Social Links Search User Login Menu
Tools
Close
Close
REA yamtaka mwendelezaji wa mradi wa kufua umeme wa Maguta mkoani Iringa kuongeza kasi
Frank A. Mugogo 133

REA yamtaka mwendelezaji wa mradi wa kufua umeme wa Maguta mkoani Iringa kuongeza kasi

Serikali imemtaka Mwendelezaji wa Mradi wa kufua umeme kwa kutumia maporomoko ya maji wa Maguta  uliopo katika Kijiji cha Masisiwe Wilayani Kilolo Mkoani Iringa kuukamilisha kwa wakati.

Mkurugenzi wa Teknolojia za Nishati Jadidifu na Mbadala kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA), Mhandisi Advera Mwijage ametoa maelekezo hayo Agosti 26, 2024 alipofanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa mradi huo ambao umefikia asilimia 95.

Mradi unatekelezwa na Mkandarasi ZECO ambaye Makao Makuu yake yapo Nchini Italia. Mwendelezaji ametakiwa kuhakikisha makubaliano ya utekelezaji wa mradi kati yake na  ZECO yanatekelezwa kwa wakati ili mradi ukamike ifikapo Desemba 2024. 

"Hatua iliyofikiwa inaridhisha; hakuna kikwazo kinachosababisha mradi uchelewe, Mkandarasi anapaswa kuhakikisha ifikapo Desemba mwaka huu awe amekamilisha na umeme umeingia kwenye Gridi ya Taifa," ameelekeza Mhandisi Advera. 

Mhandisi Advera amefafanua kuwa mradi umesanifiwa kuzalisha Megawati 2.4 na kwamba unatekelezwa kwa awamu ambapo awamu ya kwanza inayoendelea hivi sasa itazalisha megawati 1.2. 
Amesema licha ya kuongeza umeme kwenye Gridi ya Taifa, mradi utazalisha ajira kwa wananchi wa eneo la mradi, utapunguza uzalishaji wa hewa ya ukaa, ni rafiki kwa mazingira, utaimarisha hali ya upatikanaji wa umeme kwenye maeneo mengi na hivyo kuleta chachu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwa wananchi wa Kilolo na maeneo mengine. 

"Kukamilika kwa mradi huu kutakuwa na manufaa makubwa kwa wananchi wa maeneo haya na maeneo mengine pia; umeme ni injini ya uchumi hivyo tunatarajia kuona maendeleo makubwa baada ya kuanza uzalishaji wa umeme," amesema. 
Mhandisi Advera amebainisha kuwa mradi unatumia Nishati Safi na Salama kutokana na maporomoko ya maji hivyo ili uwe endelevu ametoa wito kwa kila mwananchi kulinda na kutunza mazingira ya maeneo ya vyanzo vya maji. 

"Umeme unaokwenda kuzalishwa hapa ni wa maporomoko ya maji, sasa tusipolinda mazingira yanayozunguka hivi vyanzo vya maji yaani hii Mito tutasababisha mradi ushindwe kutupa matokeo tunayoyatarajia," amesisitiza Mhandisi Advera. 

Akizungumzia utekelezaji wa mradi kwa ujumla, msimamizi wa mradi ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Lung'ali Natural Resources Co. Ltd inayosimamia mradi huo kwa niaba ya Kanisa Katoliki-Parokia ya Jimbo la Iringa, Padri Luciano Mpoma ameishukuru Serikali kwa mchango wake katika kuhakikisha mradi unakamilika. 

Amesema mradi unatekelezwa kwa ufadhili wa Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Benki ya Uwekezaji Tanzania (TIB) pamoja na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuendeleza Mitaji kwa ajili ya Maendeleo (UNCDF). 

"REA imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha mradi unafanikiwa na unaleta manufaa yanayokusudiwa. Mara zote wamefika hapa kukagua na kutushauri tunawashukuru sana," amepongeza.

Miongoni mwa majukumu ya msingi ya REA ni pamoja na kuwezesha ujenzi wa miradi ya kuzalisha umeme kwa kutumia nishati Jadidifu ambayo ni Nishati Safi na Salama.

Imetolewa na:

Mkurugenzi Mkuu
Wakala wa Nishati Vijijini
Jengo la REA
28 Mtaa wa Medeli
Dodoma

Share

Print
«July 2025»
MonTueWedThuFriSatSun
30
REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

REA Yasambaza Mitungi na Majiko ya Gesi kwa Watumishi wa Gereza la Ukonga Dar es Salaam

Serikali imesambaza kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza (Gereza la Ukonga) mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko yake 464 ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kama njia ya utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya kupikia nchini ambapo msisitizo ni angalau asilimia 80 ya Watanzania wawe wanatumia Nishati Safi ifikapo Mwaka 2034.

Read more
1
Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Mhe. Rais Samia Apongezwa Kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia kwa Vitendo

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amepongezwa kwa kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kwa vitendo.

Read more
2
REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

REA Yasambaza Mitungi, Majiko ya Gesi kwa Watumishi 461 wa Magereza Mkoa wa Mara

Katika kuendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imegawa jumla ya mitungi ya gesi ya kilogramu 15 pamoja na majiko ya sahani mbili 461 kwa Watumishi wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Mara.

Read more
3
REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

REA Yaja na Mpango Kabambe wa Kuwezesha Ujenzi wa Vituo vya Mafuta Vijijini

Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inatekeleza mpango wa kuwezesha ujenzi na uendeshaji wa vituo vipya vidogo vya gharama nafuu vya bidhaa za mafuta (petrol na dizeli) maeneo ya vijijini ili kuondoa madhara yatokanayo na njia zisizo salama.

Read more
4
Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Watanzania Watakiwa Kuachana na Dhana Potofu Kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni Gharama

Wakala wa Nishati Vijijini (REA) umewasihi Watanzania kote nchini kuachana na dhana ya kwamba Nishati Safi ya Kupikia ni gharama ikilinganishwa na matumizi ya kuni na mkaa.

Read more
5
Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Vitongoji Vyote 64,359 Vitakuwa na Umeme Ifikapo 2030

Imeelezwa kuwa hadi kufikia mwaka 2030 vitongoji vyote Tanzania Bara vitakuwa vimefikishiwa nishati ya umeme kupitia miradi mbalimbali inayotekelezwa na kusimamiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

Read more
6
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031123
45678910

Archive

Contact Us

E-Mail
General Information:  info@rea.go.tz
Director General:  dg@rea.go.tz
Procurement (PMU):  pmu@rea.go.tz
Webmaster:  webmaster@rea.go.tz

Mailing Address

Director General
Rural Energy Agency - REA
REA Building
28 Medeli Street
P. O. Box 2153
Dodoma, Tanzania

Phone & Fax

Tel: +255 26 2323504, +255 26 2323506
+255 26 2323507
Fax: +255 26 2323507

Time Zone

Please note that we are based in Tanzania, Time zone (GMT+03:00). Although we may not be in office at times convenient for all international enquiries, we do monitor our e-mail outside normal office hours.

Back To Top