Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Rais Samia Apeleka Neema ya Umeme Katika Vitongoji Lindi
Mohamed Saif 1

Rais Samia Apeleka Neema ya Umeme Katika Vitongoji Lindi

Zaidi ya Bilioni 25 Kusambaza Umeme Vitongoji 159 Lindi

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa shilingi bilioni 25.8 wa kusambaza umeme katika vitongoji 159 utakaonufaisha kaya 5,116 mkoani Lindi.

Meneja Usimamizi wa Miradi ya Kusambaza Umeme wa REA, Mhandisi Deogratius Nagu amebainisha hayo Januari 27, 2026 mkoani Lindi wakati wa kumtambulisha Mkandarasi Mzawa aliyeshinda zabuni ya kutekeleza mradi huo, Kampuni ya Jaitech Co Ltd kwa ofisi ya mkuu wa mkoa huo.

“Tunamshukuru Rais Mheshimiwa Dkt.Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia kiasi cha shilingi 25,826,594,700.00 kitumike kusambaza umeme katika vitongoji 159 mkoani hapa na leo hii tumefika hapa kumtambulisha Mkandarasi na maandalizi ya awali ya kutekeleza mradi yameanza,” amesema Mhandisi Nagu.

Akizungumzia hali ya usambazaji umeme mkoani humo, Mhandisi Nagu amesema kuwa,vijiji vyote 523 vimefikishiwa umeme na kwamba hadi sasa vitongoji 1,831 vimefikishiwa umeme kati ya vitongoji 2,402.

“REA inaendelea na utekelezaji wa miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji vilivyobaki, hivi tunavyozungumza Wakandarasi wanaendelea na kazi na hadi sasa katika vitongoji hivyo vilivyobaki vitongoji 378 vipo kwenye mpango wa kufikishiwa umeme,” amebainisha.

Amesema, dhamira ya Serikali ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2030 vitongoji vyote nchini viwe vimefikishiwa nishati ya umeme na kwamba REA ikiwa na dhamana hiyo imejipanga kikamilifu kupitia miradi mbalimbali ya kimkakati kufikia dhamira hiyo.

Aidha,Mhandisi Nagu ametoa wito kwa wananchi watakaopitiwa na mradi kuhakikisha wanatoa ushirikiano ili kumuwezesha Mkandarasi kutekeleza kazi ndani ya muda na kwa ubora unaopaswa na kwamba mradi huo unazo faida lukuki kuanzia hatua za awali za utekelezaji hadi hapo utakapokamilika.

Pia, Mhandisi Nagu ameiomba Ofisi ya Mkoa kushirikiana na REA kufikisha elimu na taarifa sahihi kwa wananchi kuwa hakutokuwa na fidia kwa wananchi ambao maeneo yao yatapitiwa na mradi hasa ikizingatiwa kuwa umeme ni fursa ya kiuchumi na kijamii.

“Tunaomba ushirikiano kutoka katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa ili kurahisisha utekelezaji wa mradi ikiwemo kuruhusu mradi kukatiza katika baadhi ya maeneo ya misitu sambamba na kuwa na miundombinu wezeshi kuruhusu kusafirisha vifaa vya mradi maeneo mbalimbali atakapokuwa mkandarasi,” amesema Mha. Nagu.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Katibu Tawala wa mkoa huo, Zuwena Omari ameipongeza REA kwa kuendelea kuenzi kwa vitendo dhamira ya Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kufikisha maendeleo kwa wananchi.

Amesema, Ofisi ya Mkoa wa Lindi itatoa ushirikiano kwa Mkandarasi muda wote wa utekelezaji wa mradi na alimtaka Mkandarasi kuhakikisha anatoa taarifa endapo atakutana na changamoto yoyote.

Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya Jaitech Co Ltd, Isihaka Kibode ameishukuru Serikali kwa kupata kazi  na ameahidi kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa ufanisi na kwamba atashirikiana karibu na viongozi na wananchi wa maeneo ya mradi.

Share

Print
«January 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
2930311234
5678910
Wananchi Kahama Wamshukuru Rais Samia Kuwafikishia Umeme wa REA

Wananchi Kahama Wamshukuru Rais Samia Kuwafikishia Umeme wa REA

Wananchi Kata za Wendele na Mwendakulima Wilaya ya Kahama Mkoani Shinyanga wamemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwawezesha kubadilisha maisha yao kupitia mradi wa umeme uliotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Read more
11
12131415
Serikali Kupitia REA Kuzindua Miradi Mikubwa Ya Kimkakati

Serikali Kupitia REA Kuzindua Miradi Mikubwa Ya Kimkakati

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatarajia kuzindua Kituo cha Kupoza na Kusambaza Umeme cha Mtera na Kusaini Mikataba ya kutekeleza mradi kabambe wa kusambaza umeme kwenye vitongoji 9,009 katika Mikoa yote Tanzania Bara.

Read more
161718
19
Mkurugenzi Mkuu REA Awafunda Wahandisi wa Mikoa

Mkurugenzi Mkuu REA Awafunda Wahandisi wa Mikoa

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mha. Hassan Saidy amewaelekeza Wasimamizi wa Miradi wa Mikoa kuhakikisha wanaimarisha Mawasiliano na Ushirikiano na wadau mbalimbali kwenye maeneo ya miradi ili kurahisisha utekelezaji wake.

Read more
202122232425
2627
Rais Samia Apeleka Neema ya Umeme Katika Vitongoji Lindi

Rais Samia Apeleka Neema ya Umeme Katika Vitongoji Lindi

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mradi wa shilingi bilioni 25.8 wa kusambaza umeme katika vitongoji 159 utakaonufaisha kaya 5,116 Mkoani Lindi.

Read more
282930311
2345678

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top