kuendelea kuwasimamia kwa karibu Wakandarasi wanaotekeleza miradi ya nishati vijijini ikiwemo kuwa na ratiba yao ya kila siku na  kuhakikisha wanatoa taarifa za mara kwa mara kwa viongozi katika ngazi mbalimbali kuanzia vitongoji hadi ngazi ya mkoa ili kuwapa nafasi ya kutambua hatua mbalimbali za utekelezaji wa miradi.

"Hakikisheni mkandarasi anaripoti kwenye uongozi wa kitongoji kabla hajaanza kutekeleza kazi yoyote ya mradi na pia msisitize katika suala la kutoa ajira kwa wananchi eneo la mradi," ameelekeza Mha. Saidy.

Vilevile amewataka kuhakikisha wanawasilisha taarifa za utekelezaji wa miradi kwa viongozi huko walipo kwenye maeneo yao ya miradi ili iweze kujulikana na namna inavyoendelea kutekelezwa ikiwepo kutambua changamoto zilizopo na kuzitafutia suluhisho mapema.

Pia, amewasisitiza kushirikiana na Taasisi zingine za Serikali ili kurahisisha utekelezaji wa miradi hasa ikizingatiwa kuwa mradi unapitia hatua mbalimbali za utekelezaji na kila hatua inakuwa inahitaji ushirikiano na wadau wengine zikiwemo baadhi ya taasisi zinazotekeleza miradi ya maendeleo maeneo ya vitongoji zikiwemo TARURA na TFS.

Kikao hicho kimelenga kujadili namna  bora ya kusimamia utekelezaji wa miradi, hatua zilizofikiwa na mikakati ya kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa ubora na kasi ili ikamilike ndani ya muda.

Share

Print
«September 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
31123456
789
Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

IRINGA, Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini kwa kuendesha mafunzo maalum ya wiki moja yaliyolenga kujenga uwezo wa waendelezaji wa miradi midogo ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower).

Mafunzo hayo yaliyoanza tarehe 7 Septemba, 2026 katika Hoteli ya Sunset mkoani Iringa, yamewakutanisha waendelezaji wa miradi (Developers) zaidi ya 15, hususan kutoka maeneo ya Nyanda za Juu Kusini. Lengo kuu ni kuwajengea uwezo wa kiufundi ili kuongeza ubora wa miradi yao ili iweze kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, tarehe 9 Septemba, 2026, Kaimu Meneja wa Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi kutoka REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya, alisema kuwa REA haishii tu kutoa msaada wa upatikanaji wa nishati vijijini, bali inajikita pia katika kuongeza ujuzi wa wataalamu wa ndani.

"Kuongeza ujuzi kwa waendelezaji hawa kutasaidia kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu na ubora unaohitajika. Hatua hii itaongeza idadi ya miradi inayofikia vigezo vya kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa, kuongeza uzalishaji wa umeme, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii vijijini," alisema Mhandisi Yesaya.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ushirikiano kati ya REA na Wataalamu kutoka Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia (CoET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Maeneo yaliyofundishwa ni pamoja na usanifu wa miradi, upembuzi yakinifu, sayansi ya maji (hydrology), uhandisi wa umeme na elektroniki, pamoja na uendeshaji na matengenezo ya mitambo.

Mbali na mafunzo, REA imebainisha kuwa imekuwa ikisaidia waendelezaji hao kupitia ruzuku za ujenzi, maandalizi ya maandiko ya miradi na usanifu.

Aidha, Wakala huo upo katika mchakato wa kuandaa mfumo wa mikataba ya muda mrefu (Framework Contract) na taasisi za elimu ili kutoa mafunzo endelevu kwenye nishati jadidifu ikiwemo nishati ya jua na mifumo ya gesi vunde.

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wamepongeza mafunzo hayo; akizungumza na Wanahabari, Mhandisi Denis Makoyi kutoka kampuni ya Africa Power Investment, alisema mafunzo hayo yameongeza uelewa mkubwa wa kiufundi katika hatua za utekelezaji wa miradi. Naye Lutengano Kigola kutoka mradi wa Nyalawa Hydropower, aliongeza kuwa mafunzo hayo yanathibitisha kuwa Tanzania ina wataalamu wa ndani wenye uwezo mkubwa wa kuendeleza miradi ya umeme wa maji.

  • MWISHO –

 

Read more
10111213
14
REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuwezesha waendelezaji wadogo wa miradi ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kwa kutoa fedha, msaada wa kitaalamu na mafunzo, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa nishati nchini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top