Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Naibu Waziri Maji Nishati na Madini Zanzibar aipa kongole REA
Frank A. Mugogo 99

Naibu Waziri Maji Nishati na Madini Zanzibar aipa kongole REA

Naibu Waziri Wizara ya Maji Nishati na Madini Zanzibar, Zawadi Nassor ameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa hatua unazochukua, mikakati na mipango inayoendelea nayo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi za Kupikia.

Ametoa pongezi hizo Agosti 24, 2024 baada ya kutembelea Banda la Wakala katika Maonesho ya Kizimkazi yanayofanyikia Kizimkazi Dimbani Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.

"Tulichokishuhudia hapa na maelezo tuliyopata tumehamasika na tutakaa na pacha wetu kwa maana ya Wizara ya Nishati Bara ili tuone ni vipi nasisi tunaweza kuhamasisha wananchi wetu kutumia Nishati Safi ya Kupikia na kuachana na kuni," amesema Zawadi.

Alibainisha kuwa kufika kwake katika Banda la REA kumemuongezea uelewa wa uwepo wa baadhi ya bidhaa za Nishati Safi za Kupikia ambazo hajapata kuziona hapo kabla ambazo alisema kwa ufanisi wake ametamani ziwafikie wananchi wengi zaidi visiwani humo.

"Baadhi ya majiko hapa sikuwahi kuyaona hapo kabla, lakini kufika hapa nimejionea na nimeshuhudia namna yanavyofanya kazi, yanahamasisha; ni muhimu sasa nasi tukashirikiana na wadau na tukaongeza kasi ya kuhamasisha wananchi," alisema.

Alisema kwa upande wa Bara tayari mwamko wa matumizi ya bidhaa za Nishati Safi za Kupikia ni mkubwa ikilinganishwa na Zanzibar na alitoa wito kwa watengenezaji, wawekezaji, wauzaji na wasambazaji wa bidhaa hizo kuwekeza Zanzibar ili kusogeza huduma kwa wananchi.

"Tutashirikiana kwa karibu na Wizara ya Nishati Bara ili kuona namna bora ya kusogeza bidhaa hizi kwa wananchi sambamba na kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwani wenzetu tayari wamepiga hatua," alisema. 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala kutoka REA, Mhandisi Advera Mwijage alimueleza Naibu Waziri huyo majukumu ya Wakala na hatua zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali kupitia Wakala na wadau wengine ili kuhamasisha wananchi kutumia bidhaa za Nishati Safi za Kupikia. 

"Kwa sasa tunatekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 2024-2034 ambao ulizinduliwa Mwezi Mei mwaka huu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambao umesisitiza kuwa kufikia 2034 asilimia 80 ya wananchi wawe wanatumia Nishati Safi ya Kupikia," alisema Mhandisi Advera.

Akizungumzia ushirikiano na mchango wa Serikali kupitia REA kwa wadau wa bidhaa za Nishati Safi za Kupikia Mhandisi Advera alisema REA inawawezesha kifedha wauzaji, watengenezaji na wasambazaji wa bidhaa za Nishati Safi za Kupikia kwa namna mbalimbali ikiwemo utoaji wa ruzuku kwa lengo la kuhakikisha kila mwananchi anamudu gharama na pia kuhakikisha kila eneo linafikiwa na huduma. 

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«March 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
242526272812
3456
Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Arusha Wavutiwa na Bidhaa za Nishati Safi ya Kupikia

Wananchi Jijini Arusha wamevutiwa na bidhaa mbalimbali za Nishati Safi ya Kupikia na wameipongeza Serikali kwa kuona umuhimu wa kufikisha bidhaa hizo katika Maonesho yanayoendelea mkoani humo kuelekea Siku ya Wanawake Duniani.

Read more
789
10
Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake REA Washiriki Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Jijini Arusha

Watumishi Wanawake wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) wameshiriki katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika Kitaifa Jijini Arusha Machi 8, 2025.

Read more
111213141516
171819
Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini Yahitimisha Ziara ya Ukaguzi wa Miradi ya Umeme Mkoani Njombe

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imekamilisha ziara yake ya siku tatu mkoani Njombe kwa kukagua utekelezaji wa miradi ya Nishati Vijijini (REA) inayotekelezwa na serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa kushirikiana na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO). Kwa upande wa REA ziara hiyo imehitimishwa katika kijiji cha Welela, Jimbo la Lupembe, ambapo kamati hiyo imepongeza juhudi zinazofanywa na Serikali kuhakikisha umeme unawafikia wananchi wa vijijini kwa kasi inayostahili.

Read more
20212223
24252627282930
31123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top