Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
Naibu Waziri Maji Nishati na Madini Zanzibar aipa kongole REA
Frank A. Mugogo 25

Naibu Waziri Maji Nishati na Madini Zanzibar aipa kongole REA

Naibu Waziri Wizara ya Maji Nishati na Madini Zanzibar, Zawadi Nassor ameupongeza Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kwa hatua unazochukua, mikakati na mipango inayoendelea nayo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi za Kupikia.

Ametoa pongezi hizo Agosti 24, 2024 baada ya kutembelea Banda la Wakala katika Maonesho ya Kizimkazi yanayofanyikia Kizimkazi Dimbani Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.

"Tulichokishuhudia hapa na maelezo tuliyopata tumehamasika na tutakaa na pacha wetu kwa maana ya Wizara ya Nishati Bara ili tuone ni vipi nasisi tunaweza kuhamasisha wananchi wetu kutumia Nishati Safi ya Kupikia na kuachana na kuni," amesema Zawadi.

Alibainisha kuwa kufika kwake katika Banda la REA kumemuongezea uelewa wa uwepo wa baadhi ya bidhaa za Nishati Safi za Kupikia ambazo hajapata kuziona hapo kabla ambazo alisema kwa ufanisi wake ametamani ziwafikie wananchi wengi zaidi visiwani humo.

"Baadhi ya majiko hapa sikuwahi kuyaona hapo kabla, lakini kufika hapa nimejionea na nimeshuhudia namna yanavyofanya kazi, yanahamasisha; ni muhimu sasa nasi tukashirikiana na wadau na tukaongeza kasi ya kuhamasisha wananchi," alisema.

Alisema kwa upande wa Bara tayari mwamko wa matumizi ya bidhaa za Nishati Safi za Kupikia ni mkubwa ikilinganishwa na Zanzibar na alitoa wito kwa watengenezaji, wawekezaji, wauzaji na wasambazaji wa bidhaa hizo kuwekeza Zanzibar ili kusogeza huduma kwa wananchi.

"Tutashirikiana kwa karibu na Wizara ya Nishati Bara ili kuona namna bora ya kusogeza bidhaa hizi kwa wananchi sambamba na kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwani wenzetu tayari wamepiga hatua," alisema. 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala kutoka REA, Mhandisi Advera Mwijage alimueleza Naibu Waziri huyo majukumu ya Wakala na hatua zinazoendelea kuchukuliwa na Serikali kupitia Wakala na wadau wengine ili kuhamasisha wananchi kutumia bidhaa za Nishati Safi za Kupikia. 

"Kwa sasa tunatekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia 2024-2034 ambao ulizinduliwa Mwezi Mei mwaka huu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambao umesisitiza kuwa kufikia 2034 asilimia 80 ya wananchi wawe wanatumia Nishati Safi ya Kupikia," alisema Mhandisi Advera.

Akizungumzia ushirikiano na mchango wa Serikali kupitia REA kwa wadau wa bidhaa za Nishati Safi za Kupikia Mhandisi Advera alisema REA inawawezesha kifedha wauzaji, watengenezaji na wasambazaji wa bidhaa za Nishati Safi za Kupikia kwa namna mbalimbali ikiwemo utoaji wa ruzuku kwa lengo la kuhakikisha kila mwananchi anamudu gharama na pia kuhakikisha kila eneo linafikiwa na huduma. 

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«September 2024»
MonTueWedThuFriSatSun
26
REA yamtaka mwendelezaji wa mradi wa kufua umeme wa Maguta mkoani Iringa kuongeza kasi

REA yamtaka mwendelezaji wa mradi wa kufua umeme wa Maguta mkoani Iringa kuongeza kasi

Serikali imemtaka Mwendelezaji wa Mradi wa kufua umeme kwa kutumia maporomoko ya maji wa Maguta  uliopo katika Kijiji cha Masisiwe Wilayani Kilolo Mkoani Iringa kuukamilisha kwa wakati.

Read more
27
Wananchi waaswa kutunza mazingira

Wananchi waaswa kutunza mazingira

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewaasa wananchi kutunza mazingira na kulinda miundombinu pamoja na vyanzo vya maji ili kuendelea kupata huduma ya umeme pamoja na kuwa na miradi endelevu ya kufua umeme.

Read more
282930311
2345678
9101112
EXTENDED DEADLINE FOR INVITATION FOR PROPOSALS - Supply of Starter Packs of LPG for Prison Staffs in Areas of Rural Mainland Tanzania

EXTENDED DEADLINE FOR INVITATION FOR PROPOSALS - Supply of Starter Packs of LPG for Prison Staffs in Areas of Rural Mainland Tanzania

The Government of Tanzania through the Rural Energy Agency (REA) in collaboration with Tanzania Prisons Services (TPS) in response to attainment of sustainable development goals, has opened a   financing   window to support distribution of 15,920 units of 15kg LPG Starter Packs to earmarked Staffs in all Tanzania Prisons. This is part of the Clean Cooking Packages that the parties have agreed to cooperate inorder to enable these institutions to stop using environmentally and healthily harmful cooking solutions.

Read more
131415
16171819202122
23242526272829
30123456

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
PSSSF Building, 7th Floor
Makole Road
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top