Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Naibu Waziri Maji Nishati na Madini Zanzibar aipa kongole REA
Frank A. Mugogo 804

Naibu Waziri Maji Nishati na Madini Zanzibar aipa kongole REA

Naibu Waziri Wizara ya Maji Nishati na Madini Zanzibar, Zawadi Nassor ameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa hatua unazochukua, mikakati na mipango inayoendelea nayo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi za Kupikia.

Ametoa pongezi hizo Agosti 24, 2024 baada ya kutembelea Banda la Wakala katika Maonesho ya Kizimkazi yanayofanyikia Kizimkazi Dimbani Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.

"Tulichokishuhudia hapa na maelezo tuliyopata tumehamasika na tutakaa na pacha wetu kwa maana ya Wizara ya Nishati Bara ili tuone ni vipi nasisi tunaweza kuhamasisha wananchi wetu kutumia Nishati Safi ya Kupikia na kuachana na kuni," amesema Zawadi.

Alibainisha kuwa kufika kwake katika Banda la REA kumemuongezea uelewa wa uwepo wa baadhi ya bidhaa za Nishati Safi za Kupikia ambazo hajapata kuziona hapo kabla ambazo alisema kwa ufanisi wake ametamani ziwafikie wananchi wengi zaidi visiwani humo.

"Baadhi ya majiko hapa sikuwahi kuyaona hapo kabla, lakini kufika hapa nimejionea na nimeshuhudia namna yanavyofanya kazi, yanahamasisha; ni muhimu sasa nasi tukashirikiana na wadau na tukaongeza kasi ya kuhamasisha wananchi," alisema.

Alisema kwa upande wa Bara tayari mwamko wa matumizi ya bidhaa za Nishati Safi za Kupikia ni mkubwa ikilinganishwa na Zanzibar na alitoa wito kwa watengenezaji, wawekezaji, wauzaji na wasambazaji wa bidhaa hizo kuwekeza Zanzibar ili kusogeza huduma kwa wananchi.

"Tutashirikiana kwa karibu na Wizara ya Nishati Bara ili kuona namna bora ya kusogeza bidhaa hizi kwa wananchi sambamba na kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwani wenzetu tayari wamepiga hatua," alisema. 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala kutoka REA, Mhandisi Advera Mwijage alimueleza Naibu Waziri huyo majukumu ya Wakala na hatua zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali kupitia Wakala na wadau wengine ili kuhamasisha wananchi kutumia bidhaa za Nishati Safi za Kupikia. 

"Kwa sasa tunatekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 2024-2034 ambao ulizinduliwa Mwezi Mei mwaka huu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambao umesisitiza kuwa kufikia 2034 asilimia 80 ya wananchi wawe wanatumia Nishati Safi ya Kupikia," alisema Mhandisi Advera.

Akizungumzia ushirikiano na mchango wa Serikali kupitia REA kwa wadau wa bidhaa za Nishati Safi za Kupikia Mhandisi Advera alisema REA inawawezesha kifedha wauzaji, watengenezaji na wasambazaji wa bidhaa za Nishati Safi za Kupikia kwa namna mbalimbali ikiwemo utoaji wa ruzuku kwa lengo la kuhakikisha kila mwananchi anamudu gharama na pia kuhakikisha kila eneo linafikiwa na huduma. 

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«September 2026»
MonTueWedThuFriSatSun
31123456
789
Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

Rea Yawajengea Uwezo Waendelezaji wa Miradi Midogo ya Umeme Unaozalishwa na Maporomoko ya Maji

IRINGA, Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuimarisha upatikanaji wa nishati nchini kwa kuendesha mafunzo maalum ya wiki moja yaliyolenga kujenga uwezo wa waendelezaji wa miradi midogo ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower).

Mafunzo hayo yaliyoanza tarehe 7 Septemba, 2026 katika Hoteli ya Sunset mkoani Iringa, yamewakutanisha waendelezaji wa miradi (Developers) zaidi ya 15, hususan kutoka maeneo ya Nyanda za Juu Kusini. Lengo kuu ni kuwajengea uwezo wa kiufundi ili kuongeza ubora wa miradi yao ili iweze kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa kupitia Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, tarehe 9 Septemba, 2026, Kaimu Meneja wa Usaidizi wa Kiufundi kwa Waendelezaji Miradi kutoka REA, Mhandisi Emmanuel Yesaya, alisema kuwa REA haishii tu kutoa msaada wa upatikanaji wa nishati vijijini, bali inajikita pia katika kuongeza ujuzi wa wataalamu wa ndani.

"Kuongeza ujuzi kwa waendelezaji hawa kutasaidia kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia viwango vya kitaalamu na ubora unaohitajika. Hatua hii itaongeza idadi ya miradi inayofikia vigezo vya kuunganishwa kwenye Gridi ya Taifa, kuongeza uzalishaji wa umeme, na kuchochea maendeleo ya kiuchumi na kijamii vijijini," alisema Mhandisi Yesaya.

Mafunzo hayo yameendeshwa kwa ushirikiano kati ya REA na Wataalamu kutoka Ndaki ya Uhandisi na Teknolojia (CoET) ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM). Maeneo yaliyofundishwa ni pamoja na usanifu wa miradi, upembuzi yakinifu, sayansi ya maji (hydrology), uhandisi wa umeme na elektroniki, pamoja na uendeshaji na matengenezo ya mitambo.

Mbali na mafunzo, REA imebainisha kuwa imekuwa ikisaidia waendelezaji hao kupitia ruzuku za ujenzi, maandalizi ya maandiko ya miradi na usanifu.

Aidha, Wakala huo upo katika mchakato wa kuandaa mfumo wa mikataba ya muda mrefu (Framework Contract) na taasisi za elimu ili kutoa mafunzo endelevu kwenye nishati jadidifu ikiwemo nishati ya jua na mifumo ya gesi vunde.

Kwa upande wao, baadhi ya washiriki wamepongeza mafunzo hayo; akizungumza na Wanahabari, Mhandisi Denis Makoyi kutoka kampuni ya Africa Power Investment, alisema mafunzo hayo yameongeza uelewa mkubwa wa kiufundi katika hatua za utekelezaji wa miradi. Naye Lutengano Kigola kutoka mradi wa Nyalawa Hydropower, aliongeza kuwa mafunzo hayo yanathibitisha kuwa Tanzania ina wataalamu wa ndani wenye uwezo mkubwa wa kuendeleza miradi ya umeme wa maji.

  • MWISHO –

 

Read more
10111213
14
REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

REA Yaendelea Kuwezesha Miradi ya Umeme wa Maji Nyanda za Juu Kusini

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umeendelea kuwezesha waendelezaji wadogo wa miradi ya uzalishaji wa umeme unaotokana na maporomoko ya maji (Small Hydropower) katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini kwa kutoa fedha, msaada wa kitaalamu na mafunzo, hatua inayolenga kuongeza uzalishaji wa nishati nchini.

Read more
151617181920
21222324252627
2829301234
567891011

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top