Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Mkurugenzi Mkuu REA Atoa Wito Kwa Watumishi Kuendelea Kutekeleza Majukumu Yao Kwa Weledi
Mohamed Saif 57

Mkurugenzi Mkuu REA Atoa Wito Kwa Watumishi Kuendelea Kutekeleza Majukumu Yao Kwa Weledi

Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Hassan Saidy amewanasihi watumishi wa wakala kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa kufuata miongozo ya utumishi wa umma kwa kuzingatia sheria, taratibu na kanuni zilizopo.

Ametoa rai hiyo Jijini Dodoma Mei 15, 2026 katika kikao kazi na watumishi wote wa Wakala ambapo amewanasihi kuimarisha usimamizi wa miradi na kuwa sehemu ya miradi sambamba na kuimarisha mawasiliano na viongozi wa Serikali maeneo ya mradi.

“Tusirudi nyuma, tusilewe sifa tufikirie mambo makubwa zaidi. Tuwe wabunifu, tuchape kazi kwa weledi na ushirikiano na hii ndiyo nguzo itakayofanya tuendelee kusonga mbele,” amesema Mha. Saidy.

Mha. Saidy amesema Wakala umejipanga kuhakikisha miradi yote ya kusambaza nishati vijijini inakamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakikana.

Katika kikao kazi hicho, watumishi walipata fursa ya kujadili masuala mbalimbali yanayolenga kuimarisha utendaji wa kazi, kukumbushana kuhusu miongozo mbalimbali ya utumishi wa umma pamoja na kupima afya zao kwa kuwa afya ni msingi wa ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao.

Wakati huohuo; Madaktari kutoka Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete kwa mwaliko maalum wa Menejimenti ya REA wameendesha zoezi la upimaji wa magonjwa yasiyoambukiza (moyo; homa ya ini na ugonjwa wa kisukari).

Zoezi hilo lilienda sambamba na utoaji wa chanjo ya kujikinga na ugonjwa wa homa ya ini ambapo Zaidi ya Watumishi 100 walipata huduma hiyo ya kinga.

Share

Print
«June 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
25262728293031
12
Bodi, Menejimenti REA Wabadilishana Uzoefu Na Ujumbe Kutoka Algeria

Bodi, Menejimenti REA Wabadilishana Uzoefu Na Ujumbe Kutoka Algeria

Bodi ya Nishati Vijijini (REB) pamoja na Menejimenti ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wamekutana na kufanya mazungumko na ujumbe kutoka nchini Algeria ukiongozwa na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya GISB Electric ambaye pia ni Makamu wa rais wa Kongani ya Viwanda vya Umeme Algeria (CIEL), Dk. Khelifa Mohammed.

Read more
34567
891011121314
15161718192021
22232425262728
293012345

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top