Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mwenyekiti Bodi Ya REA Atoa Wito Kwa Wananchi Kulinda Miundombinu Ya Umeme
Iddy Mwema 70

Mwenyekiti Bodi Ya REA Atoa Wito Kwa Wananchi Kulinda Miundombinu Ya Umeme

Vijana Maeneo Ya Mradi Wa Umeme Kwenye Vitongoji Kupewa Kipaumbele Kwenye Ajira

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) imetoa wito kwa wananchi kuwa walinzi wa kwanza wa miundombinu ya miradi ya kufikisha umeme vijijini inayotekelezwa na serikali, huku ikieleza kusikitishwa na matukio ya wizi wa vifaa vya umeme ikiwemo waya za mashine umba (transfoma) katika baadhi ya maeneo.

 

Wito huo umetolewa leo Mkoani Manyara na Mwenyekiti wa Bodi ya Nishati Vijijini, Mhe. Balozi Meja Jenerali (Mstaafu), Jacob Kingu wakati akihitimisha ziara ya Bodi hiyo katika mikoa ya Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara ya kukagua utekelezaji wa miradi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) ikiwa ni miradi ya nishati safi ya kupikia pamoja na miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji.

 

Balozi Kingu amesema serikali imetumia fedha nyingi kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya umeme, hivyo ni jukumu la kila mwananchi kushiriki kikamilifu katika kulinda miundombinu hiyo dhidi ya vitendo vya hujuma na wizi vinavyoweza kuchelewesha maendeleo ya wananchi.

 

Katika ziara hiyo mkoani Manyara, Bodi ya REB imefanya kikao na Wakandarasi wanaotekeleza mradi wa kupeleka umeme katika vitongoji ambao ni kampuni ya Sagemcom Energy & Telecom Tanzania pamoja na China Railway Seventh Group.

 

Awali akitoa taarifa ya utekelezaji wa miradi hiyo, Msimamizi wa Miradi wa REA Mkoa wa Manyara, Mhandisi Geofrey Mkeni, amesema serikali kupitia REA imetenga zaidi ya shilingi bilioni 45.8 kwa ajili ya miradi ya kusambaza umeme katika vitongoji 267 vya mkoa wa Manyara.

 

Mhandisi Mkeni amesema miradi hiyo inalenga kuongeza upatikanaji wa huduma ya umeme kwa wananchi wa vijijini ili kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii.

 

Pia ametoa wito kwa wananchi wanaoishi katika maeneo yanayofikiwa na miradi hiyo kuanza kufanya maandalizi ya miundombinu ya ndani ya nyumba ikiwemo wiring ili wawe tayari kuunganishiwa huduma ya umeme mara baada ya miradi hiyo kukamilika.

 

Kwa upande wao, wakandarasi wanaotekeleza miradi hiyo wameahidi kuhakikisha kazi zinakamilika kwa wakati huku wananchi wakinufaika kupitia ajira zinazotokana na utekelezaji wa miradi hiyo.

 

Akizungumza kwa niaba ya kampuni ya Sagemcom Energy & Telecom Tanzania, Afisa Mahusiano ya Jamii na Mazingira, Oliver Charles, amesema miradi hiyo imefungua fursa mbalimbali za ajira kwa vijana wanaoishi katika maeneo yenye miradi ili wawe sehemu ya maendeleo yanayoletwa na serikali.

 

Naye Mhandisi wa Miradi kutoka kampuni ya China Railway Seventh Group, Estheria Fumbuka, amesema kampuni hiyo itaendelea kufanya kazi kwa bidii kuhakikisha miradi yote inakamilika kwa wakati ili malengo ya serikali ya kuwafikishia wananchi huduma ya umeme vijijini yaweze kutimia.

Share

Print
«June 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
25262728293031
12
Bodi, Menejimenti REA Wabadilishana Uzoefu Na Ujumbe Kutoka Algeria

Bodi, Menejimenti REA Wabadilishana Uzoefu Na Ujumbe Kutoka Algeria

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) pamoja na Menejimenti ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wamekutana na kufanya mazungumko na ujumbe kutoka nchini Algeria ukiongozwa na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya GISB Electric ambaye pia ni Makamu wa rais wa Kongani ya Viwanda vya Umeme Algeria (CIEL), Dk. Khelifa Mohammed.

Read more
34567
891011121314
15161718192021
22232425262728
293012345

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top